Barua ya wazi kwa Tundu Lissu kumuonya dhidi ya kutetea masikini na wapumbavu

Barua ya wazi kwa Tundu Lissu kumuonya dhidi ya kutetea masikini na wapumbavu

Aisee nakwenda kuihibiri hii madhabuhi kanisaniii ila sitaiweka ktk mlengo wa Ki Lisu bali kwa wapumbavu na wajinga. Najua watakuwepo watapasuka mbavu tu kwa vicheko.
 
Fikira Fikirini
Wazo Wazeni
Ubongo umesizi
Akili imedoda
Nimechoka

Bazazi
 
BARUA YA WAZI KWA TUNDU LISU

Na, Robert Heriel
Taikon wa Fasihi,
S.L.P 9977, JIBI,
Kutoka Nyota ya Tibeli.
30, 07. 2020.

YAH: KUKUONYA DHIDI YA KUTETEA MASIKINI NA WAPUMBAVU.

Ndugu Mhe Lisu, Kichwa cha habari hapo juu cha husika.

Ninafuraha kubwa kukuandikia barua hii ya wazi ambapo najua watu wengi wataisoma nawe itakufikia. Utanisamehe ikiwa njia hii niliyoitumia pengine isikufurahishe lakini ni katika hali ya kukupa ujumbe wenye manufaa wewe na wale wote wenye tabia kama zako, mimi nikiwa mmoja wao.

Mhe. Lisu, nimekufuatilia kwa miaka saba sasa, sisemi nakufahamu lakini angalau ninachakusema kidogo kukuhusu. Umejipambanua kama mtu apendaye haki, mtu apendaye utawala wa sheria, mtu apendaye demokrasia. Lisu umekuwa mstari wa mbele kukemea maonevu uyaonayo ndani ya nchi yako, umejigeuza kama msemaji wa wanaoonewa, kutetea wanyonge wanaonyimwa haki zao. Upo sawa, lakini umekosea jambo moja; nalo ni kushindwa kujua unatetea watu wa aina gani. Hilo ndilo kosa lako kuu.

Huwezi tetea haki za masikini ukabaki salama, huwezi tetea haki za wapumbavu ukabaki salama. Huwezi tetea watu wasiojielewa, huwezi tetea watu wasiojua unapigania nini kwao, huko ni kujitafutia matatizo makubwa ambayo hao unaowatetea hawatakusaidia kitu kwa sababu wao ni wapumbavu na masikini.

Kikawaida masikini ni watu wasiojithamini, watu wasio na shukrani, watu wasiojitambua, wengi wao ni wachawi, wanga, watu wasio na fadhila, masikini ukimsaidia huyo huyo ndio atakuja kukusema unajidai, ukimtetea masikini au mpumbavu huyo huyo ndio atakuambia unakihere here. Kamwe nakusihi acha mara moja kuhangaika na masikini.

Masikini unachoweza kuwasaidia ni kuwadhulumu hata kile kidogo walichonacho, kuwabagua, kuwatenga, kuwadharau, hicho ndicho wakipendacho masikini. Lakini ukijifanya unawapenda, unawajali nakuhakikishia unajiingiza mkenge, utaumia, utasagika na hakika utamalizika.

Nikukumbushe Ndugu Mhe. Lisu, hakuna aliyewahi kuwatetea masikini, na kuwapigania masikini akabaki salama. Wote waliojiingiza katika harakati hizo walikufa vifo vibaya, wengine walipewa adhabu kali za kuliwa na mamba, kuliwa na simba, kuchomwa moto, wakapotea na kuangamia.

Katika Dini, wapo Manabii walikuja kutetea haki za wanyonge, haki za masikini lakini wote waliuawa, tena wakazomewa na hao hao masikini. Nakupa mifano ya watu katika dini waliokuwa wanaharakati kama wewe, Musa, ndiye yule Mlawi aliyewatoa waisrael Misri, naye aliwapigania watumwa wale na kutaka kuwa uhuru wao. walichomlipa wote tunajua, walianza kulalamika kuwa bora warudishwe utumwani Misri kuliko kuwa huru Kanaani katika nchi yao. Mungu alitaka kuwaua lakini Kihere here cha Musa akawatetea, siku zilizofuata wakataka kumuua Musa wasijue huyo ndiye aliwatetea wasiuawe na Mungu. Musa alipowashtaki kwa Mungu, Mungu akamuambia, wewe si uliwatetea hao masikini, watumwa, wapumbavu wasiojielewa. Acha wakuue ili uwe na akili. Musa akabaki katumbua macho. Biblia inasema, Mungu aliwafyeka wote njiani, akambakiza Joshua na Kalebu. Huwezi kukomboa masikini, huwezi komboa watumwa, huwezi komboa wapumbavu ukabaki salama. Kuwatetea wapumbavu ni kutaka kutofika kanaani, usishangae kwa nini Musa hakufika Kanaani, aliwaendekeza wapumbavu wale.

