BBC wachakachua uzi wa mwana JamiiForums

BBC wachakachua uzi wa mwana JamiiForums

Hadi miaka ya 1990 muziki uliokua unapigwa zaidi na wanamuziki wa kitamzania ilikua ni
Dansi
Taarabu
Muziki wa asili
Na band zilizokua zinagonga copy

Hadi kufika 1993 vinaja wengi wakaanza kujitokeza kufanya muziki kwa kuiga zaidi mahadhi ya muziki wa kimarekani yaani Rap na rnb pamoja na raggae
Na hii ilichagizwa zaidi na Saleh Jabir alipo tembea na beat za ice ice baby na kuweka maneno ya kiswahili

1994 Radio One ikaanzishwa na ikaanza kupiga kwa wingi nyimbo hizo, na hapo ndipo jina rasmi la BONGO FLEVA likazaliwa ndani ya kipindi maarufu enzi hizo kikiwa chini ya Taji Liundi na Mike Muhagama....... hawa ndio waanzilishi wa Jina BONGO FLEVA wakimaanisha muziki wa kitanzania wenye mahadhi ya kimarekani bila kujali kama ni Hip hop au rnb au raggae as long as uliimbwa na watanzania

Hadi kufikia mwishoni ya 90 wasanii wa hip hop hawakupendezwa na jina la Bongo fleva ila waimbaji waliokua wanafuata mahadhi yaki RNB wao walikubaliana na jina hilo na hapo ndio Dully anapoingia

Wana hip hop waliwaona waimbaji kama mabishoo fulani hivi wakati wenyewe ni wagumu flani hivi....... Dully ubishoo hakuuonea aibu aliubeba na kujisifia sana kwa ubishoo lakini sio kwamba yeye ndio muanzilishi wa Bongo fleva

So Baada ya Bongo fleva na hip hop kuanza kutenganishwa kwa upande wa Bongo fleva(waimbaji)Dully alikua kwenye pick yake na alikua anafanya vizuri sana, na ikumbukwe kwamba waimbaji walikua wachache kuliko wana hip hop

Wapo waimbaji walioanza kabla ya Dully kama Unique Sisters, Mr Paul, Krewz Flava na wengine siwakumbuki
umemaliza
 
miaka ya 1990 hii miziki yoote inayojulikana leo kama bongo fleva haikuwa inaeleweka kabisa kwa jamii. muziki wa dansi ndio ulishika hatamu wakati huo. kumbi zilijaza watu wakienda kutazama bendi maarufu za dansi wakati huo. watu walienda kutazama bendi na sio mwimbaji fulani. waimbaji maarufu walikuwa ni wale waliojihusisha na muziki wa dansi na labda taarabu ndio ilifuatia kwa mbali sana. bendi za dansi zilisajili waimbaji wazuri kwa ahadi au donge nono kama tuonavyo timu za mipira zinavyofanya leo hii.

bongo fleva ile ya wakati ule hata mimi nadiriki kusema nilikuwa sielewi vijana wale wakiimba kitu gani. niliona wanaimba makorokocho yasiyo na maana yoyote na hasa kwa lugha walizokuwa wanatumia maana kuna wakati wakichanganya viingereza tena vile vya amerika humo kwenye nyimbo zao. kwa ujumla haukuwa muziki ukivutia kusikiliza hasa ukifananisha na muziki wa dansi au taarabu zilizokuwa na meseji za wazi kabisa hadi msikilizaji unaelewa mwimbaji anaimba kuhusu nini. hawa wa bongo fleva walionekana kuimba vitu vya ajabuajabu wanavyovielewa zaidi wao wenyewe labda na wengine wa itikadi iyo.

mavazi yao nayo ilikuwa shida nyingine iliyofanya huo muziki uonekane kuwa nje ya maadili yetu ya kitz. sasa ukichanganya yote hayo-kuimba vitu visivyoeleweka, mavazi ya waimbaji wake na lugha vikafanya muziki huu kuwa wa makundi fulani fulani tu kwenye jamii. hii redio ya taifa haikuwa ikipiga nyimbo hizo uenda kwa sababu ya hayo niliyoyaeleza. maana hawa ilikuwa lazima wakielewe hicho unachokiimba kwanza ndio wakurekodi au kuchukua wimbo wako. maana hii ni redio ya taifa huwezi kupeleka vitu hata wewe mwenyewe huvielewi.

kipindi icho wote waliojihusisha kwa namna moja ama ingine na miziki hii ya bongo fleva na wao walichukuliwa kama ni wahuni/waliopotea/wasio na maadili/wasio stara.

