Barua yangu ya wazi kwa Wana JF wote

Azimio la kazi

Senior Member
Joined
Jun 7, 2023
Posts
138
Reaction score
452
Habari Wana JF ni matumaini yangu kuwa wote ni wazima wa afya.

Ni mimi kijana wenu mpendwa, ninaesomeshwa Kwa Kodi zenu katika moja ya Chuo kikuu hapo Dar es salaam.

Ni ukweli usiopingika kuwa, hatima ya taifa lolote lile lipo mikononi mwa walimu.

Kwa miaka ya hivi karibuni taaluma ya Ualimu imekuwa ikibezwa sana, na walimu kuonekana kama kundi ya mwisho katika utumishi Serikalini na sekta binafsi.

Wana JF, ukweli ni kwamba falsafa ya mwalimu ni falsafa ya wanafunzi, na falsafa ya wanafunzi ni falsafa ya taifa, falsafa ya taifa ni dira na muelekeo wa maendeleo kiuchumi, kijamii, kitamaduni na kisiasa.

Hivyo basi umaskini huu tunauona hivi sasa, ukosefu wa uadilifu kwa Wana jamii, mmonyoko wa maadili, rushwa, na mambo kama hayo ni matokeo ya laana ya kuweka taaluma ya ualimu na walimu kama kundi la mwisho.

Kwa mtazamo wangu, naona Kuwa serikali iandae mpango mkakati wanaotaka kusoma ualimu wawe ni wale cream, kuwe na vetting za kutosha ili mtu awe mwalimu kapikika kweli kweli.

Pia Serikali iboreshe maslahi na mazingira ya kazi ya walimu yawe bora, hii itatoa motisha na nguvu baina ya walimu katika kujenga taifa.

Nimemaliza field yangu, lakini nimegundua walimu Wana manunung'uniko juu ya kazi kubwa wanayofanya, licha ya maslah yao kuwa chini.
 
Majority wanaandaliwa KUWA wapita Kura tu.resoning capacity,zero.mpaka cku tutakapotambua kwamba elimu Bora ndio kitu muhimu KWA wananchi.kwa ss maslahi Bora KWA mwanasiasa ndo kitu muhimu.
 

Labda tuambie masilahi ya juu ni shilingi ngapi na yanaanzia shilingi ngapi na masilahi ya walimu yanaanzia shilingi ngapi na kuishia shilingi ngapi!
 
Ualimu mbaya, muulize biteko, na kina msonde watakuambia Kama mbaya au mzuri, watu wametusua na ualimu.
 
MWALIMU NYERERE ANAMALIZA KWA USHAIRI KWENYE KITABU CHAKE.

UONGOZI WETU NA HATMA YA TANZANIA.

Ole wake Tanzania Tusipoisaidia
Niwezalo nimelifanya kushauri na kuonya nimeonya.

tahadhali nimetoa ushauri na kuonya nimeshatoka kitini zaidi nifanye nini.

Namlilia Jaalia atumulikie njia Tanzania ailinde WAOVU wasiishinde.

Amina Tena Amina Amina Tena amina


UONGOZI WETU NA HATMA YA TANZANIA.
MWALIMU JK NYERERE
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…