Behind the curtain: September 11

Behind the curtain: September 11

The Bold umesamehewaa, Ila usikawie Sana, lisaa limoja linakaribia kukata.
 
NAFARIJIKA SANA KUSOMA MANDIKO YAKO,,UBARIKIWE SANA
BEHIND THE CURTAIN: SEPTEMBER 11

View attachment 471418


Siku ya Jumanne, tare 11 mwezi September mwaka 2001 majira ya saa 2 na dakika 46 asubuhi mpaka saa 4 na dakika 28 asubuhi lilifanyika shambulio kubwa na baya zaidi kuwahi kutokea na kufanywa na adui katika ardhi ya nchi ya Marekani.

Majira ya saa 2 na dakika 46, ndege aina ya Boeing 767-223ER (A.A. Flight 11) iliyosajiliwa kwa namba N334AA, mali ya shirika la American Airlines ambayo iliruka kutoka Boston katika uwanja wa ndege wa Logan International Airport ikitegemewa kutua katika uwanja wa ndege wa Los Angels International Airport ambamo ndani yake kulikuwa na abiria 81 na wafanyakazi 11 ilijibamiza na kulipua jijini New York kwenye jengo la Kaskazini (North Tower) la kituo cha kibiashara cha kimataifa (World Trade Center) jengo ambalo lilikuwa na ghorofa 110.

Dakika chache baadae, ndege nyingine aina ya Boeing 767-222 (U.A Flight 175) iliyosajiliwa kwa namba N6126UA inayomilikiwa na shirika la United Airlines ambayo pia iliruka kutoka Boston katika uwanja wa ndege wa Logan International Airport na ikitegemewa pia ikatue katika uwanja wa ndege wa Los Angeles International Airport ambamo ndani yake ilikuwa na abiria 56 na wafanyakazi 9 ilinibamiza na kujilipua pia jijini New York kwenye jengo la kusini (South Tower) la kituo hicho hicho cha biashara cha kimataifa. Jengo hili pia lilikuwa na ghorofa 110.

Kujibamiza kwa kwa ndege hizi na kulipua majengo haya kulisababisha maghorofa haya kudondoka kabisa (total collapse) na yalisababisasha kudondoka kwa majengo mengine kama vile ghorofa la 7 WTC Tower na maghorofa mengine kumi yaliyomo ndani ya kituo cha cha kimataifa (WTC Complex).

Wakati haya yakitokea jijini New York, ndege nyingine aina ya Boeing 757-223 (A.A. Flight 77) iliyosajiliwa kwa namba N644AA inayomilikiwa na shirika la American Airlines ambayo iliruka kutoka katika uwanja wa ndege wa Washington Dulles International Airport ikitegemewa ikatue kwenye uwanja wa Los Angels International Airport ambmo ndani yake ilikuwa na abiria 58 na wafanyakazi iligeuza njia na kurudi nyuma na kwenda kujibamiza na kulipua jengo la Pentagon, ambalo ndio Makao Makuu ya Wizara ya Ulinzi ya Marekani (US Department of Defense).

Muda huo huo pia, ndege nyingine aina ya Boeing 757-222 (U.A Flight 93) iliyosajiliwa kwa namba N591UA mali ya shirika la United Airlines ambayo iliruka kutoka Newark Intenational Airport ikiwa na abiria 37 na wafanyakazi 7 na ikitegemewa ikatue katika uwanja wa San Fransisco International Airport ilidondoka karibu na eneo la Shanksville, Pennsylvania na inasadikiwa ndege hii ilikuwa njiani kwenda kujibamiza katika Ikulu ya marekani.

Mfululizo wa mashambuluo haya ya siku hii yalikuwa ni tukio baya zaidi katika historia kwa Marekani kushambuliwa na adui katika ardhi yake mwenyewe.

Jumla ya watu 2997 walifariki na watu 6000 wengine walijerehiwa vibaya mno.
Hasara ya kudondoka kwa majengo yote haya na uharibifu wa miundombinu uliotokea thamani yake inafikia shilingi za Kitanzania Trilioni 20.
Lakini tukijumlisha na harasa za mifumo, rasilimali watu, majengo, miundombinu, na kitega uchumi chenyewe cha WTC, hasara hii inafikia jumla ya shilingi za kitanzania Quadrillion 6 (Trilioni elfu sita za kitanzania).



Swali la kujiuliza iliwezekana vipi kutekeleza shambulio kubwa kiasi hiki tena kwa mfululizo kwenye nchi ambayo ndio kioo cha dunia kuhusu masuala ya usalama, ujasusi na intelijensi?? Ni nini hasa kilitokea??



Ili kulielewa kwa uzuri zaidi suala hili, yatupasa tuangalie jinsi mioango ilivyoanza kupangwa kwa umakini na ustadi mkubwa kwa muda wa miaka mitano.
Yaani ndio kusema kwamba, mipango ya utekelezaji wa tukio hiliilianzawaka 1996.!

Lakini pia, kabla hatujaanza kuitazama jinsi mipango na mikakati ya tukio hili ilivyopangwa, ni vyema kuangalia chimbuko la "mbegu" iliyochochea kuwapa hamasa watu hao kutekeleza tukio hili.

MBEGU INAPANDWA: CIA, Operation Cyclone

Mwaka 1978 yalitokea maoinduzi nchini Afghanistan yaliyomuweka madarakani Rais Nur Mohammad Taraki.

Baada ya Rais Nur Taraki kuchukua madaraka alianzisha Urafiki na nchi ya Urusi ya kipindi hicho ambayo ilikuwa imepania kueneza Ukomunisti ulimwenguni.

Hii ilipelekea December 5, mwaka huo 1978 Rais Taraki kusaini makubaliano ya "Urafiki" wa miaka 25 kati ya Urusi na Afghanistan.

Hii ikipelekea Rais Taraki kuanzisha sera Kikomunisti ambazo zilikuwa hazikubaliki katika jamii ya Afghanistan.

