Barua ya wazi kwa Waziri wa Maji na Mkurugenzi wa DAWASA

Hata angetumbua DAWASA yote bado aliyesababisha Dar kuwa na uhaba wa maji hadi sasa ni yeye. Ujenzi wa bwawa la Kidunda ulipaswa uwe umekamilika siku nyingi all plans were already done. Kwa roho mbaya yake mradi ukayeyuka.
 
NYERERE ALIFANYA KOSA KUBWA SANA KUIUNGANISHA TZ

MACHAME KWETU KULIKUWA NA MAJI YA BURE TENA YA BOMBANI , ACHA YA KWENYE VIJITO ...

MWISHO WA SIKU PUMBA ZITAJITENGA NA MCHELE
 
Tatzo la maji dsm litaendelea kuwa Sugu miaka ming sana, watu na mji unaongezeka kwa kasi sana huku chanzo cha maji kikiwa kile kile Mto Ruvu.. Nashauri Wizara ya Maji itafute chanzo mbadala mfano visima au kuchukua maji mito ya karibu na dsm kama Rufiji ambapo maji yanaingia meng Baharini bure tu
 
Kweli kabisa, ila haya mambo yanafikirisha sana,kwamba rais hajui kabisa kua Dar ni mji unakua kwa kasi na mahitaji ya maji ni Mengi? Dar ina shughuli nyingi sana kuliko mkoa wowote tz,na shughuli hizo zote zinahitaji maji na zinaongezeka kila siku.

Tanzania tunapoteza maji mengi sana wakati wa mvua,serikali ichimbe mabwawa yakuvuna maji katika maeneo yanayozunguka Dar.
 
Kama watu wanazidi kuongezeka kwa kasi maji yatazidi kuwa tatizo tu. Jitihada za kuongeza upatikanaji maji lazima ziende sambamba na kudhibiti overpopulation.
Pia watu wengi wa vijijini wamekuwa na tatizo la maji muda mrefu sana huku jitihada kubwa zikielekezwa mjini.
 
Subiri mvua zianze kunyesha
Leo nimeulizia lori la.maji lita 3000 inafika shiingi za kitanzania laki moja na hamsini. Wanadaiaji wanachota Mbezimwisho ndio kuna afueni yanatoka.

Wahusika hebu tokeni kwenye viyoyozi mje mseme maji yatapatikana lini
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…