Yesu naye walimuua, wakamsulubisha, na kumtemea mate. Na wale aliokuwa anawatetea ndio hao hao waliomtukana, walioimba asulubiwe. Huwezi Mkomboa masikini hata siku moja. Huwezi komboa mtu mpumbavu ukasalimika.

Hata kwenye maisha ya kawaida, wale unaowasaidia ndio hao hao watakaogeuka maadui zako. Hao hao ndio watakao kuteta.

Mhe Lisu, naomba nikuonye, na ikikupendeza fuata ushauri wangu. Acha kutetea haki za wapumbavu, haki za masikini, haki za wanyonge sijui upuuzi gani. Mungu mwenyewe atahangaika na watu wake. Ikiwa yeye kaacha watu waonewe wewe unakuja kuwatetea huoni unatafuta maneno.

Masikini ni kama swala au digidigi mbugani, huwezi mgeuza digidigi akawa simba alafu ukabaki salama. Ili mbuga iwe na amani ni lazima swala aliwe, kumtetea swala ni kuchafua amani ya mbugani.

Nature inataka dunia iende hivyo, wote waliojifanya kutetea tabaka la chini walipotezwa, na uhakika ni kuwa watazidi kupotezwa.

Nakushauri; tetea watu wenye akili, watu matajiri, watu wenye nguvu, hao utapata ulinzi, hao hawana unafiki, hao utapata cheo, na utaishi kwa amani.

Matajiri ukiwatetea wanajua thamani ya kile unachokifanya, hivyo nawe watakutetea siku yakikukuta yako. Lakini masikini ukiwatetea kwanza wao wenyewe hawajui thamani yao iweje wajue thamani ya kile ukifanyacho, zaidi sana watakutelekeza siku yakikupata kisha watakuambia ulikuwa unakihere here.

Watu wenye akili ukiwatetea watakulinda, kwa maana wanajali kile ukifanyacho, watakulipa hisani na fadhila. Lakini wapumbavu ukiwatetea hao hao watakuwa wakwanza kukusnitch na kukuuza kwa bei ya kutupwa, mwisho utauawa na kuangamizwa.

Wenye nguvu ukipendekeza kwao, watakulinda. Wao wanajua na kuthamini mchango wako kwao. Lakini sio kwa watu wanyonge na fukara. Wanyonge wataishia kukusengenya na kukuloga, ukiwa mbele yao wanakushangilia ukitoka wanakusema. Wataachaje kukusema ikiwa hawana kazi, kazi yao ni kusengenya watu vijiweni.

Mhe. Lisu, acha kupoteza muda wako. Hutapata zawadi popote pale iwe huku duniani au kwa yule aliyeiumba hii dunia.

Aliyeumba hii dunia ndiye anataka dunia iwe hivi ilivyo, wapumbavu wahenyeke, wenye hekima wale bata. Masikini wachapike, matajiri wale upepo mwanana.

Namna bora ya kumsaidia masikini ni kumdhulumu na kumuonea. Namna bora ya kumsaidia mpumbavu ni kumfundisha upumbavu,.

Kufikia hapa Mhe, Lisu niseme ni matumaini yangu barua hii utakuwa umeielewa. Na utaifanyia kazi.

Wako katika majukumu

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
robertheriel99@gmail.com

Nakala moja kwa

1. Tundu Anthipas Lisu
2. Wanaharakati wote
3. Wanamageuzi

Nakala nyingine nitabaki nayo.
bora kufa kwa kutetea unacho kiamini mkuu kuliko kufa kwa malaria by the way kila mtu alipozaliwa tiyari kifo chake kilisha pangwa ni mazingira gani utapia kufa so lazima alima utetee kile unachokiamin never give up mkuu , ila nikili kwenye hayo magroup yako mi simo mkuu
 
Mleta mada umeandika ukweli mtupu kwani tunaona hata kwenye mtandao huu wale wanaotetewa ndio hao hao wanaokula buku saba na kuendelea kumtukana humu.Hawathamini kabisa alichowafanyia kuwasaidia wao na kwamba ndicho hicho kilichomletea adha yote anayopata. Ni kumwombea tu Mungu amsaidie !!!
 
BARUA YA WAZI KWA TUNDU LISU

Na, Robert Heriel
Taikon wa Fasihi,
S.L.P 9977, JIBI,
Kutoka Nyota ya Tibeli.
30, 07. 2020.

YAH: KUKUONYA DHIDI YA KUTETEA MASIKINI NA WAPUMBAVU.

Ndugu Mhe Lisu, Kichwa cha habari hapo juu cha husika.

Ninafuraha kubwa kukuandikia barua hii ya wazi ambapo najua watu wengi wataisoma nawe itakufikia. Utanisamehe ikiwa njia hii niliyoitumia pengine isikufurahishe lakini ni katika hali ya kukupa ujumbe wenye manufaa wewe na wale wote wenye tabia kama zako, mimi nikiwa mmoja wao.

