Basi la TFF kukamatwa, kupigwa mnada kulipa deni

Basi la TFF kukamatwa, kupigwa mnada kulipa deni

Kitimoto

JF-Expert Member
Joined
Aug 25, 2012
Posts
6,941
Reaction score
7,808
BAADA ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam kuliamuru Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kulipa deni la Sh 56,446,700, wakili wa Taasisi za Filbert Bayi, Karoli Tarimo amefungua maombi kukazia hukumu akiiomba mahakama iruhusu kulikamata basi la TFF lenye namba za usajili T581 CGR liuzwe ili kulipa deni hilo.

Taasisi hiyo inaidai TFF fedha hizo kwa miaka mitatu ambazo kwa mujibu wa Tarimo zilikuwa ni gharama ya kambi kwa timu za vijana chini ya miaka 13, 15, 17 na ile ya wanawake katika taasisi hiyo Kibaha mkoani Pwani.

Alisema Juni 3, 2019 taasisi hiyo iliingia makubalino na TFF ya miaka mitatu kutoa huduma za viwanja, usafiri, kambi na chakula wenye thamani ya Sh521.4 milioni ambazo walikubaliana zilipwe kwa awamu na kusalia Sh76.4 milioni ambazo Julai 20, mwaka jana rais wa TFF, Wallace Karia alikiri katika mahojiano na gazeti hili na kusema suala hilo lilikuwa linashughulikiwa.

mwanaspoti_tz~p~CgdvVkoKjof~1.jpg
 
Manara ni special guy amechangamsha na kuipaisha juu mno ligi ya Tanzania bara huu ni ukweli mchungu japo inaeleweka ana kauli za kukera na kuumiza sana mioyo ya anaowaponda, sasa huyu jamaa ukimgusa ukimunder estimate tu na kumuonea na kumkomoa tayari ushajiharibia, ni mikosi tu inaanza kukuandama kama Karia eti kamfungia kwa kumwambia ukweli tu hataki kufuatwafuatwa sasa hapo Karia kaingia cha kike sasa ataisoma namba mpaka akome huu ni mwanzo tu wa anguko lake , sijui huyu Bugatti ana kitu gani Mungu anajua, jamaa akihama timu inakufa kama Simba wamedorora na wanaboa kinoma kwa kubaki na furushi la hasira na matusi tu na Simba inaweza kufa kabisa wakizembea!

TFF timu ya Taifa Stars ina kocha mzee kaishiwa mbinu bado wanae tu tunapigwa home na Algeria hata kusikia wamemkaripia kocha hamna weka Mgunda wewe Kolo Fc Karia.

Basi liuzwe deni lilipwe Karia na wenzake watoke TFF Makolo wale hawana akili ya mpira ni promo tu wanajua!

What goes around comes around!! malipo hapa hapa Lupaso!
 
Manara ni special guy amechangamsha mno ligi ya Tanzania bara huu ni ukweli mchungu sasa ukimgusa tu na kumuonea na kumkomoa tayri ushajiharibia ni mikosi tu inaanza kukuandama kama Karia kaingia cha kike sasa ataisoma namba mpaka akome huu ni mwanzo tu wa anguko lake , sijui huyu Bugatti ana kitu gani Mungu anajua, jamaa akihama timu inakufa kama Simba wamedorora na wanaboa kinoma kwa kubaki na furushi la hasira na matusi tu na Simba inaweza kufa kabisa wakizembea!
Habari inahusu basi la TFF we umehamia kwa Manara
 
Manara ni special guy amechangamsha mno ligi ya Tanzania bara huu ni ukweli mchungu sasa ukimgusa tu na kumuonea na kumkomoa tayri ushajiharibia ni mikosi tu inaanza kukuandama kama Karia kaingia cha kike sasa ataisoma namba mpaka akome huu ni mwanzo tu wa anguko lake , sijui huyu Bugatti ana kitu gani Mungu anajua, jamaa akihama timu inakufa kama Simba wamedorora na wanaboa kinoma kwa kubaki na furushi la hasira na matusi tu na Simba inaweza kufa kabisa wakizembea!

TFF timu ya Taifa Stars ina kocha mzee kaishiwa mbinu bado wanae tu tunapigwa home na Algeria hata kusikia wamemkaripia kocha hamna weka Mgunda wewe Karia.
Kweli mashabiki wa yanga ni vilaza. Sasa hapa kuna uhusiano gani hapa.
 
Manara ni special guy amechangamsha mno ligi ya Tanzania bara huu ni ukweli mchungu sasa ukimgusa tu na kumuonea na kumkomoa tayri ushajiharibia ni mikosi tu inaanza kukuandama kama Karia kaingia cha kike sasa ataisoma namba mpaka akome huu ni mwanzo tu wa anguko lake , sijui huyu Bugatti ana kitu gani Mungu anajua, jamaa akihama timu inakufa kama Simba wamedorora na wanaboa kinoma kwa kubaki na furushi la hasira na matusi tu na Simba inaweza kufa kabisa wakizembea!

TFF timu ya Taifa Stars ina kocha mzee kaishiwa mbinu bado wanae tu tunapigwa home na Algeria hata kusikia wamemkaripia kocha hamna weka Mgunda wewe Karia.

Basi liuzwe Karia na wenzake watoke Makolo wale hawana akili ya mpira ni promo tu wanajua!
Hapo ndo mnapokosea, sehemu kubwa ya soka la Tz ashikuriwe Simba kimataifa, ashukuriwe MO kwa mabadiliko, ishukuriwe Azam...

Huyo zeruzeru Simba ndo imemfikisha hapo alipo
 
nimeelewa aisee maana ya akili
1. Kushabikia Makolo FC inayoongozwa na demu, isiyo na uwezo uwanjani, isiyo na pesa za usajili wa kiwango, isiyo na kombe hata moja kabati limejaa vumbi

2. Kumponda Manara hata kama kaonewa kwa vile tu kahama simba imedorora na inaboa!

3. Kumsifia Kolo Karia ambae hafai TFF inafungwa tu na ina madeni na bus linaenda Filbert Bay I!

4. Kukaa kimya na kumeza mawazo yenye takataka ya wanasimba ambao ni mataahira wana hasira za timu yao mbovu
5.
6.
 
Manara ni special guy amechangamsha mno ligi ya Tanzania bara huu ni ukweli mchungu sasa ukimgusa tu na kumuonea na kumkomoa tayri ushajiharibia ni mikosi tu inaanza kukuandama
Kwa hiyo kama Manara asingeguswa, deni lingesamehewa? Wakati mwingine huwa natamani kuwepo masharti ya viwango vya elimu kwa anayetaka kujiunga JF
 
Kwa hiyo kama Manara asingeguswa, deni lingesamehewa? Wakati mwingine huwa natamani kuwepo masharti ya viwango vya elimu kwa anayetaka kujiunga JF
elimu ni nini? tuanzie hapo weka ubishoo pembeni!
 
Back
Top Bottom