Mfano, Taraki akaondoa sheria iliyokuwa inaruhusu wazazi kumchagulia mchumba binti yao pia akaaruhusu wanawake kushiriki siasa.

Pamoja na hili akaanzisha Mapinduzi ya Sera ya ardhi ambayo ilidhibiti kiasi cha ardhi kinachoweza kumilikiwa na familia moja.
Hii ilisababisha zaidi ya hekari milioni 1.6 kupokonywa kutoka kwa familia mbali mbali na kurudishwa serikali.

Pamoja na hilo Rais Taraki akaanzisha kampeni ya kuwafunga gerezani wapinzani wake wa kisiasa nje ya chama chake na hata ndani ya chama chake cha People's Democratic Party of Afghanistan.
Inakadiriwa kwamba zaidi ya wapinzani 27,000 waliuwawa kipindi cha utawala wa Rais Taraki.

Hii ikapelekea Rais Taraki kuchukiwa mno ndani ya Afghanistan na mwishoni akapinduliwa kutoka madarakani na rafiki yake aliyeitwa Hazifizullah Amin.

Baada ya Amin kuingia madarakani ilikurudisha imani ya wananchi akaanza kuondoa sera za ukomunisti akaanza kukata mawasiliano na Urusi.

Kutokana na mahusiano ya Afghanistan na Urusi kuzorota mno hii ikapelekea December 24, 1979 Majeshi ya Urusi yakaivamia Afghanistan na kumuua Rais Amin na kumuweka kibaraka wao aliteitwa Babrak Karmal.

Baada ya Karmal kuwa rais akaanza kurejesha tena sera za Ukomunisti na kujenga tena ukaribu na Urusi.
Hasira za wananchi zikawaka zaidi.

Kwanza walipinga uvamizi wa Urusi, lakini pia walipinga Sera za ukomunisti nchini mwao.

View attachment 471420
Majeshi ya Urusi yakiigia Afghanistan Desembe 24, 1979.

Ndipo hapa vikaanza kuibuka vikundi vya upiganaji vya Mujahedeen kila kona ya nchi.

Vikundi hivi viliungana mwaka 1981 na kuunda umoja uliojulikana kama Islamic Unity of Afghanistan Mujahedeen.
Vikundi hivi vilipambana kila kona ya nchi kupinga uwepo wa majeshi ya Urusi nchini Afghanistan na uwepo wa vibaraka wa Urusi serikalini.

Ikumbukwe kwamba kipindi hiki ndicho kipindi ambacho 'Vita Baridi' kati Urusi na Marekani ilikuwa imepamba moto.

Ndipo hapa ambapo Marekani kwa kushirikiana na nchi nyingine za Kiarabu wakaanzisha mkakati wa kuvisaidia vikundi hivi vya Mujahedeen kupambana na majeshi ya Urusi nchini Afghanistan.

Mkakati huu ulisimamiwa na Shirika la ujasusi la CIA, na mkakati huu ulijulikana rasmi kama OPERATION CYCLONE

Operation Cyclone ilikuwa na malengo makuu mawili;

Moja:- kuwapatia mafunzo waoiganaji wa Mujahedeen.
Mafunzo hawa yalikuwa yanafanyika nchini Pakistan kwa kushirikiana na jeshi la nchi hiyo na Idara yake ya Ujasusi (ISI - Inter Service Intelligence).
Jumla ya wapiganaji wa Mujahedeen 100,000 walipatiwa mafunzo ya kijeshi kuanzia mwaka 1978 mpaka 1992.

Mbili:- kutoa msaada wa kifedha kwa vikundi vya Mujahedeen.
Msaada huu ulikuwa katika mtindo wa fedha taslimu na silaha.
Pia msaada huu ulitolewa katika awamu mbili.
Miaka sita ya kwanza (1981-1987) marekani ilitoa jumla silaha na fedha taslimu zenye thamani ya Dola bilioni 3.2.

Katika awamu ya pili (1987-1993) Marekani waliwapa vikundi vya Mujahedeen jumla ya fedha silaha na fedha tasilimu vyenye thamani ya dola za kimarekani bilioni 4.2

Nchi ya Saudi Arabia nayo ikaweka ahadi ya ya "kumatch a dollar for a dollar" yaani kama marekani akitoa dola moja nao wanatoa moja, wakitoa bilioni nao wanatoa bilioni.

Kwahiyo, Mujahedeen nchini Afghanistan walikuwa na rasilimaki fedha za kutosha, silaha za kutosha na mafunzo adhimu kabisa ya kijeshi. Hivyo vita ilikuwa kali kweli kweli.

View attachment 471421
Wapiganaji wa Mujahedeen nchini Afghanistani, 1981.

Wakati huo huo,

Nchini Suadi Arabia, kulikuwa na familia maarufu ya Bilionea ambaye ndiye alikuwa raia tajiri zaidi asiyekuwa mwanafamilia ya kifalme (wealthiest non-royal citizen)! Bilionea huyu aliitwa Mohammad bin Awad bin Laden na alikuwa ndiye mmiliki wa kampuni ya SAUDI BINLADEN GROUP, kampuni kubwa zaidi ya Ujenzi nchini Saudi Arabia.

Bilionea huyu aliuwa amezaa na mke wake wa kumi Hamida al-Attas, kijana aliyeitwa Usama bin Mohammad bin Awad bin Laden ambaye alizaliwa tarehw 10, March 1957.

Kijana huyu alisomea fani ya Uchumi na utawala wa biashara katika chuo kikuu cha King Abdulaziz University. (Japokuwa zipo taarifa zinazoonyesha kuwa huenda alisomea Uhandisi (civil engeneering)).

Wanafunzi wenzake wanaeleza kuwa alikuwa ni kijana mwenye bidii ya masomo na alikuwa muumini mtiifu wa Kiislamu dhehebu la Sunni.