Mhe. Lisu, nimekufuatilia kwa miaka saba sasa, sisemi nakufahamu lakini angalau ninachakusema kidogo kukuhusu. Umejipambanua kama mtu apendaye haki, mtu apendaye utawala wa sheria, mtu apendaye demokrasia. Lisu umekuwa mstari wa mbele kukemea maonevu uyaonayo ndani ya nchi yako, umejigeuza kama msemaji wa wanaoonewa, kutetea wanyonge wanaonyimwa haki zao. Upo sawa, lakini umekosea jambo moja; nalo ni kushindwa kujua unatetea watu wa aina gani. Hilo ndilo kosa lako kuu.

Huwezi tetea haki za masikini ukabaki salama, huwezi tetea haki za wapumbavu ukabaki salama. Huwezi tetea watu wasiojielewa, huwezi tetea watu wasiojua unapigania nini kwao, huko ni kujitafutia matatizo makubwa ambayo hao unaowatetea hawatakusaidia kitu kwa sababu wao ni wapumbavu na masikini.

Kikawaida masikini ni watu wasiojithamini, watu wasio na shukrani, watu wasiojitambua, wengi wao ni wachawi, wanga, watu wasio na fadhila, masikini ukimsaidia huyo huyo ndio atakuja kukusema unajidai, ukimtetea masikini au mpumbavu huyo huyo ndio atakuambia unakihere here. Kamwe nakusihi acha mara moja kuhangaika na masikini.

Masikini unachoweza kuwasaidia ni kuwadhulumu hata kile kidogo walichonacho, kuwabagua, kuwatenga, kuwadharau, hicho ndicho wakipendacho masikini. Lakini ukijifanya unawapenda, unawajali nakuhakikishia unajiingiza mkenge, utaumia, utasagika na hakika utamalizika.

Nikukumbushe Ndugu Mhe. Lisu, hakuna aliyewahi kuwatetea masikini, na kuwapigania masikini akabaki salama. Wote waliojiingiza katika harakati hizo walikufa vifo vibaya, wengine walipewa adhabu kali za kuliwa na mamba, kuliwa na simba, kuchomwa moto, wakapotea na kuangamia.

Katika Dini, wapo Manabii walikuja kutetea haki za wanyonge, haki za masikini lakini wote waliuawa, tena wakazomewa na hao hao masikini. Nakupa mifano ya watu katika dini waliokuwa wanaharakati kama wewe, Musa, ndiye yule Mlawi aliyewatoa waisrael Misri, naye aliwapigania watumwa wale na kutaka kuwa uhuru wao. walichomlipa wote tunajua, walianza kulalamika kuwa bora warudishwe utumwani Misri kuliko kuwa huru Kanaani katika nchi yao. Mungu alitaka kuwaua lakini Kihere here cha Musa akawatetea, siku zilizofuata wakataka kumuua Musa wasijue huyo ndiye aliwatetea wasiuawe na Mungu. Musa alipowashtaki kwa Mungu, Mungu akamuambia, wewe si uliwatetea hao masikini, watumwa, wapumbavu wasiojielewa. Acha wakuue ili uwe na akili. Musa akabaki katumbua macho. Biblia inasema, Mungu aliwafyeka wote njiani, akambakiza Joshua na Kalebu. Huwezi kukomboa masikini, huwezi komboa watumwa, huwezi komboa wapumbavu ukabaki salama. Kuwatetea wapumbavu ni kutaka kutofika kanaani, usishangae kwa nini Musa hakufika Kanaani, aliwaendekeza wapumbavu wale.

Yesu naye walimuua, wakamsulubisha, na kumtemea mate. Na wale aliokuwa anawatetea ndio hao hao waliomtukana, walioimba asulubiwe. Huwezi Mkomboa masikini hata siku moja. Huwezi komboa mtu mpumbavu ukasalimika.

Hata kwenye maisha ya kawaida, wale unaowasaidia ndio hao hao watakaogeuka maadui zako. Hao hao ndio watakao kuteta.

Mhe Lisu, naomba nikuonye, na ikikupendeza fuata ushauri wangu. Acha kutetea haki za wapumbavu, haki za masikini, haki za wanyonge sijui upuuzi gani. Mungu mwenyewe atahangaika na watu wake. Ikiwa yeye kaacha watu waonewe wewe unakuja kuwatetea huoni unatafuta maneno.

Masikini ni kama swala au digidigi mbugani, huwezi mgeuza digidigi akawa simba alafu ukabaki salama. Ili mbuga iwe na amani ni lazima swala aliwe, kumtetea swala ni kuchafua amani ya mbugani.

Nature inataka dunia iende hivyo, wote waliojifanya kutetea tabaka la chini walipotezwa, na uhakika ni kuwa watazidi kupotezwa.

Nakushauri; tetea watu wenye akili, watu matajiri, watu wenye nguvu, hao utapata ulinzi, hao hawana unafiki, hao utapata cheo, na utaishi kwa amani.

