BAVICHA: Tumesikitishwa na tunalaani kitendo cha BASATA kuufungia wimbo wa ‘MAMA'

BAVICHA: Tumesikitishwa na tunalaani kitendo cha BASATA kuufungia wimbo wa ‘MAMA'

Baraza la Vijana wa Chadema (BAVICHA) tumesikitishwa na tunalaani kitendo cha Baraza la Sanaa la Tanzania (BASATA) kuufungia wimbo uitwao ‘MAMA’ ulioimbwa na Msanii wa Mziki wa Kizazi Kipya, Emmanuel Elibariki (Ney wa Mitego).

Mbali ya kuufungia wimbo huo, Basata limemwagiza kusitisha mara moja kupeleka wimbo huo katika vyombo vya habari pamoja na mitandao ya kijamii kwa madai ya kwamba unakinzana na Kanuni za Basata za mwaka 2018, kanuni ya 25 (6) (d) na (i);

“Baraza katika kuhakiki maadili katika maudhui ya kazi za sanaa, litajiridhisha kuwa kazi ya sanaa;
(d) Haina maneno ya uongo, uchochezi au yanayokashifu watu wengine.
(i) Haidhoofishi umoja, ushirikiano na ustawi bora wa jamii.”

Bavicha baada ya kuusikiliza wimbo huo wa MAMA wa Msanii Ney wa Mitego hatujaona uongo, uchochezi wala kashfa yoyote zinazodaiwa na Basata kuwa sababu za kuufungia wimbo huo. Wala haudhoofishi umoja, ushirikiano na ustawi bora wa jamii yetu.

Huu ni mwendelezo wa Serikali kuweka taratibu za kisheria kwa makusudi ya kuminya uhuru wa maoni, fikra, mawazo ya kisanaa na kuwapangia maudhui wasanii katika kazi zao.

Aidha, Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeruhusu uhuru wa mawazo, Ibara ya 18 (1) ”Bila ya kuathiri sheria za nchi, kila mtu yuko huru kuwa na maoni yoyote na kutoa nje mawazo yake, na kutafuta, kupokea na kutoa habari na dhana zozote kupitia chombo chochote bila ya kujali mipaka ya nchi, na pia ana uhuru wa mawasiliano yake kutoingiliwa kati.”

Uamuzi wa Basata umevunja haki hiyo ya Katiba na umeingilia haki na uhuru wa Msanii Ney wa Mitego kutoa maoni yake.

Bavicha tunatambua kuwa, Wabunge wa Chadema wakati wa Bunge la 11, walipinga kutungwa kwa taratibu hizo kwa sababu zinaminya na kuua ubunifu katika kazi za sanaa. Lakini kutokana na nia ovu ya Serikali iliyopita na wingi wa Wabunge wa CCM, sheria hizo zilipitishwa na sasa tunaona matokeo yake.

Bavicha tunawataka wasanii washikamane na kuwa wamoja katika suala hili na kupinga matumizi ya kanuni hizi mbovu ambazo zitaua vipaji vya sanaa, kuua ndoto za vijana wengi, kuhatarisha ajira za vijana wengi na mapato yanayotokana na kazi za sanaa.

Imetolewa leo Mei 06, 2021 na,

Twaha Mwaipaya
Mratibu wa Uhamasishaji,
Bavicha Taifa.

Chama cha watu. Uhuru haki na maendeleo ya watu.
 
Bwacha na bavicha sasa hivi wamechukua nafasi ya mataga kusifia ccm
Afadhali umekiri mwenyewe kuwa WANASIFIA. Kwa sababu enzi za Mwendazake mulikuawa mnasema wapinzani wanapinga kila kitu, sasa kwa maneno yako haya umekiri mwenyewe kuwa Wapinzani Hawapingi kila kitu,vingine vikiwa vizuri wanasifia.

Tunashukuru ndugu Mataga kwa kuliweka hili vizuri
 
Afadhali umekiri mwenyewe kuwa WANASIFIA. Kwa sababu enzi za Mwendazake mulikuawa mnasema wapinzani wanapinga kila kitu, sasa kwa maneno yako haya umekiri mwenyewe kuwa Wapinzani Hawapingi kila kitu,vingine vikiwa vizuri wanasifia.

