Bei ya kadi ya mwendokasi (DART) ni kubwa kama ni muhimu sana itolewe bure au huduma iunganishwe kwenye N card

Bei ya kadi ya mwendokasi (DART) ni kubwa kama ni muhimu sana itolewe bure au huduma iunganishwe kwenye N card

Ziro Buyu

Member
Joined
Nov 1, 2016
Posts
39
Reaction score
39
Nipende kuipongeza serikali katika jitihada zake za kuboresha huduma za Usafifi wa Mabasi ya Mwendokasi Dar (DART).

Hivi karibuni DART wamefanya ukarabati wa vituo vya mwendo kasi kwa kuweka mifumo ya ukataji tiketi kwa kutumia Kadi ambapo kadi hiyo ni Kwaajili ya DART Tuu inauzwa Tsh 5000. Tukumbuke kunakadi ya N Card gharama ya kuipata ni 1000 ambayo inatumika maeneo mengi. Sasa kadi ambayo haina matumizi katika maeneo mengi inauzwa Tsh 5000 wakati N Card 1000.

DART walishakuwa na mfumo kama huu wa Kadi, wananchi wakanunua na wakawa nazo halafu mifumo yao ilipogoma wakawaacha wananchi na kadi zao pasina kusema chochote.

Nashauri kwanza, kwanini hiyo huduma ya DART ya isiongezwe kwenye N Card ili hata mifumo yao kifeli tena kuwe hakuna hasara kwa wananchi. Pili, Bei ya kadi ni kubwa ukilinganisha na huduma inayotolewa lakini pia tunajua LATRA ndio hupanga bei za nauli sasa hii bei ya kadi ni kigezo gani kilichotumika kupanga kadi iuzwe bei hiyo. Mwisho Kama ni muhimu DART kuwa na kadi yao basi zitolewe bure iwe kama namna wanavyogharamia tiketi za karatasi.
 

Attachments

  • Screenshot_20240905_075648_NCard.jpg
    Screenshot_20240905_075648_NCard.jpg
    214.8 KB · Views: 9
  • Screenshot_20240905_075753.jpg
    Screenshot_20240905_075753.jpg
    217.5 KB · Views: 9
Huo mfumo wao ni mbovu,nchi za wenzetu kuna kadi za kwenye treni na mabasi kama hayo,unaweza kulipia mwaka mzima au miezi 6 yenye punguzo, unarenew tu mwaka ukiisha huwazi ila hapo katikati ya mwaka unafanya safari zako unavyotaka kwa malipo yale yale ya mwaka mzima,sasa kuna haja gani kuwa na kadi na bei ni zile zile za nauli ya kila rout wakati kwa wenzetu ukilipia mwaka haawaangalia routs unasafiri unavyotaka ukishalipia kadi inakuwa active mda wote bila kuangalia utasafiri mara ngapi hadi umalize mda uliolipia. Kwa mtindo wanaofanya daladala binafsi ni afadhali kuliko huo mfumo wao.
 
mitanzania inapenda dezo sana sasa kadi itolewe bure kwenye mradi wa mabilioni ya hela? aisee sisi bado sana ndiomaana kuna majitu yanawaza hata kutolipa kodi sasa sijui nchi itajiendeshaje. Shame on us
 
mitanzania inapenda dezo sana sasa kadi itolewe bure kwenye mradi wa mabilioni ya hela? aisee sisi bado sana ndiomaana kuna majitu yanawaza hata kutolipa kodi sasa sijui nchi itajiendeshaje. Shame

mitanzania inapenda dezo sana sasa kadi itolewe bure kwenye mradi wa mabilioni ya hela? aisee sisi bado sana ndiomaana kuna majitu yanawaza hata kutolipa kodi sasa sijui nchi itajiendeshaje. Shame on us
Hii ni kadi ya huduma na ndio maana hata tiketi za karatasi wanatoa bure kwa gharama zao kwa sababu ni huduma! Mfano Kadi ya benk inatolewa bure.
 
Waafrika weusi ni viumbe wa ajabu sana hata akijitia amesoma ni bure tu.
Wakikabidhiwa taasisi za umma kuziendesha hakuna kitu watafanikisha zaidi ya wizi tu!
Nasikitika hata mradi wa SGR utaishia kwenye hasara tu na hautaleta tija yoyote.
 
Hivi hua mnashindwa nini kutoa maoni bila kusifu na kutukuza...🤔
 
Back
Top Bottom