Matajiri ukiwatetea wanajua thamani ya kile unachokifanya, hivyo nawe watakutetea siku yakikukuta yako. Lakini masikini ukiwatetea kwanza wao wenyewe hawajui thamani yao iweje wajue thamani ya kile ukifanyacho, zaidi sana watakutelekeza siku yakikupata kisha watakuambia ulikuwa unakihere here.

Watu wenye akili ukiwatetea watakulinda, kwa maana wanajali kile ukifanyacho, watakulipa hisani na fadhila. Lakini wapumbavu ukiwatetea hao hao watakuwa wakwanza kukusnitch na kukuuza kwa bei ya kutupwa, mwisho utauawa na kuangamizwa.

Wenye nguvu ukipendekeza kwao, watakulinda. Wao wanajua na kuthamini mchango wako kwao. Lakini sio kwa watu wanyonge na fukara. Wanyonge wataishia kukusengenya na kukuloga, ukiwa mbele yao wanakushangilia ukitoka wanakusema. Wataachaje kukusema ikiwa hawana kazi, kazi yao ni kusengenya watu vijiweni.

Mhe. Lisu, acha kupoteza muda wako. Hutapata zawadi popote pale iwe huku duniani au kwa yule aliyeiumba hii dunia.

Aliyeumba hii dunia ndiye anataka dunia iwe hivi ilivyo, wapumbavu wahenyeke, wenye hekima wale bata. Masikini wachapike, matajiri wale upepo mwanana.

Namna bora ya kumsaidia masikini ni kumdhulumu na kumuonea. Namna bora ya kumsaidia mpumbavu ni kumfundisha upumbavu,.

Kufikia hapa Mhe, Lisu niseme ni matumaini yangu barua hii utakuwa umeielewa. Na utaifanyia kazi.

Wako katika majukumu

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
robertheriel99@gmail.com

Nakala moja kwa

1. Tundu Anthipas Lisu
2. Wanaharakati wote
3. Wanamageuzi

Nakala nyingine nitabaki nayo.
Hii ni mojawapo ya hekima kubwa iliyowahi kuwakilishwa vyema hapa jukwaani kuhusiana na wale wenye kutambulika kama wanyonge ndani ya taifa letu. Hii ni sura halisi ya watu hao, na hata kuweza kuthibitika wazi ktk maisha yetu ya kila siku.

Umaskini ni kama laana tu, mtu maskini ni vigumu sana kuaminika, tunaona hata viongozi wetu wote waliowahi kuliongoza Taifa, wenye kuhusudu sera za kijamaa zenye kukumbatia sera za umaskini wa pamoja na kuchukia mafanikio ya mtu mmoja mmoja jinsi ambavyo wamefeli.
 
Sasa nimekuekewe wewe kweli n taikon wa Fasihi few will catch you
 
BARUA YA WAZI KWA TUNDU LISU

Na, Robert Heriel
Taikon wa Fasihi,
S.L.P 9977, JIBI,
Kutoka Nyota ya Tibeli.
30, 07. 2020.

YAH: KUKUONYA DHIDI YA KUTETEA MASIKINI NA WAPUMBAVU.

Ndugu Mhe Lisu, Kichwa cha habari hapo juu cha husika.

Ninafuraha kubwa kukuandikia barua hii ya wazi ambapo najua watu wengi wataisoma nawe itakufikia. Utanisamehe ikiwa njia hii niliyoitumia pengine isikufurahishe lakini ni katika hali ya kukupa ujumbe wenye manufaa wewe na wale wote wenye tabia kama zako, mimi nikiwa mmoja wao.

Mhe. Lisu, nimekufuatilia kwa miaka saba sasa, sisemi nakufahamu lakini angalau ninachakusema kidogo kukuhusu. Umejipambanua kama mtu apendaye haki, mtu apendaye utawala wa sheria, mtu apendaye demokrasia. Lisu umekuwa mstari wa mbele kukemea maonevu uyaonayo ndani ya nchi yako, umejigeuza kama msemaji wa wanaoonewa, kutetea wanyonge wanaonyimwa haki zao. Upo sawa, lakini umekosea jambo moja; nalo ni kushindwa kujua unatetea watu wa aina gani. Hilo ndilo kosa lako kuu.

Huwezi tetea haki za masikini ukabaki salama, huwezi tetea haki za wapumbavu ukabaki salama. Huwezi tetea watu wasiojielewa, huwezi tetea watu wasiojua unapigania nini kwao, huko ni kujitafutia matatizo makubwa ambayo hao unaowatetea hawatakusaidia kitu kwa sababu wao ni wapumbavu na masikini.

Kikawaida masikini ni watu wasiojithamini, watu wasio na shukrani, watu wasiojitambua, wengi wao ni wachawi, wanga, watu wasio na fadhila, masikini ukimsaidia huyo huyo ndio atakuja kukusema unajidai, ukimtetea masikini au mpumbavu huyo huyo ndio atakuambia unakihere here. Kamwe nakusihi acha mara moja kuhangaika na masikini.

