Bashiru v/s Sponsor: Kuna dalili mtu kutema au kutemeshwa mnofu soon

Bashiru v/s Sponsor: Kuna dalili mtu kutema au kutemeshwa mnofu soon

Msanii

Platinum Member
Joined
Jul 4, 2007
Posts
25,252
Reaction score
36,513
Mungu ni mwema sana sana.

Hivi sasa roho wa uharibifu ameanza kumalizia kazi yake ndani ya CCM, na tukae mkao wa soap series yenye maeneo mengi ya wanaCCM kutafunana wenyewe kwa wenyewe huku wakielekea kwenye anguko lao taradadi.

I am not joking. Nilishaona kuyumba kwa mwelekeo wa chama hiko since 2005 na hatimaye leo tunaahuhudia nyufa kubwa zisizorwkwbishika.

Hivi karibuni amesikika aliyewahi kuwa Katibu Mkuu CCM Taifa akiwahamasisha wanyonge hususani wakulima kuwavimbishia shingo wanyonyaji ambao ndiyo watawala akisema ni sharti wakubwa watimize wajibu na siyo sahihi kuwasifia sifia.

Kishindo hiki cha dafu kuanguka kutoka kwenye mti wa komamanga kumewaibua wapayukaji na wale wanaoongea huku akili zao zikiwa zimwfungiwa kwenye kasiki wakimnanga na kumuonya Bashiru kuwa hapaswi na hana haki ya kumkosoa kiongozi mkuu wa chama.

Kwa mnaotembelea mitandaoni, fuatilieni pia posts za chakubanga wetu kipepe mfukuza wahuni za hivi karibuni mtagundua kuwa kuna muunganiko usio wa kawaida na tukio la Katibu Mstaafu kutoa msimamo wake na kauli yake ya kwanza baada ya kuenguliwa Ukatibu na kung'olewa pale Ikulu.

Nasema muunganiko usio wa kawaida ni kwa sababu post yake ya mwisho ya bwana yule amerudia kauli yake iliyompelekea kuteuliwa ili kumziba mdomo inayohusu masela fulani wa kihuni.

Ninatabiri kuwa wawili hawa wanaweza kutema nyama ama kutemeshwa wakati wowote na upo uwezekano orodha ikawa ndefu na kilichokuwa kinasubiriwa ni nani ataanza kuongea wakati wa kula ili timua timua ianze.

Kwa ninavyoifahamu CCM inachoangalia ni nafasi yake kuendelea kushika dola hata kama kuna nafsi kadhaa zitakazopaswa kukutanishwa na Ziraili.

Bado msimamo na imani yangu kwamba Watanzania tusiwe moved na drama maana chama dola kina hulka ya kuja na episodes zinazosisimua nyakati za kuelekea uchaguzi lakini this time wamemeza mwiba wa pono na umenasa kooni.

Screenshot_20221121_034403.jpg


#KataaCCMuliokoeTaifa
 
Bashiru ni takataka, wakati amechaguliwa katibu Mkuu wa CCM alisema hicho ni cheo chake cha mwisho, lakini akachaguliwa katibu Mkuu kiongozi na akakubali. Na sasa amepewa ubunge wa viti maalum na amekubali. Mtu wa aina hiyo hata akitemeshwa ulaji ni sawa na hana kitu atafanya.
 
Bashiru nduli aliyetamka wazi bila aibu CCM itatumia dola kukaa madarakani na ndiye alikuwa Engineer wa wizi mkubwa wa kura kuwahi kutokea Tanzania, aliiba viti vya ubunge na kuwabambikia wapinzani kesi na wengine kufungwa maisha, walitumia state organs kama usalama kuua upinzani na wapinzani au yeyote asiyekubaliana na agenda zao, wafanyabiashara na wananchi walikuwa terrorized usiku na mchana, neno kama watu wasiojulikana, utekaji, viroba etc ilikuwa ndio hali halisi Tanzania, nduli yeyote hatakiwi kuwa karibu na nafasi ya uongozi anatakiwa kuwa jela
 
Bashiru nduli aliyetamka wazi bila aibu CCM itatumia dola kukaa madarakani na ndiye alikuwa Engineer wa wizi mkubwa wa kura kuwahi kutokea Tanzania, aliiba viti vya ubunge na kuwabambikia wapinzani kesi na wengine kufungwa maisha, walitumia state organs kama usalama kuua upinzani na wapinzani au yeyote asiyekubaliana na agenda zao, wafanyabiashara na wananchi walikuwa terrorized usiku na mchana, neno kama watu wasiojulikana, utekaji, viroba etc ilikuwa ndio hali halisi Tanzania, nduli yeyote hatakiwi kuwa karibu na nafasi ya uongozi anatakiwa kuwa jela
Lakini si alisema kweli kuhusu kutumia dola au aliongea uongo.
 
Bashiru huyu Ambae Ni zero form six
ambaye kaingizwa udsm na kinyondo with unequalify Marks na baadae kuja KUSOMA degree yake ya Mchongo

BASHIRU Ni muhuni Sana

Hana Exposure kuhusu SIASA
Za nchi hii Tanzania.
Wewe uliyeingia 1.7 vipi?
Mjibuni hija Zeke tu kama kadanganya sawa
 
Chadema na walamba asali dhidi ya wananchi wenye nchi.

Hii sio ya kukosa.
 
Kwa mnaotembelea mitandaoni, fuatilieni pia posts za chakubanga wetu kipepe mfukuza wahuni za hivi karibuni mtagundua kuwa kuna muunganiko usio wa kawaida na tukio la Katibu Mstaafu kutoa msimamo wake na kauli yake ya kwanza baada ya kuenguliwa Ukatibu na kung'olewa pale Ikulu.
 
Kwanza alienda kwenye mle mkutano kama nani? alialikwa na nani? Mimi napata na hawa CCM hichi ni chama ilikuwa zamani ukienda kinyume nao hadharani ulikuwa unaitwa kwenye vikao vyao na ambulance inasubiri nje utapigwa nyundo humo ukitoka kama umetoka uchi leo hii Bashiru sijui polepole wanasimama kuchallenge Chama? Leo Bashiru anajifanya kawa Ronaldo? hata Ronaldo Man u wanamshughulikia mtu mwenye ushawishi mkubwa sembuse Bashiru. CCM mnatuangusha sana...
 
Kwa mnaotembelea mitandaoni, fuatilieni pia posts za chakubanga wetu kipepe mfukuza wahuni za hivi karibuni mtagundua kuwa kuna muunganiko usio wa kawaida na tukio la Katibu Mstaafu kutoa msimamo wake na kauli yake ya kwanza baada ya kuenguliwa Ukatibu na kung'olewa pale Ikulu.
Wamoja hao.
Hasira za kuzuiwa usajili wao.

Waache wanyofoane macho. Sisi tunaitaka Tanzania yetu salama
 
Back
Top Bottom