Ilipoanza redio one ya mzee Mengi (RIP) ndio chat ya kupiga hizi nyimbo ikapanda. wakipiga sana huko na taratibu jamii na hasa vijana waliokuwa wasikilizaji wakuu wa hizi redio za FM wakaanza kuuzoea huo muziki wa bongo fleva na badae kuukubali.

Kwa hisani ya Braza Kede
 
Dar young mob,wagume weusi asilia,mac muga,nigaz 2 public,deplomatz, kwanza unit, mawingu band list nyingine nmesahau hapo dully bado sana

Ova
Dully Syjes hata siku za "Yo Rap Bonanza" ya Kim Mgomelo alikuwa hayupo.

Tumesnzisha hili game. Too Proud anaingia mjini na kukaribishwa na Dar Young Mob tunamuona.
 
Wengi walikuepo
Sasa hivi wako wapi wako wapi
Balozi Bado nipo
Ninapanda kwenye chati kwenye chati
Nashuka Ile Ile
Ile Moja namba nataman

Sijui nani aliimba ila nilikua napenda kusikia hii chorous
Kaimba Balozi
 
Dully Syjes hata siku za "Yo Rap Bonanza" ya Kim Mgomelo alikuwa hayupo.

Tumeqnzisha hili game. Too Proud anaingia mjini na kukaribishwa na Dar Young Mob tunamuona.
Mkuu Kiranga , umenikumbusha mbali!. Mimi ndio nilikuwa MC wa Yo Rap Bonanza ya DJ Kim!. Coincidently leo nikiwa joint fulani hapa Dodoma, nikakutana na mtoto wa DJ Kim anaitwa Kareem.

Sponsor wa Yo Rap Bonanza, alikuwa Alex Massawe mzee wa AM investment.
P
 
Mkuu Kiranga , umenikumbusha mbali!. Mimi ndio nilikuwa MC wa Yo Rap Bonanza ya DJ Kim!. Coincidently leo nikiwa joint fulani hapa Dodoma, nikakutana na mtoto wa DJ Kim anaitwa Kareem.

Sponsor wa Yo Rap Bonanza, alikuwa Alex Massawe mzee wa AM investment.
P
Naam.

Haya majina wanayajua watu fulani waliokuwapo siku fulani hivi Dar.

Ile Yo! Rap Bonanza ndiyo ilikuwa mashindano ya mwanzoni kabisa ya hip hop /rap Tanzania ukiacha yale yaliyokuwa yanafanyika Lang'ata akashinda Fresh XE Eddo Mtui wa Oysterbay kwao pale kona ya Mkwawa na Bongoyo opposote na kwa Jaji Lubuva pale.

Yule dogo mtoto wa Kim kuna siku niligusia stories za baba yake alikuwapo hapa JF alifurahi sana, inaonekana Kim alifariki wakati yeye alikuwa mdogo sana hakupata kumjua baba yake.

Alikuwa natafuta sana stories za watu waliokuwapo siku zile. Kuna documents /videos anazo anaandaa kitu kama kitabu au documentary ya historia ya "Yo! Rap Bonanza".

Kim alikuwa Article Don. Nilikuwa namfuata nyumbani kwake pale City Centre nyuma ya Billicanas, tulikuwa tunapanga naye mikakati ya mashindano, mtu mmoja very cool anajua ku deal na watu wa kika aina vizuri kuliko maelezo.

Maana yale mashindano yalijumuisha watoto wa mjini wote kuanzia wale ma summer boys wa IST kule Masaki na kina Raiders Posse/ Kwanza Unit, mpaka watoto wa Temeke kina GWM na Dar Young Mobb, na kina Ras Pompidou kutoka Chamazi huko, vichwa ngumu wote wa Dar walikuwapo halafu Kim akawatuliza wakae pamoja kwenye competition bila fujo.

Ilikuwa poa sana.
 
Naam.

Haya majina wanayajua watu fulani waliokuwapo siku fulani hivi Dar.
True
Ile Yo! Rap Bonanza ndiyo ilikuwa mashindano ya mwanzoni kabisa ya hip hop /rap Tanzania ukiacha yale yaliyokuwa yanafanyika Lang'ata akashinda Fresh XE Eddo Mtui wa Oysterbay kwao pale kona ya Mkwawa na Bongoyo opposote na kwa Jaji Lubuva pale.
Bongoyo mtaa wa wazee wa Eagle!.
Yule dogo mtoto wa Kim kuna siku niligusia stories za baba yake alikuwapo hapa JF alifurahi sana, inaonekana Kim alifariki wakati yeye alikuwa mdogo sana hakupata kumjua baba yake.