Masikini unachoweza kuwasaidia ni kuwadhulumu hata kile kidogo walichonacho, kuwabagua, kuwatenga, kuwadharau, hicho ndicho wakipendacho masikini. Lakini ukijifanya unawapenda, unawajali nakuhakikishia unajiingiza mkenge, utaumia, utasagika na hakika utamalizika.

Nikukumbushe Ndugu Mhe. Lisu, hakuna aliyewahi kuwatetea masikini, na kuwapigania masikini akabaki salama. Wote waliojiingiza katika harakati hizo walikufa vifo vibaya, wengine walipewa adhabu kali za kuliwa na mamba, kuliwa na simba, kuchomwa moto, wakapotea na kuangamia.

Katika Dini, wapo Manabii walikuja kutetea haki za wanyonge, haki za masikini lakini wote waliuawa, tena wakazomewa na hao hao masikini. Nakupa mifano ya watu katika dini waliokuwa wanaharakati kama wewe, Musa, ndiye yule Mlawi aliyewatoa waisrael Misri, naye aliwapigania watumwa wale na kutaka kuwa uhuru wao. walichomlipa wote tunajua, walianza kulalamika kuwa bora warudishwe utumwani Misri kuliko kuwa huru Kanaani katika nchi yao. Mungu alitaka kuwaua lakini Kihere here cha Musa akawatetea, siku zilizofuata wakataka kumuua Musa wasijue huyo ndiye aliwatetea wasiuawe na Mungu. Musa alipowashtaki kwa Mungu, Mungu akamuambia, wewe si uliwatetea hao masikini, watumwa, wapumbavu wasiojielewa. Acha wakuue ili uwe na akili. Musa akabaki katumbua macho. Biblia inasema, Mungu aliwafyeka wote njiani, akambakiza Joshua na Kalebu. Huwezi kukomboa masikini, huwezi komboa watumwa, huwezi komboa wapumbavu ukabaki salama. Kuwatetea wapumbavu ni kutaka kutofika kanaani, usishangae kwa nini Musa hakufika Kanaani, aliwaendekeza wapumbavu wale.

Yesu naye walimuua, wakamsulubisha, na kumtemea mate. Na wale aliokuwa anawatetea ndio hao hao waliomtukana, walioimba asulubiwe. Huwezi Mkomboa masikini hata siku moja. Huwezi komboa mtu mpumbavu ukasalimika.

Hata kwenye maisha ya kawaida, wale unaowasaidia ndio hao hao watakaogeuka maadui zako. Hao hao ndio watakao kuteta.

Mhe Lisu, naomba nikuonye, na ikikupendeza fuata ushauri wangu. Acha kutetea haki za wapumbavu, haki za masikini, haki za wanyonge sijui upuuzi gani. Mungu mwenyewe atahangaika na watu wake. Ikiwa yeye kaacha watu waonewe wewe unakuja kuwatetea huoni unatafuta maneno.

Masikini ni kama swala au digidigi mbugani, huwezi mgeuza digidigi akawa simba alafu ukabaki salama. Ili mbuga iwe na amani ni lazima swala aliwe, kumtetea swala ni kuchafua amani ya mbugani.

Nature inataka dunia iende hivyo, wote waliojifanya kutetea tabaka la chini walipotezwa, na uhakika ni kuwa watazidi kupotezwa.

Nakushauri; tetea watu wenye akili, watu matajiri, watu wenye nguvu, hao utapata ulinzi, hao hawana unafiki, hao utapata cheo, na utaishi kwa amani.

Matajiri ukiwatetea wanajua thamani ya kile unachokifanya, hivyo nawe watakutetea siku yakikukuta yako. Lakini masikini ukiwatetea kwanza wao wenyewe hawajui thamani yao iweje wajue thamani ya kile ukifanyacho, zaidi sana watakutelekeza siku yakikupata kisha watakuambia ulikuwa unakihere here.

Watu wenye akili ukiwatetea watakulinda, kwa maana wanajali kile ukifanyacho, watakulipa hisani na fadhila. Lakini wapumbavu ukiwatetea hao hao watakuwa wakwanza kukusnitch na kukuuza kwa bei ya kutupwa, mwisho utauawa na kuangamizwa.

Wenye nguvu ukipendekeza kwao, watakulinda. Wao wanajua na kuthamini mchango wako kwao. Lakini sio kwa watu wanyonge na fukara. Wanyonge wataishia kukusengenya na kukuloga, ukiwa mbele yao wanakushangilia ukitoka wanakusema. Wataachaje kukusema ikiwa hawana kazi, kazi yao ni kusengenya watu vijiweni.

Mhe. Lisu, acha kupoteza muda wako. Hutapata zawadi popote pale iwe huku duniani au kwa yule aliyeiumba hii dunia.

Aliyeumba hii dunia ndiye anataka dunia iwe hivi ilivyo, wapumbavu wahenyeke, wenye hekima wale bata. Masikini wachapike, matajiri wale upepo mwanana.

