BASATA kaeni mkao wa kula, Video ya Chura anarukaruka, ikitoka fungia kisha tia Kapuni

BASATA kaeni mkao wa kula, Video ya Chura anarukaruka, ikitoka fungia kisha tia Kapuni

Aiseeeee ila wimbo huo huez angalia na watoto
 
Basata wanavyopenda nyuchi, utafungiwa kwenu wao watakuwa wakiendelea kuutumbulia mimacho kila siku asubuhi huku midushelele yao ikiwa imesimama wima kama askari anayekaguliwa
Hahahahaaa,nimecheka sana aseeeee
 
Snura amesema huu wimbo hautoi kwenye kideo... Anayeutaka anaenda kucheki YouTube.
Sio mjinga yeye, anajua akiutoa utafungiwa
 
Target yao ilikuwa You Tube...'biashara' imekuwa ngumu toka Magu aanze kutumbua majipu....
Watu wamekuja na strategy mpya za kusaka soko
 
FANI IMEVAMIWA SHILOLE NA SNURA .........
 
Heshima kwenu wakuu,

Hii video ya Snura ya Wimbo wa Chura anarukaruka, ikitoka tu naomba ifungiwe. Mkishaifungia mumpige msanii marufuku ya kujihusisha na Muziki kwa Miaka mitatu. Hatuwezi endelea kulealea huu ujinga.

Kama mliweza kuufungia Wimbo wa Roma wa Viva Roma Viva ambao haukua na tatizo katika Swala la maadili, naamin huu wimbo ukitoka msanii atawekwa mbaroni hata siku mbili.

Imetosha sasa kwa hawa dada zetu kujifanya eti wamepinda, wao ndo wanajua kukata mauni, wao ndo wanajua kutembea uchi.

Naomba BASATA msiangalie Nyani usoni
**USHAURI WA BURE KWA BASATA**
kwa hali ya mambo ilivyo sasa basata inapaswa kuwa wakali kwa wasanii wachafu (putting deterrence) kwanza kwa kutoa leseni za kazi kwa wasanii wote ili endapo msanii inakiuka maadili ya utendaji wake anafungiwa mara moja leseni. kwa msanii kama snura na wengineo wanapaswa kufungiwa vyote video na audio kutokupigwa katika vituo vyote hapa nchini, pamoja na fine kali. wasanii huwa wana viburi kuwa ikifungiwa video bado atapiga pesa kupitia audio kwenye stations za redio, hivyo hapa dawa ni kumtisha kuwa vyote viwili (audio na video) zitafungiwa......
 
ImageUploadedByJamiiForums1462263084.890585.jpg

Chura anaruka ruka.
Huyu snura katuharinia kabisa watoto wetu.
 
hii tasnia ya filamu na bongo fleva nadhani kwa sasa imebinafsishwa kwa lusifa.

Ni mapepo matupu watu wanalishwa, huwezi kukaa na watoto ukaangalia uchafu unaofanywa na hawa maajenti wa kuzimu.

Ukija kwenye miziki ni mapepo ya zinaa wanaingiziwa watu kupitia nyimbo na filam.

Sisi tuliozaliwa zamani tunakumbuka nyimbo za kina marehemu tx moshi wiliam, mzee ngurumo, dr remiy ongala, mbaraka mushee. Zilikuwa ni nyimbo zenye maadili na mafunzo kwa jamii tofauti na sasa.

Sasa hivi ni jehanam. Hangalia hata wasanii wenyewe. Yaani ni vituko ni maajenti kweli kweli.
 
Hivi huyo snura mushi anasali kanisa gani nikaonane na kiongozi wake wske huyo wa kiroho?
 
Hivi huyo snura mushi anasali kanisa gani nikaonane na kiongozi wake wske huyo wa kiroho?
 
Nimepata tu msemo mpya, but wimbo wa kijinga na uchezaji wake ni wa kijinga pia
 
Back
Top Bottom