Tunashukuru ndugu Mataga kwa kuliweka hili vizuri
Maccm hayana jema. Leo yamebadilika tena.
 
Maisha yanabadilika sana.
Kuna watu hadi leo hawaamini kilichotokea.

Ukweli Zama za Mzee watu waliumia ndani ya mioyo tena sana tena waliumia kwa maonevu kabisa,Wakajitahidi onesha tabasamu usoni ila ndani moyo ukiwa wavuja dam.

Ila sa hivi wanaoumia wanaumia kwa wivu .
Mama kuachia vyomho vya habari viwe huru watu wanaumia .
Mama kutaka kuongea na wapinzani kuwaskiza watu wanaumia.
Mama kutaka kufungua mipaka watu wanaumi.

Si kwamba mama hakosei ila anakosea kama binadamu ila ukweli anaonesha fraha na amani kwa watu sio maubabe ,na kuonea makundi flani.
Yaaan Wajukuu wamzee wanaumia tuu kwa kupenda kujiumiza mana walizoea kandamiza upande mwingine wao wakishangilia. Na sa hivi mama hana hataki kuweka ma genge ya kijinga au makundi.

Nyimbo iko wazi kabisa shida wanataka ukweli usiwekwe wazi tuendele kama zama zile zile
Sasa kama waliumia kwann waendelee kushikilia maumivu ingekua waliumia kama mnavyo Sema wala msingekua mnalaum
 
Inshu sio kusifia ccm, hujiulizi ni kwanini kibao kimegeuka?!wapinzani wanampenda Mama, wakati ma CCM, wanamchukia?kwani mama anatanguliza maslahi ya nchi kwanza badala ya ccm, na ndio kitu cha muhimu.Sasa ccm mnaumia kwani mlizoeshwa siasa za kishamba za kuona aliye na mawazo tofauti na mwenyekiti wenu ni mzandiki!!
Anatanguliza Maslahi ya nchi mbele sawa sawa, badae msije mkasema ccm ni ile ile na huyo Mama ukamkataa, maana binadamu wana tabia za kinyonga
 
Yaan hawana policy,hawana majukumu.Ila ni vurugu tupu.Halafu huyu yeye Ney ,hana nyimbo kama kina Diamond. Ni nyimbo za siasa tu.
 
Anatanguliza Maslahi ya nchi mbele sawa sawa, badae msije mkasema ccm ni ile ile na huyo Mama ukamkataa, maana binadamu wana tabia za kinyonga
Vyovyote itakavyokuwa lakini hawezi fikia kiwango cha unyama cha bwana yule!!kwani daa yule alikuwa sio binadamu
 
Kwani sio wapinzani hawahawa walimsifia JPM alipoingia na kusema anatumia sera za chadema ikiwa ni ku represent hate zao kwa JK ambaye soon wakamwita malaika?

Hatujawahi kuwa na serious upinzani[emoji16][emoji16]
Inshu sio kusifia ccm, hujiulizi ni kwanini kibao kimegeuka?!wapinzani wanampenda Mama, wakati ma CCM, wanamchukia?kwani mama anatanguliza maslahi ya nchi kwanza badala ya ccm, na ndio kitu cha muhimu.Sasa ccm mnaumia kwani mlizoeshwa siasa za kishamba za kuona aliye na mawazo tofauti na mwenyekiti wenu ni mzandiki!!
 
Kwani sio wapinzani hawahawa walimsifia JPM alipoingia na kusema anatumia sera za chadema ikiwa ni ku represent hate zao kwa JK ambaye soon wakamwita malaika?

Hatujawahi kuwa na serious upinzani[emoji16][emoji16]
Ki ukweli MEKO, alianza vizuri hasa kwenye vita dhidi ya rushwa, na uzembe kazini!!lakini kadri siku zilivyoenda ndio akazidi kujipambanua ngozi yake!!kama ni jeshini alianza na cheo cha GENERAL, ila cha kusikitisha ameondoka na cheo kama MGAMBO!!!
 
