Bei ya mahindi kwa gunia la debe 6 lafika shilingi 9000

Za jioni wandugu, naomba tushirikiane kuwaonea huruma wakulima mazao yanashuka bei ilhali pembejeo bei iko juu. Mliokaribu na wanasiasa washitueni 2020 sio mbali
Hapo hapi unalaumu sembe kupanda bei
Hiyo ni commerce mambo ya demand vs supply,waambie waunde ushirika waje sokoni na sauti moja
 
Acha utani wewe, kwa iyo nikihamia huko nanunua gunia kumi kwa 170,000/=. Hapo uhakika wa kumuunga Raisi mkono kwa ufyatuaji wa watoto ningeufanya vizuri.
Pole yao wakulima kwa bei hiyo wanakula hasara himilivu.

Tatizo miundombinu, usafirishaji kutoka huko ni shida sana. Niliwahi kwenda pia maeneo ya wilaya ya Tanganyika, bei ya mazao ni nzuri, lakini unalazimika kupitia Uvinza Kigoma then ndo uanze safari ya kurudi mjini
 
Astaghfirulah astaghfirulah[emoji20] [emoji20] [emoji20]
 
Nani alikwambia tunataka kura yako?

Tunalo jeshi la polisi na tume yetu pendwa.
Pambaneni na hali zenu
Za jioni wandugu, naomba tushirikiane kuwaonea huruma wakulima mazao yanashuka bei ilhali pembejeo bei iko juu. Mliokaribu na wanasiasa washitueni 2020 sio mbali
 
Imeshuka Kwa kasi mno. Mwaka juzi gunia ilikuwa 120000 hadi 150000, mwaka Jana ikawa 80000 ila mwaka huu ndo shida zaidi pamoja na hyo bei wanunuzi hakuna
Wakati ukitoka nayo ukayafikisha Sudan tu hapo unakula hela za kutosha lakini huruhusiwi. Yaani bora yakuozee upate hasara wao wachekelee eti mfumuko wa bei umeshuka huku wakulima wanateketea
 
Za jioni wandugu, naomba tushirikiane kuwaonea huruma wakulima mazao yanashuka bei ilhali pembejeo bei iko juu. Mliokaribu na wanasiasa washitueni 2020 sio mbali
Ni Chuo gani ulichohitimu kozi ya Uzamivu ya UONGO mkuu!?
JF sio Instagram!
 
Wewe unaongea kwasababu upo mjini hujui uchungu wanao upitia wakulima. Alafu ndo mnahamasisha eti vijana wasikimbilie mijini, kwa mtindo huu nani atapenda kuwa mkulima. Ndio maana ukulima limekuwa tusi na laana Tanzania, wakati katika nchi zinazojielewa ni utajiri na heshima.

Mkulima hatokuja kufanikiwa kwa mtindo huu, itafikia kipindi watapata akili na mimi naomba wapate hiyo akili waamue kulima mazao ya biashara kwa ajili ya kujikimu tu na haya ya chakula walime ya kwao tu alafu sisi wa mjini tutie akili.

Mkulima hasaidiwi chochote anapambana analima akivuna mnambana katika kuuza jasho lake, kama rahisi na nyinyi si mlime? Yaani sasa hivi mkulima inabidi auze magunia mawili au matatu ndo apate pesa ya kununua kiroba kimoja cha mbolea. Je mshawahi kupiga hesabu gharama za wastani wa kuzalisha gunia moja la mahindi linagharimu shilingi ngapi?

Tunawaonea sana wakulima kwa unafuu wa maisha yetu wakati sisi tunakikimbia kilimo.
 
mwaka huu nililima heka mbili mahindi na maharage mwisho wa siku nikavuna maharage nimeuza yote ila mahindi nimehifadhi kwanza bei ikae vzr sitaki hasala mm
 
Kutishia kuwa 2020 iko karibu hakuna maana yoyote maana hao hata wakiuza mahindi shilingi 0 bado kura watampigia huyo mcc,

sina cha kuwashauri.
 
Mmmh!!!
Huku niliko debe ni 5000.
 
ip

mikoa gani hiyo kwa bei hiyo? kwa kuwa soko linaonekana mahindi mwaka huu sio mengi kama mwaka jana kwa miji kama dodoma bei ya chini inasimamia 6000 debe
Uko sahihi Mkuu, huku Mpwapwa vijijini, wakulima wanauza debe 3500 - 4500
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…