BASHE: Hayati Magufuli aliniambia mfumo wa korosho ungefeli angenitumbua na Kuniweka ndani

BASHE: Hayati Magufuli aliniambia mfumo wa korosho ungefeli angenitumbua na Kuniweka ndani

mack255

JF-Expert Member
Joined
Aug 26, 2021
Posts
551
Reaction score
1,230
Bashe ametoa Siri aliyoificha kwa muda, kuwa Magufuli alitaka amtumbue na amuuweke ndani. CHEKI VIDEO


Waziri Bashe amesema, alipoteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Kilimo alikumbana na sakata la korosho ambapo ghala la Serikali lilijaa korosho, na korosho mpya zilikuwa zinaingia.

Ili kukabiliana na hilo akatoa kauli ya ununuzi binafsi wa korosho ambao utakuwa wa uwazi. Kauli hiyo aliitoa mkoani Lindi alipokuwa na Rais Magufuli ziarani.

Rais Magufuli alimuuliza kama mfumo anaoupendekeza utafanikiwa, ambapo Bashe alimhakikishia Rais kuwa mfumo huo utafanya kazi tofauti na mfumo wa Serikali kununua korosho.

Rais Magufuli akamwambia ikitokea mfumo huo umefeli atamtumbua na kumuweka ndani. Bashe akajibu kwa kumwambia Rais abariki mfumo huo na ataona matokeo.
 
Mzimu utawatesa sana
Sikiliza clip Bashe is such a gentleman; siku zote anamnenea vizuri Magufuli.

Anachosimulia ni kwamba alitoa wazo boss akauliza una uhakika na unachonadi, akajibu nina uhakika. Magufuli akasapoti mpango wake hadharani ila akamwambia ukibuma utajuta.

The guy is very loyal, yeye anataka kazi yake iongee kwa boss wake hata huyu aliyepo sio kuishi kwa kujipendekeza tu kama vijana wenzake ambao ni mawaziri.
 
Sikiliza interview Bashe is such a gentleman; siku zote anamnenea vizuri Maguful...
Maisha ya mtandaoni mengi ya kuigiza au hujui. Kwani lile sakata la kuiba hela hazina hela alizificha nani? watu wale wa kanda ya kaskazini kule ziwani kama sio bwasheee
 
Magufuli alikuwa na nguvu sana halafu kuna wajinga wajinga wanaamini hakushinda uchaguzi wa 2020
MJINGA NI WEWE UNAYEAMINI HIVYO NDIO MAANA MOLA akafanya yake Katika Maisha OGOPA SANA kumpa HAKI mwanadamu ya kukunung'unikia Kwa MUNGU kwa ULIYOMTENDEA kama vile Kumtia kilema Kutoa Uhai wake HAKIKA MUNGU hatakuacha MALIPO ya UOVU huo ni hapa hapa Duniani
Mwendazake Ananung'unikiwa mpaka LEO
 
Magufuli alikuwa na nguvu sana halafu kuna wajinga wajinga wanaamini hakushinda uchaguzi wa 2020
Nguvu ipi? ya kumtishia mtu Jela kisa katoa strategy yake?

Uchaguzi wa 2020 whether alishinda au hakushinda nani ataamini wakati mliuvuruga wazi wazi.

Mfano kata yangu hakukua na uchaguzi wa diwani Wala mbunge na walipita bila kupingwa!! Eti mgombea hawezi kujaza fomu wakati aligombea miaka yote tokea 2010!!

Funny enough eti kura za Urais voter turnout ya kata yetu ni zaidi ya 90% na JPM alichukua zoteee. Kuna vitu vilimchafua JPM na mojawapo ni hili.

Mimi naamini angechapa kazi tu bila kupambana na wapinzani angeshinda kihalali kabisa bila hata kuiba sema angepata 60% ila hiyo 84% hata mtoto anajua hakuipata!!
 
MJINGA NI WEWE UNAYEAMINI HIVYO NDIO MAANA MOLA akafanya yake Katika Maisha OGOPA SANA kumpa HAKI mwanadamu ya kukunung'unikia Kwa MUNGU kwa ULIYOMTENDEA kama vile Kumtia kilema Kutoa Uhai wake HAKIKA MUNGU hatakuacha MALIPO ya UOVU huo ni hapa hapa Duniani
Mwendazake Ananung'unikiwa mpaka LEO
Bush mpaka leo anadunda!
Obama mpaka leo anadunda na ameua watu wengi sana huko duniani kwa ajili ya maslahi yake!
.mungu wako angekuwa na akili kama angeiua CCM, maana mpaka leo bado inakutesa!
 
Back
Top Bottom