Uchaguzi 2020 Barua ya Wazi kwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kuhusu Mwenendo wa Kampeni za Uchaguzi Mkuu (2020) za Mheshimiwa Tundu Lissu

Hajayaona yote hayo, kaliona na Lissu tu kufafanua Muungano wa Tanganyika
 
Hadi hao wafugaji watakuwa wameshangazwa na Lissu badala ya kuwaambia walau atawatengea sehemu ya misitu ya akiba watumie kwa shughuli zao; yeye anadai akichaguliwa wataenda kulisha mifugo mbugani kabisa kwa raha zao.

Imagine hali ya NEC na vyombo vya ulinzi tangia ameingia Tanzania kuanzia kuvunja kanuni za uchaguzi kwa kuanza campaign mapema, uhamasishaji wa ghasia, mara sijui anataka kutengenezewa ajali ya ndege na jana kaja na hoja za kuvunja muungano nina uhakika huko NEC washamchoka huyo Lissu kwa sasa awajui wafanye nae nini.
 
Point hapo ni " Uchaguzi wa huru a haki". Ikitokea umeona hujatendewa haki basi Kuna njia za kisheria za kufuata na sio kumwaga damu ya wananchi

Wizi mkubwa ni kwenye kura za urais, njia za kisheria baada ya kuibiwa ni zipi? Bila machafuko sioni mabadiliko ya maeneo yanayolalamikiwa.
 
Kakojoe ukalale ila barua kwa Tume ya Uchaguzi ya Magufuli imefika amekabidhiwa yeye mwenyewe. Ila akiishughulikia na yeye atashughulikiwa
 
We binti jiheshimu basi
 

Hivi nawewe unajihesabu unaakili timamu?

Nizaidi ya kichaa
 
Nimeongelea suala la kuhatarisha amani ya nchi na kupelekea machafuko

Amani ni zao la haki, tendeni haki ili watu wakiingia barabarani waingie kwa shughuli zao binafsi za matumizi ya barabara na si vinginenvyo.

BTW, nafasi zimejaa sana sijui unalenga nafasi ipi ya uteuzi ili tukuangalizie kama ipo. Lakini pia muwe mnakumbuka kurudisha feedback kwa Polepole kumwambia kuwa mapokezi ya mabandiko yenu kwenye social media mbalimbali hayapokelewi vizuri, mwambieni kuwa mnakula za uso kwelikweli, sababu watu wengi wanajielewa sana, labda mjaribu kumuomba kuelekeza nguvu kubwa vijijini.
 
Kwa kweli kampeni zake zinapandikiza chuki,woga na kuchochea vita.ni bahati mbaya kuwa na mgombea wa namna hii.sijui taifa litafanyeje kuunganisha wananchi ambao amewatawanya kwa kiwajaza chuki zisizo na msingi.
 
Ila tuseme ukweli Lissu anaushawishi wa kumfanya mtu aingie barabarani ujue! Nimemwelewa sana huyu mtoa mada. Lissu ni habari nyingine kwa ushawishi. Ujue twaweza kwenda kumfurusha mtu ofisini!

Ila lakini ukweli huw sielewi kwa nini mgombea urais wa zanzibar anachaguliwa na wajumbe toka huku Tanzania Bara (Tanganyika) wakati alipaswa achaguliwe na wajumbe toka Zanzibar pekeee. Hapa haijakaa vizuri.
 
Niwe mkweli kwamba tangu Lissu aanze kampeni nimetokea kumchukia Jiwe kupita maelezo kiasi kwamba akikatiza jirani yangu naweza mnasa kibao. Lissu anaushawishi wa ajabu sana! Sielewi kwa nini. Hapa nilipo namwona Jiwe ni muuaji, katili, jasusi, na kumwona hatofautiani na Idd Amin yule wa Uganda. Kwa kweli mleta hoja umeon mbali sana. Watu wanamchukulia poa Lissu, hapana, ana ushawishi wa ajabu sana!
 
Mimi siko pamoja na wewe kubagua watanzania wenzetu kwa kigezo cha mahali wanapoingia.

Huko kijijini unapopadharau ndiko kunakokupatia chakula chako.
 

Hiyo ya kwamba matokeo ya urais yakishatangazwa hakuna kupingwa haikubaliki, na ni kilio chetu cha muda mrefu. Sasa acha tupambane maana ccm hamko tayari hicho kifungu kiondolewe wakati hamuheshimu kura za wananchi.
 
UKOSEFU WA UMAKINI UMEFANYA MADA HII KUWA KITUKO CHA SIKU!!
Nadhani ukitulia waweza andika vema ila nadhani bado unateswa na Lisuphobia...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…