Inaelezwa kuwa alitumia muda mwingi sana chuoni kujisomea Qur'an na kufanya kazi za kujitolea.
Pia inaelezwa kuwa alianza kuwa shabiki wa Klabu ya mpira ya Arsenal tangu akiwa hapa chuoni.
Pia alipendelea sana kutunga ushahiri na kusoma vitabu vya fasihi.

Kijana huyu alivutiwa na vugu vugu la Wapiganaji wa Mujahedeen lililokuwa linaendelea nchini Afghanistan.

Kijana huyu alishawishika mno na mahubiri ya mwanatheolojia wa kiislamu mwenye asili ya Plaestina aliyeitwa Abdullah Azzam ambaye mpaka sasa ndiye anafahamika kama "Baba Wa Jihad Duniani" (Father of Global Jihad).

Kijana huyu akawasiliana na Azzam, na Azzam akamshawishi na kumsaidia ajiunge na Mujahedin.

Hivyo baada ya kumaliza chuo (wengine wanasema aliondoka miezi michache kabla ya kuhitimu) alielekea moja kwa moja Afghanistan kujiunga na wapiganaji wa Mujahedeen kupinga uwepo wa majeshi ya Urusi kwenye Ardhi ya Afghanistan.

View attachment 471422
Osama bin Laden (aliyezungushiwa duara)na wanafamilia wenzake wa Bilionea Mohammad bin Awad walipotembelea London kwa mapumziko miaka ya 1970s

Akiwa nchini Afghanistan, yeye Osama pamoja na Azzam ambaye sasa alikuwa ndiye "mentor" wake wakaanzisha Muktab al-khidamat (MAK) au kwa jina lingine ilijulikana kama Afghan Services Bureau.

Kazi kuu ya MAK ilikuwa ni kueneza propaganda na kushawishi vijana kutoka nchi za Kiarabu wajiunge na Mujahedeen nchini Afghanistan kupigana na majeshi ya Urusi.
Si hivyo tu, bali pia MAK ilikuwa na jukumu la kukusanya michango kutoka kwa watu mbali mbali duniani waliokuwa wanaunga mkono harakati za Mujahedeen.

Osama akatumia kiasi kikubwa cha utajiri wake aliorithi kutoka kwa baba yake (bilionea Muhammad bin Awad bin Laden alifariki mwaka 1967 kwa ajali ya ndege), akatumia kiasi kikubwa cha fedha kuwalipia nauli, tiketi za ndege na malazi vijana wote waliokuwa wanatoka kila pembe ya dunia kujiunga na Mujahedeen.

Kujitoa kwake huku, pamoja na uwezo wake mkubwa wa kujieleza na ushawishi, kukamjengea heshima kubwa sana kwa wapiganaji wa vikundi vya Mujahedeen.

Vita ikaendelea kati ya Mujahedeen wakiungwa mkono na marekani dhidi ya majeshi ya uvamizi ya Urusi.


Baadae Urusi ikaja kuona kwamba vita hii ilikuwa na gharama kubwa kwao. Kwanza ilikuwa gharama ya kuharibu mahusiano yao ya Kidiplomasia duniani na pia vita iligharimu kiasi kikubwa cha rasilimali fedha na rasilimali watu.

Hivyo basi kiongozi wa Urusi wa kipindi hicho, Mikhail Gorbachev akaamuru majeshi kurejea nyumbani na kikosi cha mwisho cha Urusi kiliondoka Afghanistan tareahe 15, February 1989.


Baada ya majeshi ya Urusi kuondoka, vikundi vya Mujahedeen walibakiwa na wapiganaji wengi na silaha nyingi za kutosha lakini hawakuwa na adui wa kupigana naye.

Hivyo wakaanza "kutengeneza" maadui wapya.
Wakanzisha vugu vugu la kudai kukomeshwa kwa ukandamizaji wa Israel dhidi ya Palestina na kudai "Uhuru" wa eneo la Kashmir.
Pia wakaweka msimamo kuwa hawataki uwepo wa wanajeshi wa nchi za magharibi katika nchi yoyote ya Kiarabu.

Vugu vugu hili ndilo likasababisha kuanza uadui kati yao vikundi vya Mujahedeen na mshirika wao Marekani.

Ndipo hapa ambapo viongozi kadhaa wa vikundi vya Mujahedeen wakafanya kikao cha siri ili kupanga mikakati mipya, mbinu mpya na falsafa mpya ya kumkabili adui yao mpya, Marekani na nchi za magharibi.

Kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana kutoka kwa mlinzi binafsi wa Osama Kikao hiki cha siri kubwa kilifanyika Tarehe 11 August 1988 na kiliudhuriwa na viongozi wakuu wa Mujahedeen akiwemo Ayman al-Zawahiri, Abdullah Azzam na Osama bin Laden.

Kupitia kikao hiki, kikundi kipya kikaundwa na Osama bin Laden akachaguliwa kuwa Amiri Mkuu wa kikundi (General Emir).

Ni siku hii ya kikao hiki cha tarehe 11 August 1988 ndipo ambapo kilizaliwa rasmi kikundi cha kigaidi cha AL QA'IDA, na ni ndipo hapa ambapo kizaza cha matukio ya kutisha kikaanza

Usikose SEHEMU YA PILI ambayo tutaona namna ambavyo Osama Bin Laden alitoa Fa’twa ya kwanza na Fa’twa ya pili (na impact zake).

Pia tutaangalia namna ambavyo mikakati ya tukio la September 11 ilipangwa kuanzia mwaka 1996.

BOFYA HAPA KUSOMA SEHEMU YA PILI


BOFYA HAPA KUSOMA SEHEMU YA TATU

The Bold
 
BEHIND THE CURTAIN: SEPTEMBER 11



SEHEMU YA NNE



Katikati ya mwaka 1999, kijiwe hiki kilipata mgeni adhimu kwenye ulimwengu wa watu wenye misimamo mikali, walitembelewa na Khalid al-Masri.

