BBC, habari za moto Mlima Kilimanjaro anaripoti mwandishi kutoka Kenya, ni sahihi?

Aisee kumbe likes za mabeberu zilikua nyingi eh?
 
aisee kumbe likes za mabeberu zilikua nyingi eh?
Na issue sio likes ww

Tukio lina tokea nchin kwako ww mwana habari hujui anatoka mtu toka nje ya nchi ana kujanku ripoti tukio ilo then mwanahabari ana kenua meno tu

Ata lile tukionla wanyama kuhama toka Tz kwenda Kenya wana habari wa tz walikuwa hawajui ni mpaka walipo kujaa CGTN waka rusha live bac ndio ikawa story globally.
 
kwa wanahabari hawa kina Pasco njaa kali hadi kwenye kope usitegemee chochote zaidi ya mapambio ya kusifu na kuabudu.
 
Vyombo vya habari vimeshaambiwa visiripoti kitu ambacho hakija thibitishwa na Serikali wakifanya hivyo wanafungiwa sasa wameamua kukaa pembeni, wakiripoti serikali itawajia juu na kuwaambia wanaichafua nchi yao, usishangae ndio sheria inavyo wataka waandishi wa kitanzania wakae pembeni kama kufungiwa na kulipa faini wamefanyiwa hivyo sana. labda anaweza akaripoti mtangazaji wa TBC maana wao ndio wenye serikali na hawawezi kufanywa lolote
 
Nafikiri hukumuelewa Mtoa mada. Yeye alimtaka Mwandishi yule wa BBC kufika kwenye eneo la tukio kisha kuripoti habari ile. Yaani angesema "Nikiripoti kutoka eneo la Ml. Kilimanjaro ni mimi...
 
Sirika la mabeberu, Watangazaji wao wana utimamu kushinda sisi kwaiyo tusiwapingie cha kutangaza na nani aripoti habari zipi.
 
Duuh yaani Lisu anagombea Urais Mlima unaungua, ni wa kumkataa, akishinda mlima unaweza bomoka kabisa.
 
Mwandishi wa habari na kituo cha radio au tv kikiripoti habari yoyote mbaya inayoonesha uzembe au udhaifu wa srekla na mamlaka zake za Tanzania hawezi kubaki salama atafungiwa yy na kituo chake cha kazi kiwe tv ama radio kwaiyo wanaogopa ugali wao kuingia mchanga na serkal ya tz haitaki habari za kweli zifike nje ya nchi hasa kwa mabeberu itaonesha udhaifu wskat wao hawana udhaifu ni miungu watu wa hapa Duniani.
 
Huna haki wala ruhsa ya kuyasema haya kwa umma wa watanzania na dunia nzima kaa kimya wenye mamlaka watatoa taarifa za uongo na sio hizo zako.
 
Kawaida sana mbona ....kwa Tanzania Wana reporter BBC...mi cmjui Ila najua Al Jazeera na cgtn China wanae Daniel kijo...
 
Kweli mkuu hata mimi nasikiliza radio mda sasa lakini sjaskia habari hii maana yake vyombo vyote vya habari vya hapa nchini vimetii amri ya meko jiwe
 
Huna haki wala ruhsa ya kuyasema haya kwa umma wa watanzania na dunia nzima kaa kimya wenye mamlaka watatoa taarifa za uongo na sio hizo zako
Sasa kama wenye mamlaka watatoa taarifa za uongo si ni bora mimi nitoe taarifa za kweli?

Halafu kwanini unasema sina ruhusa wala haki ya kusema hayo ilihali hunifahamu?
 
Fikiria kwa kina Kabendera aliripoti the Economy tuliona kilichompata sasa unazani akina Sami awami,Abdalah famau, Jamuhuri mwavyombo hawapendi uhai wao?

Tatzo ni serikali yetu inaogopwa na watu wake.
 
Sheria inayowataka waandishi wa habari kutangaza habari ambayo serikali haijathibitisha ni ngumu sana kutokaa na mazingira ya sasa.

Radio na online Tv nyingi zimetozwa faini na zingine kufungiwa kutokana na sheria hii, wamiliki wa vyombo wote wamekuwa waoga sana, sasa Mlima Kilimanjaro umewaka moto hakuna mwandishi wa habari anathubutu kusogelea maana hata kama ameshuhudia na kuona bado ataambiwa serikali haijathibitisha taarifa hizo na atapokea kipigo cha faini au kufungiwa.

BBC swahili yupo Mkenya ndiye anaye ripoti sasa huenda kuna waandishi wajanja ndio wako site wanamrushia yeye na kumwambia kila kitu ila majina yao yamefichwa

Je, tuendelee kuishi namna hii kwa kuto habarishana matukio yaliyopo katika eneo husika kisa tunaogopa kupigwa faini?

Eeh Mungu isaidie na uibariki Tanzania
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…