Barua ya wazi kwa Rais Samia Suluhu Hassan kuhusu hali ya haki jinai nchini

Mkuu haya mambo yanakemewa sana,Fuatilia hotuba ya raisi wa TLS ya mwaka jana kwenye siku ya sheria utaona ina mambo mengi tu yalizungumzwa mle ila watawala hawajali,nadhani labda wabadili mbinu ya kuyafikisha
Kweli kabisa CCM wanawadharau sana wataalam wetu, lakini mambo haya yakisemwa na mashirika ya kimataifa ya haki za binadamu watajifikiria mara mbili tatu.
 
Tito Magoti, Pole sana kwa yaliyokupata Ila huwezi jua kwanini Mungu akaacha ukapata majanga haya.

Kwa akili yangu, Mungu alitaka uende ukaone jinsi raia wanavyoteseka na mfumo mbovu wa Sheria na haki nchini. Wewe ndiyo sauti yao.

Hata Kama Rais SSH hataliona hili, Mimi ninaliona ni zaidi ya Thesis ya Masters/ PhD.

Nakushauri ulisimamie kwa kutafuta wahisani watakao ku-support uwasemee wasio na sauti kupitia Asasi za Kiraia.

Mungu akubariki sana
 
Farolito Asante kwa kurahisisha andiko la Tito Magoti, ni rahisi kufollow hata kwa sisi lay men
 

Wasomi wengi wa Tanzania wakishangia kwenye madaraka wanakuwa hopeless. Jaribu kuangalia kila Kabudi, Kitila Mkumbo, Bashiru nk, walichokuwa wanaongea kabla ya kupata madaraka na wanachoongea baada ya kupata madaraka.
 
Correct.
 
Nje ya mada, Tito umejiunga hapa JF mwaka 2014 lakini una post chini ya 10! Naona umeona wapi unaweza weka gazeti lako ukaona ni hapa JF, kisha unaenda kushinda Twitter.

Huu mchezo anao Zitto, naye huleta post zake ndefu kisha anakuwa kama karushia mbwa, halafu anaenda zake kushinda Twitter bila kujibu lolote kwenye bandiko lake.

Tito jirekebishe kwa hilo.
 
Mkuu haya mambo yanakemewa sana,Fuatilia hotuba ya raisi wa TLS ya mwaka jana kwenye siku ya sheria utaona ina mambo mengi tu yalizungumzwa mle ila watawala hawajali,nadhani labda wabadili mbinu ya kuyafikisha

Viongozi wa kiafrika huwa hawajali malalamiko yanayotolewa kwa njia ya amani/kistaarabu, njia wanayoilewa viongozi wengi wa kiafrika ni ya maandamano, migomo au machafuko.

Haya madai ya Tito haijalishi yana ukweli kiasi gani, ili mradi yametolewa kwa njia ya kistaarabu, kwao hayana uzito wowote.

Kwa njia hii ya maelezo ya kistaarabu bila maandamano ama mgomo, yataandikwa hata miaka 100 bila kufanyiwa kazi.
 
tindo, yawezekana anayo ID nyingine kama ya kwako na Mimi hapa anayoitumia. Mara nyingine ID ya NIDA haikupi uhuru wa kujiachia kama mimi na wewe tunavyojiachia. Just thinking aloud
 
Umeeleza vizuri, ninachoona DPP ndo chanzo cha matatizo yote, kuanzia mlundikano wa mahabusu magerezani, hadi ukosefu wa dhamana kwa watuhumiwa, DPP apunguziwe mamlaka zaidi, mahakama iwe ndo mwamuzi wa mwisho kuhusu dhamana za washtakiwa
 
tindo, yawezekana anayo ID nyingine kama ya kwako na Mimi hapa anayoitumia. Mara nyingine ID ya NIDA haikupi uhuru wa kujiachia kama mimi na wewe tunavyojiachia. Just thinking aloud

Sikatai usemacho, lakini mimi nimetolea angalizo hii Id yake verified. 2014 ilikuwa dhalimu hajaingia madarakani, mbona nayo michango ni michache mpaka 2015?
 
Hili andiko ni bora sana. Yanahitajika mageuzi makubwa mno. Ikibidi kiwepo chombo huru cha kufatilia haki za mahabusu. Bora zitungwe sheria kali kwa wataobainika kuvunja hayo wasiyopenda lakini si kuumiza watu. Pole sana Tito
haya ndiiyo mambo yamefanya hasira ya mungu kuwaka na kumwondoa mfalme
 
Duuh...! Asante kwa barua nzuri,na yenye mafunzo na masuruhisho. Mpaka mwili umesisimka. Unaweza ukadhani tuko huru tunatamba mitaani kumbe ukiingia kwenye 18 za watu fulani fulani,bora ya jehanum
 
Hili andiko ni bora sana. Yanahitajika mageuzi makubwa mno. Ikibidi kiwepo chombo huru cha kufatilia haki za mahabusu. Bora zitungwe sheria kali kwa wataobainika kuvunja hayo wasiyopenda lakini si kuumiza watu. Pole sana Tito
Moyo umeniuma sana kusoma hili andika
 
Uko sahihi nadhani mbinu ibadilike
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…