Kama kawaida akaanzisha mjadala kutaka kujua mtazamo wao kuhusu vugu vugu la Jihad lilikuwa linaendeshwa na Waislamu huko Chechnya kupinga eneo hilo kudhibitiwa na Urusi.

Mjadala ulikuwa mkali, ambapo Atta na wenzake walionyesha ni kiasi gani wanaunga mkono vugu vugu hilo.
Mwishoni mwa mjadala wakamuomba Khalid al-Masri awasaidie kuingia Chechnya ili wakajiunge na mapambano hayo ya Jihad.

Khalid akawapa mawasiliano wawasiliane na mtu aliyepo maeneo ya Duisburg anayeitwa Abu Musab.
Atta na vijana wenzake wakafunga safari kumfuata Abu Musab.

Walikuwa hawajui, kumbe huu ulikuwa ni "mchongo" umepangwa kwa umahiri kabisa.

Wakupofika Duisburg na kwenda kuonana na Abu Musab, wakashikwa na butwaa kukuta kumbe Abu Musab lilikuwa ni jina la bandia, ila uhalisia ni kwamba mtu alikuwa ni Mohammedou Ould Slahi moja ya 'makachero' muhimu zaidi wa Al Qaida kwenye nchi za Ulaya.

Slahi akawaeleza vijana hawa, kwamba kwanza ni vigumu mno kuingia Chechnya kutokana na udhibiti mkali wa Urusi.
Lakini pia wanahitaji mafunzo zaidi kama wanataka kujiunga rasmi na Jihad.

Hivyo basi akawashauri waende Karachi, nchini Pakistan na maelekezo zaidi watayakuta huko.

Baada ya Atta na wenzake kukubali, Slahi akawaeleza kuwa wakifika Pakistan waende mpaka kwenye ofisi za Taliban na wamuulizid mtu anaitwa "Umar al Masri".

Atta na wenzake wakayapokea hayo maelezo na kurejea Hamburg.

November 29, mwaka 1999 Atta na Jarrah wakapanda ndege ya shirika la Turkish Airlines, Flight TK1662 kutoka Hamburg kwenda Istanbul. (Shehi aliondoka na ndege nyingine peke yake na bin al-Shibh aliondoka wiki mbili baadae).

Walipofika Istanbul wakapanda ndege nyingine ya Turkish Airlines, Flight TK1056 kutoka Istanbul kwenda Karachi.

Kama walivyoelekezwa na Slahi, wakaelekea mpaka kwenye ofisi za Taliban na baada ya kukaribishwa wakaomba kuonana na "Umar all Masri"!!
Wao hawakujua, wakidhani ni mtu, lakini hili lilikuwa ji neno la fumbo (code word) ambalo kwenye ulomwengu wa siri wa Taliban lilikuwa na maana kuwa hao walikuwa ni wageni wa "Bwana Mkubwa".

Kwahiyo wakachukukiwa kutoka hapa Karachi, Pakistan na kupelekwa Kandahar, nchini Afghanistan.

Wakiwa huku Kandahar, wakapelekwa katika nyumba ya siri, na pasipo kutegemea na kwa mshangao mkubwa... Wakakutanishwa na "Bwana Mkubwa", Usama bin Laden.

Osama akawaeleza kuwa amekuwa anawafuatilia kwa muda mrefu ya vijana hao kupendekezwa kwake na KSM.
Akawaeleza kuwa anataka wawe wahusika kwenye shambulio la kihistoria ambalo litawashikisha adabu wamarekani na hawatasahau maishani mwao mwote, lakini shambulio hilo linahitaji vijana hao wajitoe uhai wao.!! Akawauliza kama wako tayari??

Vijana hao bila kusita sita, wakamueleza kuwa hiyo itakiwa ni heshima kubwa kwao kutekeleza tukio hilo, na wako tayari kuyatoa maisha yao muhanga.

Inaelezwa kuwa Osama "akawaapisha"!
Vijana wakala kiapo cha utii na uaminifu wao kwa Osama na Al Qaida.

Baada ya hapo vijana hawa wakapelekwa kwa kamanda mkuu wa wapiganaji wa Al Qaida, Bw. Mohammed Atef ambaye aliwapa muhtasari kuhusu tukio linahusu nini. Baada ya hapo kwa karibia miezi miwili wakapewa mafunzo ya ukakamavu wa kijeshi na mbinu za mawasiliano ya kijasusi na mbinu za kishushushu.

Kisha, wakapelekwa tena Pakistan ambako huko walikutana na KSM aliyewapa 'specifics' kuhusu mission yote.

Wakiwa tayari wamewiva kwenye kile wanachotakiwa kukifanya, February 24 mwaka 2000 wakapanda ndege ya Shirika la Turkish Airlines, Flight TK1057 kutoka Karachi mpaka Istanbul na walipofika Istanbul wakapanda ndege nyingine ya shirika la Turkish Airlines, Flight TK1661 kutoka Istanbul kurejea Hamburg.

Walipofika Hamburg wakaripoti kuwa wamepoteza Passports ili kuficha walikokuwa wametoka.

Hawakutaka kupoteza muda, siku chache baadae wakajiunga na kozi za Urubani hapo hapo Ujerumani.


Baada ya Atta, al-shehhi, al-shibh na Jarrah kurudi Ujerumani walikuwa na mabadaliko makubwa.

Wengi wanaweza kudhani kwamba labda wangekuwa sasa na misimamo mikali lakini ilikuwa tofauti.

Walikuwa na mabadiliko makubwa ya haiba zao na mtindo wa maisha.

Mfano; waliacha kwenda msikito wa Al-Quds, wakanyoa ndevu walizokuwa wamefuga, wakaacha kuvaa 'kiarabu', na badala yake wakaanza kuvaa kimagharibi.