Alikuwa natafuta sana stories za watu waliokuwapo siku zile. Kuna documents /videos anazo anaandaa kitu kama kitabu au documentary ya historia ya "Yo! Rap Bonanza".
Hell do something.
Kim alikuwa Article Don. Nilikuwa namfuata nyumbani kwake pale City Centre nyuma ya Billicanas, tulikuwa tunapanga naye mikakati ya mashindano, mtu mmoja very cool anajua ku deal na watu wa kika aina vizuri kuliko maelezo.
Lile jengo next to nyumbani kwao, ile floor ya chini yote ndio ilikuwa ofisi ya PPR, kodi tuu ya pango NHC ni TZS. 3.5 per month, wakati mshahara wa DC ni 3.M halafu kuna majinga humu yakasema natafuta u DC!.
Maana yale mashindano yalijumuisha watoto wa mjini wote kuanzia wale ma summer boys wa IST kule Masaki na kina Raiders Posse/ Kwanza Unit, mpaka watoto wa Temeke kina GWM na Dar Young Mobb, na kina Ras Pompidou kutoka Chamazi huko, vichwa ngumu wote wa Dar walikuwapo halafu Kim akawatuliza wakae pamoja kwenye competition bila fujo.

Ilikuwa poa sana.
Mimi na Kim tumejuana akiwa DJ pale hotel next to Tanganyika Meat, siu unajua tena ujana, nimetua mahali kumbe mali za DJ Kim, ma DJ wanapendwa tuu lakini hawana chapaa! sawa na sisi watangazaji wa RTD ile enzi za redio moja!.

Kim akanivaa na kuniambia yeye ndie mmiliki na tayari wame bond!. Demu akanyosha maelezo it was over imebaki heshima. Kim akasema hata kama, sipendi kuona unachezewa!. Tukapatanishwa tukaanza kuwa marafiki.

Disco lake naingia bure ila na yeye atakunywa bia zangu. Tuksendelea kuwa marafiki mpaka mwisho.
P
 
Kwani issue ni mwanzilishi wa neno Bongo fleva au mwanzilishi wa muziki wa Bongo Fleva?.
Nikiwa RTD mwaka 1992 nimepiga wimbo wa ICE ICE Baby na OPP wa Saleh Jabir, wakaja kina Ramsey na kikundi Cha Kwanza Unit, cha kina Adili Kumbuka, hata Balozi Dola Soul, 2Proud, na Soggy Doggy walianza zamani, Radio One imeanzishwa 1994!.
P
Naam shekhe

Kwenye hili uko sawa kabisa
 
Naam.

Haya majina wanayajua watu fulani waliokuwapo siku fulani hivi Dar.

Ile Yo! Rap Bonanza ndiyo ilikuwa mashindano ya mwanzoni kabisa ya hip hop /rap Tanzania ukiacha yale yaliyokuwa yanafanyika Lang'ata akashinda Fresh XE Eddo Mtui wa Oysterbay kwao pale kona ya Mkwawa na Bongoyo opposote na kwa Jaji Lubuva pale.

Yule dogo mtoto wa Kim kuna siku niligusia stories za baba yake alikuwapo hapa JF alifurahi sana, inaonekana Kim alifariki wakati yeye alikuwa mdogo sana hakupata kumjua baba yake.

Alikuwa natafuta sana stories za watu waliokuwapo siku zile. Kuna documents /videos anazo anaandaa kitu kama kitabu au documentary ya historia ya "Yo! Rap Bonanza".

Kim alikuwa Article Don. Nilikuwa namfuata nyumbani kwake pale City Centre nyuma ya Billicanas, tulikuwa tunapanga naye mikakati ya mashindano, mtu mmoja very cool anajua ku deal na watu wa kika aina vizuri kuliko maelezo.

Maana yale mashindano yalijumuisha watoto wa mjini wote kuanzia wale ma summer boys wa IST kule Masaki na kina Raiders Posse/ Kwanza Unit, mpaka watoto wa Temeke kina GWM na Dar Young Mobb, na kina Ras Pompidou kutoka Chamazi huko, vichwa ngumu wote wa Dar walikuwapo halafu Kim akawatuliza wakae pamoja kwenye competition bila fujo.

