Bashungwa: Barabara za mwendokasi ambazo hazijaanza kutumika, zitumike kwa magari binafsi ili kupunguza foleni

Bashungwa: Barabara za mwendokasi ambazo hazijaanza kutumika, zitumike kwa magari binafsi ili kupunguza foleni

Waziri wa Ujenzi wa Tanzania Innocent Bashungwa ametoa ushauri wa Mamlaka husika kuruhusu barabara zinazotumiwa na Mabasi ya ‘Mwendokasi’ ziwe zinatumika na magari binafsi hususani wakati wa asubuhi kwenye kuwahi kazini na jioni wakati wa kurudi nyumbani na kusema hiyo itapunguza foleni hasa ukizingatia wakati huu ambao mabasi ya mwendokasi yapo machache.

Akiongea Jijini Dar es salaam leo October 22,2024 wakati wa hafla ya utiaji saini ujenzi wa daraja la Jangwani, Bashungwa amesema wazo hilo linaweza kufanyiwa kazi wakati huu ambao mabasi yako machache lakini pale Mabasi mapya yatakapoanza kazi utaratibu wa zamani utaendelea.

“Wakati foleni ikiwa kali ama ni asubuhi Watu wanaenda kazini au jioni Watu wanatoka kazini kwenda nyumbani naona zile njia za BRT tukishirikiana na Jeshi la Polisi naona haja ya kuweka utaratibu ambao utapunguza foleni, mabasi yatakapokuja tunasitisha lile zoezi lakini haileti maana unakutana Wananchi wapo kwenye foleni halafu katikati (barabara za mwendokasi) unakuta peupe kuanzia point A hadi point B”

“Kwanini tusikae na Jeshi la Polisi, TAMISEMI tukakubaliana lini mabasi mapya yatakuja na kabla mabasi hayajaja basi uratibu wa Matrafiki ku-controll magari, hata hizi barabara zitumike, mabasi yakija tutarudi kwenye utaratibu wa kawaida ili kwa sasa tupunguze foleni, kwahiyo Mh. RC ili naomba nikuachie uratibu” ——— Waziri Bashungwa...

Hili wazo hata Mimi naliunga mkono na liwe endelevu tuView attachment 3133215
Mbona Hakufanya Hivyo alipokuwa Waziri wa TAMISEMI??
 
“Kwanini tusikae na Jeshi la Polisi, TAMISEMI tukakubaliana lini mabasi mapya yatakuja na kabla mabasi hayajaja basi uratibu wa Matrafiki ku-controll magari, hata hizi barabara zitumike, mabasi yakija tutarudi kwenye utaratibu wa kawaida ili kwa sasa tupunguze foleni, kwahiyo Mh. RC ili naomba nikuachie uratibu” ——— Waziri Bashungwa...
 
Au wamemnukuu vibaya? Walahi napata wakati mgumu kuelewa.
Mimi nafikiri anamaanisha zile njia ambazo mwendokasi haijaanza kazi kama kilwa road. Ila kama anamaanisha morogoro road kwa kweli anastahili msaada wa kimawazo. Namuona kama mmoja wa mawaziri wanaojitambua
 
Kilwa road kuanzia uhasibu hadi posta ni kawaida tunatumia sana njia ya mwendokasi. Magari hayajaanza kazi kwanin ? Ingawa kuna siku wanafunga eti mkandarasi analalamika miundombinu inachakaa
Juzi na Jana nimepita kwenye mwendokasi kuanzia pale mataa ya kamata,darajani PUMA,mivinjeni,mtongani Hadi mbagala kizuian
 
Waziri wa Ujenzi wa Tanzania Innocent Bashungwa ametoa ushauri wa Mamlaka husika kuruhusu
Waziri wa Ujenzi Innocent Bashungwa amefunguka na kueleza kuwa pawepo na matumizi ya Barabara za magari ya Mwendokasi ambazo hazijaanza kutumika ili ziweze kupunguza foleni.
ziwe zinatumika na magari binafsi hususani wakati wa asubuhi kwenye kuwahi kazini na jioni wakati wa kurudi nyumbani na kusema hiyo itapunguza foleni hasa ukizingatia wakati huu ambao mabasi ya mwendokasi yapo machache.

Akiongea Jijini Dar es salaam leo October 22,2024 wakati wa hafla ya utiaji saini ujenzi wa daraja la Jangwani, Bashungwa amesema wazo hilo linaweza kufanyiwa kazi wakati huu ambao mabasi yako machache lakini pale Mabasi mapya yatakapoanza kazi utaratibu wa zamani utaendelea.

“Wakati foleni ikiwa kali ama ni asubuhi Watu wanaenda kazini au jioni Watu wanatoka kazini kwenda nyumbani naona zile njia za BRT tukishirikiana na Jeshi la Polisi naona haja ya kuweka utaratibu ambao utapunguza foleni, mabasi yatakapokuja tunasitisha lile zoezi lakini haileti maana unakutana Wananchi wapo kwenye foleni halafu katikati (barabara za mwendokasi) unakuta peupe kuanzia point A hadi point B”

“Kwanini tusikae na Jeshi la Polisi, TAMISEMI tukakubaliana lini mabasi mapya yatakuja na kabla mabasi hayajaja basi uratibu wa Matrafiki ku-controll magari, hata hizi barabara zitumike, mabasi yakija tutarudi kwenye utaratibu wa kawaida ili kwa sasa tupunguze foleni, kwahiyo Mh. RC ili naomba nikuachie uratibu” ——— Waziri Bashungwa...

Hili wazo hata Mimi naliunga mkono na liwe endelevu tuView attachment 3133215
An argument from the person with a short-sighted mind.
Huyu Waziri anapaswa akumbuke kwamba Kabla ya kutafuta suluhisho kuhusu tatizo lolote lile ni LAZIMA kwanza afanye utafiti wa kina kabisa ili kujua chanzo halisi cha tatizo husika.
Baada ya kujua chanzo cha tatizo ndipo Sasa anaweza akatafuta suluhisho au utatuzi wake.
Aidha, daima anapaswa akumbuke kwamba muda wowote ule anapotaka kufanya Uamuzi wa kudumu ni LAZIMA azingatie sababu za kudumu. Asiwe anakurupuka katika kufanya Maamuzi.

KIINI cha kuwepo kwa Janga la foleni za barabarani katika mifumo ya usafiri na usafirishaji katika Mji wa Dsm ni kutokana na kukosekana kwa Mipango-miji, kuna tatizo la kifo cha taaluma ya Mipango-miji katika nchi hii.
 
Iwapo wataruhusu tu basi hakuna cha kukataza tena maana tunajijua
Angalia walipoambiwa jamaa zetu zile hela za kubrashi walivyoongeza kasi kuzidai
Na mwingine akasema kuleni kiasi, ndio akafungulia ziliwe zote

Who let the Dogs out?
 
Wazo zuri sana.
Ingependeza gari za Abiria tu ndio zipite Mwendokasi Asubuhi na Jioni ili kuwawahisha Wafanyakazi Makazini.
Ila Malori ya mizigo yapite njia ya kawaida.
Kuyapitisha Malori kwenye Mwondokasi ni kuharibu Barabara na pia kuongeza foleni kwakuwa mengi yanaharibikia barabarani na kusababisha foleni muda mwingi.
Naunga mikono Hoja.
 
Back
Top Bottom