Hao wasanii wa bongo Acha wapambane na hali zao wenyewe

Ova
 
Ukweli alivyoimba kuponda viongozi bila ushahidi pia si sahihi

Yuko Chadema LAKINI TUHUMA ALIZOWAKILISHA HAZINA USHAHIDI

PILI HAJUI MAJUKUMU YA RAISI.majukumu yake sio kuingilia mambo ya bunge ya akina Halima mdee

kifupi alichoimba ni ujinga mtupu uliojaa uchochezi na tuhuma zisizo na ushahidi

pole yake kwa kupoteza pesa za kurekodi studio heri angefungua genge
 
Na nyie acheni kimbelembele.
Mnawapigania mwisho wa siku wanaenda kufanya kampeni CCM.
Acha waumizwe
 
CCM wamezoea mbeleko.... Hivi mwana FA washindane kwa hoja na Godbless Lemma/ au yule meneja wa diamond umweke na Zitto.... Mama anataka mjadala wa wazi bungeni(amesifia bunge la Kenya,huwa anaskiliza)...
 
BASATA bado ipo ktk "MODE" ya mwendazake! Bado jinamizi la Jiwe linawaandama.
Midhali kuna Wizara inayohusu utamaduni na wako maafisa utamaduni SIONI HAJA YA KUWEPO "BASATA" kwani inaendeshwa kwa mihemko ya kisiasa badala ya weledi.
Ama kukosoa na kufariji walioachiwa madonda kwa basata huenda ni makosa...
Ingekuwa ni rahisi wao BASATA wangetunga na kuimba nyimbo zao ingependeza...
Wakifungia walipe na fidia...
 
Baraza la Vijana wa Chadema (BAVICHA) tumesikitishwa na tunalaani kitendo cha Baraza la Sanaa la Tanzania (BASATA) kuufungia wimbo uitwao ‘MAMA’ ulioimbwa na Msanii wa Mziki wa Kizazi Kipya, Emmanuel Elibariki (Ney wa Mitego).

Mbali ya kuufungia wimbo huo, Basata limemwagiza kusitisha mara moja kupeleka wimbo huo katika vyombo vya habari pamoja na mitandao ya kijamii kwa madai ya kwamba unakinzana na Kanuni za Basata za mwaka 2018, kanuni ya 25 (6) (d) na (i);

“Baraza katika kuhakiki maadili katika maudhui ya kazi za sanaa, litajiridhisha kuwa kazi ya sanaa;
(d) Haina maneno ya uongo, uchochezi au yanayokashifu watu wengine.
(i) Haidhoofishi umoja, ushirikiano na ustawi bora wa jamii.”

Bavicha baada ya kuusikiliza wimbo huo wa MAMA wa Msanii Ney wa Mitego hatujaona uongo, uchochezi wala kashfa yoyote zinazodaiwa na Basata kuwa sababu za kuufungia wimbo huo. Wala haudhoofishi umoja, ushirikiano na ustawi bora wa jamii yetu.

Huu ni mwendelezo wa Serikali kuweka taratibu za kisheria kwa makusudi ya kuminya uhuru wa maoni, fikra, mawazo ya kisanaa na kuwapangia maudhui wasanii katika kazi zao.

Aidha, Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeruhusu uhuru wa mawazo, Ibara ya 18 (1) ”Bila ya kuathiri sheria za nchi, kila mtu yuko huru kuwa na maoni yoyote na kutoa nje mawazo yake, na kutafuta, kupokea na kutoa habari na dhana zozote kupitia chombo chochote bila ya kujali mipaka ya nchi, na pia ana uhuru wa mawasiliano yake kutoingiliwa kati.”

Uamuzi wa Basata umevunja haki hiyo ya Katiba na umeingilia haki na uhuru wa Msanii Ney wa Mitego kutoa maoni yake.

