BASATA kaeni mkao wa kula, Video ya Chura anarukaruka, ikitoka fungia kisha tia Kapuni

BASATA kaeni mkao wa kula, Video ya Chura anarukaruka, ikitoka fungia kisha tia Kapuni

Heshima kwenu wakuu,

Hii video ya Snura ya Wimbo wa Chura anarukaruka, ikitoka tu naomba ifungiwe. Mkishaifungia mumpige msanii marufuku ya kujihusisha na Muziki kwa Miaka mitatu. Hatuwezi endelea kulealea huu ujinga.

Kama mliweza kuufungia Wimbo wa Roma wa Viva Roma Viva ambao haukua na tatizo katika Swala la maadili, naamin huu wimbo ukitoka msanii atawekwa mbaroni hata siku mbili.

Imetosha sasa kwa hawa dada zetu kujifanya eti wamepinda, wao ndo wanajua kukata mauni, wao ndo wanajua kutembea uchi.

Naomba BASATA msiangalie Nyani usoni
Tatizo maneni ya wimbo au kukata viuno???
 
Tatizo maneni ya wimbo au kukata viuno???
Yote sawa. Wewe kama unajua kukata mauno ukaambiwa ni Chura utakubali? Nataka tumshikishe adabu, anawafundisha binti zetu tabia mbaya
 
Chura ni jipu afungiwe,muziki huo unafundisha mini kama sio maadili mabaya,BASATA tutoleeni huo uchafu
 
Kama wewe umeiona tuwekee hapa na sisi tuone. Kwanini ufaidi mwenyewe?
 
Bila shaka punde baada ya kutoka itafungiwa....Basata wasipoifungia basi watakuwa na matatizo ,kama waliweza kuifungia video ya kawaida mno ya AY sioni sababu kwann hii ibaki.
 
Hii ata wasipo fungia tu TV itakayo onyesha hii video itakua sio timamu.. Puuu
 
Back
Top Bottom