Namna bora ya kumsaidia masikini ni kumdhulumu na kumuonea. Namna bora ya kumsaidia mpumbavu ni kumfundisha upumbavu,.

Kufikia hapa Mhe, Lisu niseme ni matumaini yangu barua hii utakuwa umeielewa. Na utaifanyia kazi.

Wako katika majukumu

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
robertheriel99@gmail.com

Nakala moja kwa

1. Tundu Anthipas Lisu
2. Wanaharakati wote
3. Wanamageuzi

Nakala nyingine nitabaki nayo.
Huu ni mtazamo kwa wanyama porini ambapo mwenye nguvu ndio anaishi (survival for the fittest). Ukitaka wanadamu waishi hivyo ni kuwataka waishi kama wanyama pori. Sina uhakika kama unafurahia kuona mtu akiibiwa au kudhulumiwa na mwenye nguvu zaidi. Siku za kuishi mawazo yako ni zama za kale kabla hata watu hawajavumbua moto. Mwanadamu amebadilika sana na anaendelea kupata hekima ya juu zaidi. Mambo mengi sana yamebadilika kuhusu haki na ustaarabu, hata mimi kijana nimeshuhudia mengi mno yakibadilika kijijini kwangu ukilinganisha na miaka ya tisini. Tundu Lissu anafanya kazi adhimu kabisa ya kuwatetea wanyonge ili wasidhulumiwe na wadhalimu. Hili ni jambo la juu sana na linawahusu wenye fikra na upeo mkubwa na ndio maana wengi hawawezi. Ni rahisi kutetea matumbo na hisia binafsi. Tundu Lissu anayafanya ya akina Yesu, Nyerere, Mandela, n.k na hata akifa, angali bado anaishi. Akina Idd Amin, Mobutu, Bokassa na wengine wamekufa na wamekufa kweli.
 
Narudia kusoma Tena na Tena nimegundua kitu kimoja kwako. Wewe Ni mwandishi wa fasihi. Tundu Lissu wewe endelea na harakati ndio maana Mungu alikuponya ukanusurika kifo. Kufa utakufa tu hata wewe mwandishi siku ikifika hakuna namna. Sote tutakabiliana na kifo kwahiyo tusihofu kutenda mazuri.
Talanta ziko nyingi, Kuna wengine wamepewa ya uongo, ukarimu, upole, ukatili, huruma nk. Hatuwezi kulingana wote Ni lazima kila mmoja wetu aitendee talanta yake haki inayostahili.
 
Kwani mkuu, hujawahi kusoma "aliyenacho ataongezewa na asiyenacho atanyang' anywa" jamaa kaongea ukweli unaochomachoma!
Ni kweli Mkuu ila hii issue iko subjective maana humohumo wameandika katka 3Yohana 1:2
"Mpenzi naomba ufanikiwe katika mambo yote............."
 
Huyu ndugu Heriel yuko sahihi sana. In a philosophical point of view, hamaanishi moja kwa moja binadamu tusisaidiane. Kusaidiana viumbe hai ni natural. We are living symbiotically. Kila kiumbe kinamtegemea kiumbe mwingine ili uhai/uzima na maisha yaendelee. Kusaidiana ili maisha yaendelee kuna sura na ni kwa aina nyingi.
SASA unatakiwa umakini mkubwa linapofika suala la kusaidiana.
Kwa ujumla, kumsaidia maskini kuliko kuzuri ni kule kwa aina inayochukuliwa na kuonekana kama kumnyonya, kumdhurumu, kumdhalilisha, na kadhalika.
Kwa kweli ni hatari sana kwa mtu mwenye maono ya maendeleo kuwa karibu na mtu maskini. Uhusiano wenu uwe ktk kumtumikisha huku ukihakikisha 99% ya faida inabaki kwako ili aendelee kukutumikia.
Kwa kweli, umaskini ni kitu kibaya. Ni mojawapo ya laana Bwana Yesu Kristo alikuja kutuponya wanadamu (2Wakorintho 8:9).
Ila tusiache kusaidiana kwa kadiri na kwa mujibu wa imani zetu (Mambo ya Walawi 25:35; Ayubu 29: 12; Wagalatia 6:10, n.k.).
Umaskini unaandamana na taabu, mateso, adha, msongo wa mawazo, sonona; mara nyingi hutawaliwa na moyo wa kulipa kisasi hususani kwa watu wenye ukwasi, hivyo, huwa mwepesi kufanya Uovu. "Wajumbe" wengi ni maskini, si mmeshuhudia ktk maeneo mengi walilolifanya lililo kinyume na Wananchi wengi? Wamewapigia kura nyingi wale waliowapatia pesa.
Umaskini ni kitu kibaya hakika. Na maskini ni mtu wa hatari all together.
 
Umeandika kwa kutumia fasihi maridadi sana....