Bavicha tunatambua kuwa, Wabunge wa Chadema wakati wa Bunge la 11, walipinga kutungwa kwa taratibu hizo kwa sababu zinaminya na kuua ubunifu katika kazi za sanaa. Lakini kutokana na nia ovu ya Serikali iliyopita na wingi wa Wabunge wa CCM, sheria hizo zilipitishwa na sasa tunaona matokeo yake.

Bavicha tunawataka wasanii washikamane na kuwa wamoja katika suala hili na kupinga matumizi ya kanuni hizi mbovu ambazo zitaua vipaji vya sanaa, kuua ndoto za vijana wengi, kuhatarisha ajira za vijana wengi na mapato yanayotokana na kazi za sanaa.

Imetolewa leo Mei 06, 2021 na,

Twaha Mwaipaya
Mratibu wa Uhamasishaji,
Bavicha Taifa.

BASATA wanataka kila msanii aimbe wimbo kama ule wa Magufuli baba lao
 
Baraza la Vijana wa Chadema (BAVICHA) tumesikitishwa na tunalaani kitendo cha Baraza la Sanaa la Tanzania (BASATA) kuufungia wimbo uitwao ‘MAMA’ ulioimbwa na Msanii wa Mziki wa Kizazi Kipya, Emmanuel Elibariki (Ney wa Mitego).

Mbali ya kuufungia wimbo huo, Basata limemwagiza kusitisha mara moja kupeleka wimbo huo katika vyombo vya habari pamoja na mitandao ya kijamii kwa madai ya kwamba unakinzana na Kanuni za Basata za mwaka 2018, kanuni ya 25 (6) (d) na (i);

“Baraza katika kuhakiki maadili katika maudhui ya kazi za sanaa, litajiridhisha kuwa kazi ya sanaa;
(d) Haina maneno ya uongo, uchochezi au yanayokashifu watu wengine.
(i) Haidhoofishi umoja, ushirikiano na ustawi bora wa jamii.”

Bavicha baada ya kuusikiliza wimbo huo wa MAMA wa Msanii Ney wa Mitego hatujaona uongo, uchochezi wala kashfa yoyote zinazodaiwa na Basata kuwa sababu za kuufungia wimbo huo. Wala haudhoofishi umoja, ushirikiano na ustawi bora wa jamii yetu.

Huu ni mwendelezo wa Serikali kuweka taratibu za kisheria kwa makusudi ya kuminya uhuru wa maoni, fikra, mawazo ya kisanaa na kuwapangia maudhui wasanii katika kazi zao.

Aidha, Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeruhusu uhuru wa mawazo, Ibara ya 18 (1) ”Bila ya kuathiri sheria za nchi, kila mtu yuko huru kuwa na maoni yoyote na kutoa nje mawazo yake, na kutafuta, kupokea na kutoa habari na dhana zozote kupitia chombo chochote bila ya kujali mipaka ya nchi, na pia ana uhuru wa mawasiliano yake kutoingiliwa kati.”

Uamuzi wa Basata umevunja haki hiyo ya Katiba na umeingilia haki na uhuru wa Msanii Ney wa Mitego kutoa maoni yake.

Bavicha tunatambua kuwa, Wabunge wa Chadema wakati wa Bunge la 11, walipinga kutungwa kwa taratibu hizo kwa sababu zinaminya na kuua ubunifu katika kazi za sanaa. Lakini kutokana na nia ovu ya Serikali iliyopita na wingi wa Wabunge wa CCM, sheria hizo zilipitishwa na sasa tunaona matokeo yake.

Bavicha tunawataka wasanii washikamane na kuwa wamoja katika suala hili na kupinga matumizi ya kanuni hizi mbovu ambazo zitaua vipaji vya sanaa, kuua ndoto za vijana wengi, kuhatarisha ajira za vijana wengi na mapato yanayotokana na kazi za sanaa.

Imetolewa leo Mei 06, 2021 na,

Twaha Mwaipaya
Mratibu wa Uhamasishaji,
Bavicha Taifa.

Wimbo umejaa u-BAVICHA, haufai kabisa
 
Back
Top Bottom