Pia mtu kama Atta ambaye alikuwa ni mkimya kupindukia akabadilika na kuwa mtu mcheshi.

Hii haikiwa bahati mbaya, walifanya hivi ili wasiweze kutilowa mashaka yoyote na watu pamoja na vyombo vya usalama.

Pia kama kawaida wakaripoti kuwa pasipoti wamezipoteza hivyo wakatengeneza nyingine.
Al-Shehhi yeye kwa kuwa alikuwa ni raia wa UAE, hivyo akaenda huko na kuomba kabisa Visa ya kwenda amarekani.

Baada ya wote kujifunza kozi za mwanzo kuhusu urushaji ndege (Basics) kila mmoja akawa anashawishi 'supervisor' wake amuandikie 'recommendation' ya kwenda kusoma zaidi kozi hizo za urubani nchini Marekani. Na wote wakifanikiwa kupata recommendations!

Baada ya hapo wakaanza kutuma maombi kwenge vyuo mbali mbali nchini Marekani.
Kwa mfano, Atta inakadiriwa alituma karibia maombi 60 kwenye vituo mbali mbali vya kufundisha urubani nchini Marekani.

Baada ya hapo wakaanza michakato ya kupata viza.

Mohamed Atta aliomba viza yake siku ya tarehe 17, mwezi May mwaka 2000 katika ubalozi wa Marekani, nchini Ujerumani.
Kutokana na kusoma kwake Ujerumani kwa kipindi kirefu, hivyo basi akaaminiwa na hakufanyiwa upembuzi wowote wa kina, na akapewa viza siku iliyofuata ya tarehe 18 May, 2000.
Akipewa Viza ya miaka mitano ya kundi la B-1/B-2 (viza ya utalii/biashara).

Kama nilivyoeleza, al-Shehhi yeye viza yake alienda kuichukulia UAE.

Lakini kwa bahati mbaya (au nzuri) rafiki zao al-Shibh na Essabar walinyimwa Viza.

Sababu kubwa ya Al-Shibh kunyimwa Viza ilikuwa ni kutokana na uraia wake wa Yemen.
Kwa miaka mingi, mpaka sasa hivi, ni ngumu mno kwa raia wa Yemen kupata Viza ya Marekani. Sababu kubwa ni vile ambavyo kwa miaka mingi, asilimia kubwa ya raia wa Yemen wakienda nchini Marekani hubakia humo Marekani kimagendo hata baada ya Viza zao kuisha muda. Hii imepelekea mamlaka za Marekani kuwakataa Wayemen wengi wanaoomba Viza kwenda nchini Marekani.

Al-Shibh hakukata tamaa haraka baada ya kukataliwa kupewa viza. Kuna kipindi alituma mpaka ada ya dola elfu mbili kwenye kituo cha urubani cha Florida kilichomkubalia kwenda kusomea urubani na akatumia kigezo hicho kwenda kuombea viza (kwamba akubaliwa na Chuo cha Marekani na elipa ada tayari), lakini bado akakataliwa Viza.
Muda mwingine alideposit hela nyingi kwenye akaunti yake ili kuonyesha hana "njaa" hivyo hawezi kibaki kimagendo nchini Marekani akikubaliwa kuingia, lakini bado ubalozi ukakataa kumpa viza.

Baadae akakubali matokeo na akaamua kubaki Ujerumani wenzakw wakielekea Marekani na akaamua kujipa jukumu la kuwatumia hela wenzake wakiwa huko na pia kuwa kuinganishi kwa wao walioko Marekani na viongozi wao waliopo Ulaya ma Uarabuni.

SEHEMU YA TANO INAENDELEA POST INAYOFUATA..
 
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] bora nianze kucheka mwenyewe mzee mzima umerudi karibu kiti, dharura, kusahau ni katika maumbile ya mwana damu, tumekusamehe ila leo iongeze urefu kidogo kaka
Ha haaa kama nakuona vile
 
BEHIND THE CURTAIN: SEPTEMBER 11


SEHEMU YA TANO



June 2, 2000 Atta alipanda basi kutoka Ujerumani mpaka Nchini Czech Republic katika jiji la Prague. Kutokea hapo akapanda ndege mpaka nchini Marekani.

Al-Shehhi yeye aliondokea kutokea Dubai ambapo alipitia Brussels na baadae akatua Marekani.

Kumbu kumbu zinaonyesha kuwa al-Shehhi alianza kuwasili na siku chache, mbele Atta naye akawasili, yaani June 3, 2000.
Wote waliwasili kupitia uwanja wa ndege wa Newark Inatenational Airport.

Kwa mwezi mzima walikuwa wanakaa kwenye mahoteli kwenye miji mbali mbali huku wakiendelea kuomba nafasi kwenye vituo mbali mbali vya kufundisha urubani.
Kumbukumbu zinaonyesha kuwa waliwahi kufika hata kituo cha chuo cha Airman Flight School kilichopo Norman, Oklahoma lakini hawakupapenda na wakaendelea "kutalii" kwenye vyuo vingine.

Hatimaye wakapata sehemu waliyoipenda, Venice, Florida ambapo walipata nafasi katika kituo cha Huffman Aviation.
Kwahiyo wakaweka kabisa makazi na kupanga apartment hapa hapa Venice, Florida.

Wote wawili wakafungua akaunti katika benki ya SubTrust na wakawa wanalokea fedha za kujikimu kutoka kwa mtu anayeitwa Ali Abdul Aziz Ali aliyeko UAE. Mtu huyu alikuja kugundulika baadae kuwa alikuwa ni mpwa wa KSM.

Rafiki yao Ziad Jarrah naye alipata kituo cha kujifunza urubani hapa hapa Venice lakini kilikuwa ni kituo tofauti na kile wanachojifunzia Atta na al-Shehhi.