Ilikuwa poa sana.
Pasco Kamuacha y thang on purpsose because yumo humu
 
Pasco Kamuacha y thang on purpsose because yumo humu
Y-Thang Mnyamwezi wangu akianza kulitema ng'eng'e unaweza kufikiri huyu ni mtoto wa Colin Powell kashuka sasa hivi kutoka Bronx au Brooklyn hata joto la Dar hajalizoea tumtafutie sehemu yenye AC.

Y-Thang alikioatia kiingerwza cha Wamarekani mpaka ikawa vigumu kumtofautisha nao.

Alikuwa A level mimi nipo O level Tambaza, basi kila mara akipenda kuniongelesha mambo ya unyamwezini, mambo ya ndoto zake za kuwa daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake, akinionesha vitabu alivyokuwa anasoma. Kuna siku alikuwa anasoma kitabu kinaitwa "Gifted Hands" cha huyu top surgeon mweusi aliyekuwa Hopkins, Dr. Ben Carson.

Y-Thang akawa ananielezea huyu ni daktari bingwa anaheshimiwa sana Marekani, ila kazaliwa ghetto tu huko Baltimore Maryland USA, kasoma mpaka kawa bingwa kabisa. Ndiyo nikamjua Ben Carson hapo early 1990s Y-Thang yupo PCB Tambaza.

Siku hizi vijana wanajiongeza hivyo kusoma nje ya mitaala?
 
Y-Thang Mnyamwezi wangu akianza kulitema ng'eng'e unaweza kufikiri huyu ni mtoto wa Colin Powell kashuka sasa hivi kutoka Bronx au Brooklyn hata joto la Dar hajalizoea tumtafutie sehemu yenye AC.

Y-Thang alikioatia kiingerwza cha Wamarekani mpaka ikawa vigumu kumtofautisha nao.

Alikuwa A level mimi nipo O level Tambaza, basi kila mara akipenda kuniongelesha mambo ya unyamwezini, mambo ya ndoto zake za kuwa daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake, akinionesha vitabu alivyokuwa anasoma. Kuna siku alikuwa anasoma kitabu kinaitwa "Gifted Hands" cha huyu top surgeon mweusi aliyekuwa Hopkins, Dr. Ben Carson.

Y-Thang akawa ananielezea huyu ni daktari bingwa anaheshimiwa sana Marekani, ila kazaliwa ghetto tu huko Baltimore Maryland USA, kasoma mpaka kawa bingwa kabisa. Ndiyo nikamjua Ben Carson hapo early 1990s Y-Thang yupo PCB Tambaza.

Siku hizi vijana wanajiongeza hivyo kusoma nje ya mitaala?
Out of content

braza Kiranga ww ulisomea combi gani hapo tambaza na chuo ulisomea wapi,course gani maana una madini siyo ya nchi hii.
 
Out of content

braza Kiranga ww ulisomea combi gani hapo tambaza na chuo ulisomea wapi,course gani maana una madini siyo ya nchi hii.
Hahaa. Mambo ya kawaida tu mkuu, mimi nilikuwa nasoma sana vitabu na magazeti.

Nilikuwa natumia sana maktaba za Tambaza, United States Information Services (USIS Peugeot House), Tanganyika Library, British Council, na hata Buddhist Temple kwenye mambo ya Eastern Philosophies. Tabia hii ya kupenda kujisomea ilianzia nyumbani kwenye maktaba ya nyumbani.

Kwa hivyo haya mambo mengi si ya combi wala shule, ni mambo ya kujiongeza wenyewe kama kwenye hiyo story mchizi wangu Y-Thang alikuwa ananiambia habari za kitabu cha "Gifted Hands", hicho kitabu ni cha maisha ya Ben Carson tu hakikuwa kwenye mitaala wala mitihani ya shule.
 
Mkuu Kiranga , umenikumbusha mbali!. Mimi ndio nilikuwa MC wa Yo Rap Bonanza ya DJ Kim!. Coincidently leo nikiwa joint fulani hapa Dodoma, nikakutana na mtoto wa DJ Kim anaitwa Kareem.

Sponsor wa Yo Rap Bonanza, alikuwa Alex Massawe mzee wa AM investment.
P
To proud au sugu nae katoa mchango mkubwa ktk huu mziki

Marehemu baba yangu alikua na album ya kwanza ya sugu ...
 
Back
Top Bottom