KERO Bayport na Banc ABC wanapata wapi namba zetu za simu na kutumbua na meseji zao?

KERO Bayport na Banc ABC wanapata wapi namba zetu za simu na kutumbua na meseji zao?

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
A

Anonymous

Guest
Mimi ni mtumishi wa serikali. Kuna malalamiko yaliwahi pia kuandikwa hapa siku za nyuma lakini lile tatizo nadhani limezidi maradufu. Kampuni za mikopo mfano Bayport, Manoto Bank, ABC na zingine zimekuwa zikituma meseji za huduma zao wakati sijawahi kujiunga wala kujaza fomu zao.

Kwa mfano hao Manoto nimeshawapigia sana kuwaomba wanitoe lakini walinijibu haiwezekani, mfumo wetu hauruhusu kumtoa mtu akishwekwa tena kwa jeuri tukagombana akakata simu. Imekuwa kero na mpaka sasa karibia kwa wiki napokea meseji mara mbili.

Nani anatoa taarifa zetu kwao? Sheria mpya inasemaje kuhusu ukusanyaji wa taarifa za watu? Kwa sheria mpya naweza kuwafungulia kesi? Imekuwa hatua nitafute mwanasheria mzuri nipate fidia. Waziri wa mawasiliano na wa fedha hili limewashinda kabisa kuwadhibiti hawa watu?
 
Kwa Nape

Nenda kawafungulie mashtaka, wakili wa kujitegemea niko hapa.
 
Shida ni kubwa, kuna hawa Tigo na simu za mkopo, full of sht
 
Hizi message zao zinakuathiri kiasi gani?
 
Ni kweli kabisa jamaa sijui wanajuaje wale,ipo sehemu wanapata taarifa wakikutumia sms potezea tu na wanajua kushawishi vibaya mno.
 
Back
Top Bottom