Atta na al-Shehhi walianza rasmi mafunzo tarehe 6 July, 2000.
Inaelezwa kuwa walikuwa na bidii haswa ya kujifunza. Walitrain kila siku asubuhi mpaka jioni kana kwamba hawana kingine chochote cha kufanya au wameletwa duniani kujifunza kurusha ndege pekee.

Mpaka kufikia mwanzoni mwa mwezi August, walikuwa wanaweza kurusha ndege wenyewe bila msimamizi au abiria (solo flight).

Wakaendelea kujifinza kwa bidii kubwa na hatimaye mwishoni mwa mwezi September, 2000 wakapata leseni za Urubani wa ndege binafsi.

Baada ya hapo mwezi October wakahama kituo cha kujifunzia na kwenda katila kituo cha Jones Aviation kilichopo Sarasota.
Lengo lao la kwenda huku ni ili wapatiwe mafunzo ya kurusha ndege kubwa zenye nguvu zaidi (multi-engines planes).
Lakini wakaanza kupewa 'longolongo' kuwa inabidi waanze na videge vidogo kisha baadae wahamoe kwenye midege mikubwa.

Hawakutaka kupoteza muda, mwezi huo huo kati kato wakarudi kwenye kituo chao cha zamani cha kujifunzia cha Huffman Aviation.

Wakaendelea kunifunza kwa bidii zaidi na zaidi na hatimaye mwezi November wakapewa daraja la 'instrument' (instrument rating).

Hawakutaka kubweteka wala kuridhika mapeka, 'wakakaza" zaidi na kuongea juhudi kubwa, na hatimaye mwezi December, 2000 wote wawili wakakabidhiwa Leseni za Urubani wa Ndege za Abiria.

Kwahiyo sasa walikuwa na rihusu kuendesha au kujifunza dege la aina yoyote haijalishi ukibwa wake.

Ndipo hapa kuanzia Desemba 22 hadi 29, wakaenda chuo Eagle International kwa ajili ya mafunzo mafupi ya Kuendesha Madege makubwa.

Kwa kuwa walikuwa wanakimbizana na muda, iliwabidi waanze kujifunza kwa njoo ya 'Mafunzo hisi' (Simulation trainings) ili kuepuka mlolongo wa urasimu wa kupata madege makubwa ya kujifunzia.

Mafunzo haya ya 'simulation' mfano mzuri kuyaelezea unakuwa kwenye chumba maalumu na chenye vifaa maakumu na ukakuwa kama vile "unacheza game" lakini tofauti na "game" za kawaida, hii yenyewe inakuwa ina uhalisia kabisa. Unakuwa kana kwa 100% kama upo kwenye ndege halisi.

Kwahiyo, kwanza wakaenda Opa-locka Airport ambapo hapa walifanya 'simulation training' ya ndege ya Boeing 727 kwa tarehe 29 na 30 ya mwezi desemba, 2000.

Baada ya hapo wakaenda Pam Am International Airport kwa ajili ya 'simulation training' ya ndege ya Boeing 767, hii walifanya tarehe 31 desemba.

Mpaka kufikia hapa walikuwa na ujuzi wote waliokuwa wanahotaji ili kurusha aina yoyote ya ndege.


WASHIRIKA WENGINE WANAWASILI


Jumla ya washiriki wote walihusika kuteka ndege na kuzilipua kwenye majengo siku ya 9/11 jumla yao walikuwa watu 19.

Tukiacha washiriki wakuu watatu kutoka "Hamburg Cell" ambao nimewaelezea kwa kina (Atta, al-Shehhi na Jarrah).. Washiriki wengi wachache waliwasili mwaka 2000 lakingi waliwasili mwanzano na kati kati ya mwaka 2001.

Washiriki hawa wote ni hawa wafuatao;


Nawaf al-Hamzi (miaka 25)& Khalid Mihdhar (miaka 26)


Hawa wawili walikuwa wanahusudiwa sana na bin Laden. Na aliwachagua yeye binafsi wawemo kwenye mpango huu.

Marafiki hawa wawili walipigana kwenye vita ya Bosnia upande wa Waislamu, na walishiri mapigano mengi huko Afghanistan.

Uraia: Saudi Arabia



Wail al-Shehri (miaka 28) & Waleed al-Shehri (miaka 22)


Hawa walikuwa ndugu. Kaka mtu alikiwa ni mwalimu wa shule ya awali na mdogo mtu alikiwa ni mwanafunzi wa chuo.
Walijiunga na kambi za Al-Qaida nchini Afghanistan mwaka 2000 na kuchagulowa kushiriki makakati huu.

Uraia: Saudi Arabia



Abdulaziz al-Omar (miaka 25)


Hakuna kumbu kumbu nyingi kumuhusi huyu, ila inafahamika tu kwamba alikuwa ni Imam na pia alikuwa mlinzi kwenye uwanja wa ndege.

Uraia: Saudi Arabia.



Satam al-Saquami (miaka 25) & Majed Moqed (miaka 24)


Hawa marafiki wote wawili walikuwa ni wanafunzi wa chuo kikuu cha Saudi Arabia wakisome sheria.
Waliacha chuo mwaka 2000 na kujiunga na kambi za Al-Qaida nchini Afghanistan.

Uraia: Saudi Arabia

Fayez Banihammad (miaka 24)

Huyu alikuwa ni kibarua ambaye alipata viza kwa programu maalumu ya 'Visa Express'.

Uraia: UAE


Hamza al-Ghamdi (miaka 20), Ahmed al-Ghamdi (miaka 22) & Mohammed al-Shehri (miaka 22)


Hawa ndugu wawili na rafiki yao wote walikuwa ni wanafunzi wa chuo kikuu.
Wote waliacha chuo mwaka 2000 na kwenda kujiunga na mapigano ya waislamu huko Chechnya. Baadae wakajiunga na kambi za Al-Qaida nchini Afghanistan.