Kwa ubunifu wa lugha uliyoitumia kuandika, wengi wanaisoma bila kutafakari, wameshindwa kukuelewa...

Binafsi nimekuelewa vizuri. Ujumbe unaokusudia kumpa Tundu Lissu, actually siyo kwamba aache harakati zake za kutetea hawa masikini, wajinga na wapumbavu...

Maudhui ya andiko hili yamejikita kwenye taahadhari zaidi kwa Tundu Lissu kwamba, lipo tatizo ktk uelewa wa wengi wa watu anaowatetea ambao kiuhalisia hawajui hata kama huyu mtu anawatetea wao, anaumia kwa ajili yao, amemwaga damu kwa ajili yao, amevuliwa ubunge wake kwa ajili yao, amepigwa risasi kiasi cha kutwaa uhai wake kwa ajili yao....

Haya mambo ndivyo yalivyo. Siku zote hakuna watetezi wa haki na uhuru wa watu malofa, masikini na wapumbavu (kama ulivyowaita) wamewahi kuungwa mkono na malofa wote. Na sababu ni moja tu, UFAHAMU na UELEWA duni....

Lakini jambo moja ni hakika. Wengi wa wapumbavu, malofa na masikini hawa wasioelewa, hufa ama hufyekelewa nbali lakini MBEBA MAONO HUWA HAFI mpaka maono yake ama kusudi alilopewa na Mungu Yehova limetimia....

Umewatolea mfano MUSA MLAWI na YESU KRISTO, MNAZARETHI...

Hawa walikuwa wajumbe maalumu waliobeba VISION na MISSION ya Mungu juu ya watu wa dunia hii ambao wengi ni malofa na masikini na wajinga na wapumbavu....

Hawa walilindwa na Mungu mwenyewe kwa nguvu zote. Hakuna aliyekufa japo walipitia kwenye dhahama kubwa ya mateso ya kufa na kupona...

Pamoja na hayo, mpango wa Mungu siku zote na milele huwa hakuna binadamu awaye yeyote anaweza kuuzuia usifanikiwe japo watajitajidi kutaka kuukwamisha...

Ndivyo ilivyokuwa kwa Musa dhidi ya kuwakomboa wana wa Israel toka Misri kwenda Kanaani nchi ya maziwa na asali. Musa hakufa. Musa alitwaliwa hai na Mungu mwenyewe....

Ndivyo ilivyokuwa kwa Yesu Kristo. Alitumwa na Mungu mwenyewe kuukomboa ulimwengu. Kumkomboa mwanadamu toka ktk utumwa wa dhambi na mauti kwa njia ya KIFO CHA MSALABA...

YESU KRISTO hakuuwawa kifo cha kawaida ili watesi wake wajitangazie ushindi. Kifo cha Yesu Kristo kiliruhusiwa na Mungu mwenyewe kama njia ya kuishinda nguvu ya mauti...

Hii haikujalisha hawa malofa na masikini na wajinga na wapumbavu wanamfikiriaje huyu mpigania haki na uhuru wao yaani YESU KRISTO...

Wakati mwingine, siyo lazima lofa, masikini na mjinga huyu aone na kutambua kuwa anakombolewa yeye. Atatambua baadaye na wakati mwingine hatatambua kabisa mpaka anakufa. Thamani ya ukombozi utafurahiwa na kizazi chao kinachofuata....

Tundu Lissu ni mbeba maono ya nchi hii. Ni mkombozi wa malofa na masikini na wapumbavu na wajinga wa nchi hii. Hajuti sasa. Hatajuta baadaye. Hahitaji kutambuliwa sasa. Atatambuliwa baadaye. Hahitaji uungwaji mkono wa hili Kundi ingalau kwa sasa...

Kumbuka, MBEBA MAONO ama KUSUDI FULANI la MUNGI diku zote huwa HAFI na wala kamwe HAJUTI hadi kusudi limetimizwa....!!
 
Umeongea ukweli unaochoma
Ndio maana Mkapa aliwaita wapinzani marofa na wapumbavu, Lisu huyu alikuwa anawatetea mabwenyenye akina accacia Kwa vitisho vikali, mala tutanyorewa kipara bila maji, ho, madini yote sio yetu, mala tutaperekwa miga mchi ifirisiwe,. Hiyo tuwaache mabwenyenye waendelee kutuibia, harafu huyu ndiye anataka nchi hawatetee masikini. Kawadanganye marofa wenzio huko
 
Nmesoma nmegundua tunahitaji ukomboz wa kifikra sio hela wala Uhuru Bali Amani...


Hongera kwa mtazamo wako uko sahihi pia,ila naona vyema zaid kama utaongezea kusema MASKINI ANAHITAJI KUKOMBOLEWA KIFIKRA (KUJITAMBUA NA KUWATAMBUA NAFASI YA KILA MTU KTK JAMII) ,Baada ya kujitambua ndio APATIWE amani ili AZIONE FURSA ZA KIUCHUMI kujiendeleza...



