Coach Slamah Hamad
JF-Expert Member
- Nov 12, 2014
- 3,740
- 4,938
Mimi pia nashangaa! Nimejiuliza ina maana wote tumeangalia video hizi hizi ama kuna nyingine?Michango mingi humu siyo ya kilichoongelewa na mdogo mtu bali ni maisha yao wao ya kila siku ndiyo wanayoitumbukiza kwenye wanachoita kuchangia.
Kinachosemwa na huyo dada ni tofauti kabisa na yanayojadiliwa hapa!
1) Walipata upako wakiwa wadogo kutoka kwa mwanamke wasiemjua.
2) Waliaminishwa Mrema ndio Nabii Eliya.
3)Waliingizwa katika Ibada ambayo walikuja kutambua baadae (hivi karibuni) kwamba ni tofauti kabisa na Mungu waliyedhani wao wanamuabudu.
4)Mama yao amepatwa na matatizo mpaka ya Afya ya akili kwa miaka yote hiyo tangu walipoingia maagano na huyo Mwanamke (stranger) aliyewapa “upako” mabinti zake.
5)Walikutana na huyo Mwanamke baada ya kufukuzwa katika makazi yao ya family na ndugu wa baba yao.
Sasa, ambacho mnajadili hapa kati ya hizo keys ni kipi?!
Beatrice kajaribu kufungua Pandora’s box….