Uraia: Saudi Arabia


Hani Hanjour (miaka 29)


Huyu Mara ya kwanza alifika Marekani mwaka 1991 na kujiunga na chuo kikuu cha Arizona akisomea Kingereza.
Mwaka mmoja baadae akaondoka na kurejea kwao.
Akarudi tens Marekani mwaka 1996 akiishi maeneo ya California akosomea tena Kiingereza lakino pia Safari hii akaongeza na masomo ya Urubani.
Mwaka 1999 akapata leseni ya Urubani wa ndege za abiria na kurejea Saudi ili kutafuta kazi.
Mwaka 2000 akajiunga na Al-Qaida na ndiko huko Osama akagundua ujuzi wake wa Urubani na kuamua kumtumia.

Uraia: Saudi Arabia

(Huyu ndiye aliyemreplace al-shibh yule mwanachama wa "Hamburg Cell" aliyenyimwa viza!! Mpango wa awali wa Osama ulikuwa ndege zote ziendeshwe na wanachama wa Kijiwe cha Hamburg, kwahiyo baada ya al-shibh kunyimwa viza ndipo ukaja ulazima wa kumtumia huyu)

Salem al-Hamzi (miaka 20)

Huyu naye alienda Marekani kama kibarua kwa program maalumu ya 'Visa Express'.

Uraia: Saudi Arabia


Ahmed al-Haznawi (miaka 20
)

Kuna taarifa chache kumuhusu huyu.
Inajulikana tu mwaka 2000 aliingia Chechnya na kujiunga ma mapigano ya waislamu na baadae akaelekea Afghanistan ambako alijiunga na Al-Qaida.

Uraia: Saudi Arabia

*Ahmed al-Nami (miaka 24)*

Huyu alikuwa ni muazini huko Saudia.
Taarifa zinaonyesha kwamba mwaka 2000 alienda Hijja na aliporejea moja kwa moja akaenda Afghanistan na kujiunga na Al-Qaida.

Uraia: Saudi Arabia


Saeed al-Ghamdi (miaka 21)


Huyu haana undugu wa kifamilia na wale "Ghamdi" nilio waorodhesha mwanzoni japo wote wanatoka kabila moja.

Huyu naye alikuwa ni mwanafunzi wa chuo nchini Saudi Arabia na aliacha chuo mwaka 2000 na kuelekea Chechnya kujiunga na mapigano ya waislamu.
Akiwa huko akashawishowa kwenda Afghanistan ambako alijiunga na kikundi cha Al-Qaida.

Uraia: Saudi Arabia



SEHEMU YA SITA INAENDELEA POST INAYOFUATA..
 
BEHIND THE CURTAIN: SEPTEMBER 11


SEHEMU YA SITA



MAELEKEZO YA MWISHO KUTOKA KWA BIN LADEN



(KONGAMANO LA SPAIN)


Mara kadhaa tangu Mohammed Atta afike nchini Marekani alisafiari mara kwenda Ujerumani na hata Indonesia, yote hii katika kuratibu tukio lilikuwa mbele yao.

Lakini katika safari zote hizi safari ya muhimu zaidi ni ile aliyoifanya July 7, 2001.

Siku hii Atta alipanda ndege ya shirika la SwissAir, Flight 117 kutoka Miami kwenda Zurich, Uswisi.

Alipofika Zuric akapanda ndege nyingine ya SwissAir, Flight 656 kwenda Madrid nchini Hispania.
Aliwasili hispania saa 10:45 jioni na kukaa katika Hoteli inayoitwa Diana Cazadora iliyopo maeneo ya Bajaras karibu kabisa na Uwanja wa ndege.

Usiku wa siku hiyo alimpigia simu mtu anayeitwa Bashar Ahmad Ali Mesleh, mwanafunzi wa Jordan mjini Hamburg.
Huyu ndiye alikuwa mtu wa kati kiunganishi kati yake na Ramzi bin al-Shibh.

Siku mbili mbele, Atta alikodi gari aina ya Hyundai Ascent na kuendesha mpaka mitaa ya beach ya Tarragona kwenye eneo linaloitwa Reus.
Hapo alikuwa anasubiriwa na bin al-Shibh aliyewasili kutoka uwanja wa ndege.

Baada ya hapo wakaelekea kwenye hoteli inayoitwa Monica na wakalala hapo mpaka kesho yake.

Siku iliyofuata hawakujulikana walienda wapi, na ina aminika kuwa walienda kwenye 'safe house' ya Al-Qaida hapo nchini Spain.

Wakiwa huko wakafanya kikao kizito sana.
Ina aminika kwenye kikao hicho alikuwepo Atta, bin al-Shibh, KSM na Said Bahaji.
Kikao hiki ndicho kilichobatizwa jina la "2001 summit" katika ulimwengu wa jamii ya Ujasusi.

Kikaoni hapa ndipo al-Shibh na KSM wakawasilisha kwa Atta maagizo kutoka kwa bin Laden.

Kwamba;

Anataka shambulio lifanyike haraka kwani, anahofia kuwa na "makachero" wengi wa Al-Qaida kwa pamoja ndani ya marekani hii inaweza kuharibu mpango wote na kushitkiwa na vyombo vya ulinzi na usalama.

Pia akataja na target anazozitaka zilipuliwe, na akataja Whitehouse, World Trade Center na Pentagon.
Akazitaja hizi kama "Symbol of America". Ndizo sehemu ambazo zitawafedhehesha, kuwadhalilisha na kuwauma Wamarekani zikishambuliwa.

Akamuagiza kuwa kama ikitokea dharura yoyote kukawa na dalili kuwa ndege haitofikia target yake, basi idondoshwe mahali popote.. Kamwe wasikubali kukamatwa wakiwa hai.

Pia akampa angalizo kuwa asiwaambie wenzake details zote hizo mpaka siku za mwisho kabisa kabla ya tukio.

Atta akapokea maagizo yote haya kwa utii. Pia akatoa dukuduku lake. Mwenzao, Jarrah.