-ELIMU ELIMU ELIMU-
Kitambo tulishaandika humu... ngumu sana "malofa na wapumbavu" wenzetu kuelewa PUNDA YAKE FIMBO NA MZIGO!!
:director: piiii piiiii, tupulize vuvuzelaa, pi piii HAMUELEWANI, ninyi si wamoja. na ilisemwa wa mbili havai moja na kinyume chake. Sishangai kabisa kwa maana hamjui kipi mnakitaka na kipi hamkitaki. Fugueni fikra zenu, amkeni toka usingizini, HAKIKA PANAHITAJIKA MAPINDUZI YA KIFIKRA KWA WATANZANIA. LA SIVYO TUTANDELEA KUCHEZA NGOMA ISIYOJULIKANA:nono::sad:

Wanasiasa wachache wenye maslahi yao wataendelea kuwatumia wapumbavu wachache ili kutimiza malengo yao ya kijinga, ninawaambia pamoja na kujiambia mwenyewe hapa ndugu zangu:

TUSIMWAMINI MWANASIASA YEYOTE AWAE HATA KAMA NI NDUGU AMA MZAZI WETU.

Kila mmoja anapigania ama kulinda maslahi yake, uchafu mtupu. (leo watu wanashawishiwa kuandamana huku na kule bila kuwapo malengo maalum)

Wenzenu huko duniani wanajua wakiandamana matokeo yakiwa tofauti watafanya nini? Leo Mtanzania anaandamana achilia mbali pasi ya kusafiria NAULI yenyewe hana, Akiumia hana bima itakayomlipa wala hana hata shekeli ya kununulia dawa, na mwisho wa yote atakwenda kutibiwa kwenye hospitali ya serikali anayoipinga! Akifika kule ataulizwa hati ya polisi namba tatu (PF.3) hapo ndio atasindikizwa na pingu kurudi hospitali kama majibu yake hayakujitosheleza. (mhanga wa maandamano - tungelimuita mhanga wa demokrasia) Na pia tujiulize tena "Je katika kuandamana kwetu magari na nyumba zinazopigwa mawe huwa zimefanya makosa gani?"

Gari la bwana Materu ambae si shabiki wa siasa na haki tunayoidai vinahusiana nini hata aadhibiwe?
Je ni kwanini Mpitanjia ambaye hayuko katika maandamano apigwe na polisi kwa kuhusishwa ya yasiomhusu?

Tunahitaji mabadiliko makubwa ya kifikra na pia tunahitaji tujiongezee busara katika maamuzi yetu, je Tanzania tuitakayo ama ijayo itakuwa ya kutotii mamlaka na utawala wa kisheria? (tuwe wakweli na tusimamie ukweli huo) Kama ni kuutafuta madaraka, umaarufu juu ya vilema na maiti za Watanzania wenzetu haya na iwe...

Yawezekana kabisa ikawa kweli tunayoyataka hatuwezi kuyapata bila shinikizo, lakini pia tuangalie sarafu yetu upande wa pili nani ataathirika zaidi na shinikizo hilo WAO au SISI?

Siioni picha njema hata kidogo. Wapo wanaodhani kwamba yanayofanyika ni sahihi (narudia tena - Wahanga wa matokeo ya upinzani wa serikali si wahusika pekee bali wengi wao ni walio nje ya wakusudiwa)

Hivyo basi kabla hatujafanya tunayotaka kufanya; Tuwafikirie watoto wetu na wazee wetu kwanza waliomo majumbani.

Tufikirie mbali zaidi ya hapo ndugu zanguni, ili tuijenge Tanzania tuitakayo. Tanzania yenye neema, demokrasia ya kweli na amani. Na hayo yote hayawezi kupatikana bila kuwa na KATIBA inayoruhusu. Lakini kabla ya katiba kupatikana tungelipaswa kuwa wapole vinginevyo tutakula virungu vya kutosha na wapo watakaokufa pia bila kujulikana.

Narudia tena ndugu zangu watanzania...

TUTAHITAJI MAPINDUZI YA KIFIKRA KWANZA, NA TUNAPASWA KUJUA TUNATAKA NINI KWA TANZANIA IJAYO.

😠
Nilipoandika hayo nilitarajia tungeshinikiza KATIBA MPYA KUPITIA VYAMA VYETU AU MAHAKAMA... TUNACHOWAZA SISI SIO WAWAZACHO WAO...
 
Ndio maana Mkapa aliwaita wapinzani marofa na wapumbavu, Lisu huyu alikuwa anawatetea mabwenyenye akina accacia Kwa vitisho vikali, mala tutanyorewa kipara bila maji, ho, madini yote sio yetu, mala tutaperekwa miga mchi ifirisiwe,. Hiyo tuwaache mabwenyenye waendelee kutuibia, harafu huyu ndiye anataka nchi hawatetee masikini. Kawadanganye marofa wenzio huko
Hiki ni kiswahili au kikabila?
 
Back
Top Bottom