Atta alikuwa na wasiwasi kuwa Jarrah anaweza akabadili mawazo kuhusu ushiriki wake katika tukio hilo.
Akadai kuwa Jarrah amebadilika mno baada ya kufika Marekani. Amekuwa anatumka pombe, na pia amepata girlfriend wa kituruki anayeishi Hamburg ambaye kila siku lazima ampigie simu na mara kwa mara anasafiri nje ya Marekani.
Akatilia mkazo zaidi kwamba hata muda huo anapotoa taarifa hiyo, Jarrah yuko kwao Yemen ameenda "kusalimia" na akiwa anarudi huko lazima atapitia Hamburg kwa girlfriend wake.

Bin al-Shibh akajitolea kuongea na Jarrah akifika Hamburg ili asije kujitoa mwishoni na kuvuruga mpango wote.

Lakini pia KSM akamsisitiza bin al-Shibh kwamba akiongea naye na akihisi Jarrah hana nia tena ya kuendelea na mpango huo, basi amjulishe mapema na nafasi yake ichukuliwe na kijana mwingine aliyeitwa Zacharias Moussaoui.

Wote wakakubaliana na kikao kikaisha.

Bin al-Shib akaondoka Spain kurudi Ujerumani tarehe 16, July 2001.

Atta akakaa Spain siku tatu zaidi.
Akakaa siku mbili katika Hoteli ya Casablanca Playa Hotel.
Kisha akakaa siku mbili nyingine Hotel Residencia Montstant.

Atta akaondoka Spain Tarehe 19, July 2001 kwa ndege ya shirika la Delta Airlines na kurejea Marekani.

Sasa ilibakia hatua moja tu! Yeye na wenzake kutekeleza tukio..



SEHEMU YA SABA ITAENDELEA SIKU YA JUMA TANO..


Stay tuned..




The Bold
 
SEHEMU YA NNE, POST # 572

SEHEMU YA TANO, POST # 575

SEHEMU YA SITA, POST # 577


Nifah Divine... glory to yhwh BansenBurner Alisen Papushikashi Magazine Fire miss chagga SANCTUS ANACLETUS mngony Excel Mussolin5 Jimena Inferiority Complex gwijimimi wambura marwa Hoshea shareef conscious wambeke The Boss Deejay nasmile gkileo Juma chief Mangi flani hivi Ngongo makaveli10 KENZY kadada wa pili Root aretasludovick jonnie_vincy Clkey KAFA.cOm mbewe makedonia Afande Nyati peterchoka Leonard Robert Nchi Kavu STUNTER Chrizo jully Van persie Khalidoun Tetramelyz punje haradari Mazigazi Alybaba babu na mjukuu platozoom jimmyfoxxgongo Nicodemas Tambo Mwikozi Ls man Heaven Sent sifongo Infantry Soldier haa mym 20acres MTS MarkHilary compos Tembo2 Erick the future nancy1983 Bulah binsaad Fazzaly the wolf everhurt Melvine Mgibeon kijana wa leo samsun Coolant Jagood pacesetter apologize payton George Betram kisengeli Kiranga Jiwe Linaloishi Madame B jay john Guasa Amboni Dinazarde Analyse Diva Beyonce snowhite Mmanu Expected Value onechromosome Missy rose Innocenthezron Immortal_MH Ficus sunola Robot la Matope mamaafacebook II JEKI likikima Compact scorpio me G'taxi YNWA adna yuzo ntamaholo Otorong'ong'o naan ngik-kundie kandukamo1 AFRICA101 mwalidebe Kobe Blaki Womani kalendi savius The Great Emanuel r2ga Ntaluke.N. Transcend Msemachochote Mchumiajuone mwampepec MTOTO WA KUKU Fukara proto cute kawombe zinginary MLALUKO JR Vupu barafu BlackPanther Ntuzu Matola impongo ntamaholo Mkoroshokigoli Deadbody KING easy mahoza Msolo kkenzki deborah1 KIDUDU buffalo44 winlicious riziki Allys MUHUNZI Moses2015 nacktary Liuumi dochivele Renzo @barbers hmjamii mbere TATIANA famicho LUCKDUBE mwanadome Straton memphis ghazar Graph Theory Honey Faith Shunie Slave ddcmanesto zinginary pacesetter Nkanaga KOMUGISHA mikatabafeki johnsonmgaya lee empire wigo MJINI CHAI Asprin mtzmweusi Erasto kalinga Chrizo kichakaa man LULU bike FORTALEZA poleni shibumi ZE DONE umande Edger Sr sir joshua sammoo Roram Password Bavaria hambiliki mwanangu Asili100 Evarist Massawe nice1 Jumong S Rogie 1babake nasreen uberito baest dustless Kilemachocho Tumosa mtembea kwa miguu Debbs Joe scorpnose musacha shibumi seeker of knowledge Simuchi Veni Vidi Vici TUJITEGEMEE abuu garcia Hon Nkundwe Festo Festo marion09 mike2k The dream bro kay vandelintz kirikou1 POINT LOAD lusaka city Dirham Rodcones bato MANCNOO multiphill90 GEORGE Dalali mwanamalundi90 MwaFreeca Roram Ta-kibombo troublemaker mambo KOMUGISHA calabocatz Papaa Azonto Msemachochote Mdomo bakuli tizo1 option dikembe iL Buono fakalava ABDUL KAREEM Gobe Justine Marack Goodluck Mchika MR UNINFORMED darcity nkasoukumu nG'aMBu thatonegAl kabanga MPARE KIBOGOYO Edward Sambai Rassa mnonje srinavas last king of uscoch proto cute Kennedy krava Rais2020 kbosho Mzee wa BsN sam2000 fuma 999 Bableee dawa yenu @charmie DON SINYORI mij adden
bwii ONTARIO Kobe The Vein
 
Back
Top Bottom