Bei ya vyakula vya mahoteli/migahawa ya njiani kwa wasafiri wa mabasi iangaliwe na mamlaka husika

Bei ya vyakula vya mahoteli/migahawa ya njiani kwa wasafiri wa mabasi iangaliwe na mamlaka husika

Mafinga na kitonga kwakweli bei zimezidi maradufu kulingana na vyakula husika ubora hakuna yani ni tabu tupu
 
Kumbe victims wa hili tuko wengi nishakulaga mishikaki hata sijuagi ni ya nyama gani pale msamvu kma unaenda dom kila mtu anasema lake wengine punda wengine ndege pori yaani kyaaa ila yote kwa yote mungu anawaona sio kwa kunionea kule mtanzania mwenzenu
 
Mie sili chips safarini, nilishawahi kupatwa na masahibu. Nilitoka Moshi kwenda Dar, tulivyofika Mombo tukaingia kula hoteli inaitwa Liverpool, nikala viwepe na mishikaki. Uwiiiiii yaani hata hatujafika mbali, tumbo likaanza kuuma, mharo unataka kuchomoza.

Nikawaza, nikimwambia konda nataka "kuchimba dawa" atasema hilo zoezi ilikuwa lifanyike hotelini tulipokula. Basi bwana akili ikaja ya ziada, nikamwendea konda, nikamdanganya kuwa NIMEANZA KU BLEED GHAFLA hivyo wasimamishe gari nikajisetiri, hahahaha, konda kusikia hivyo akamwambia dreva, gari ikasimama nikaenda kwenye hoteli mshenzi mshenzi, nikahariiiiiiishaaaaaa mpaka basi!
Tumbo linaweza kukufanya ukutane na simba porini,mana likivuruga huchagui wapi ujisaidie mana unakuta mda huo kinyesi kinagonga hodi kyupini
 
Juzi wakati natoka Kigali tulisimama eneo fulani. Basi kama mnavyojua wanaume wa Dar tunapenda Chips zege. Ile najitosa kutoa oda, mhudumu ananiambia chips zege ni tsh 6000.

Nikabaki kutoa macho badala ya kutoa hela.
Sasa si unaona, toka lini zege inauzwa 6000. Tunaomba wale waloshinda kwa kishindo watusaidie shida hii. Si wote wenye uwezo wa kununua chakula kwa gharama hizo.
 
Mafinga na kitonga kwakweli bei zimezidi maradufu kulingana na vyakula husika ubora hakuna yani ni tabu tupu
Tuzidi kupiga kelele ili wahusika washughulike hili tatizo. Inakera sana
 
Yule jamaa wa mabasi yaABC naye kafungua hoteli yake pale Morogoro wali nyama sh 7000 mshikaki 3000 marufuku kubakia kwenye basi abiria wote mnashushwa mnalazimishwa kwenda hotelini.
 
Tatizo siyo hizo migahawa bali tatizo hali ni mbaya mifukoni mwa watanzania wengi maana hizo bei bado zinaonekana za kawaida tu ni sawa na usd 3 lakini kwa mwananchi anayeishi chini ya dola moja kwake ni habari mbaya sana kwake. Hali ikiwa nzuri kimaisha wala hutaweza kufikiri hayo yote.
Maisha ni magumu sana mfano ni miaka minne na miezi kadhaa serikali haijaongeza mishahara kwa wafanyakazi kwa mujibu wa sheria (according to annual increment act) lakini viongozi wa vyama vya siasa wapo wanahangaikia matumbo yao tu, wabunge nao kimya, sasa sijui nani mtetezi wa raia wa kawaida
 
Yule jamaa wa mabasi yaABC naye kafungua hoteli yake pale Morogoro wali nyama sh 7000 mshikaki 3000 marufuku kubakia kwenye basi abiria wote mnashushwa mnalazimishwa kwenda hotelini.
Unaona sasa, haka kasecta kamesahaulika sana. hakuna anayekaangalia kuhusu mlaji, isipokuwa wale watu wa mapato na afya wakishapita basi. mlaji atajijua mwenyewe.
 
Tatizo siyo hizo migahawa bali tatizo hali ni mbaya mifukoni mwa watanzania wengi maana hizo bei bado zinaonekana za kawaida tu ni sawa na usd 3 lakini kwa mwananchi anayeishi chini ya dola moja kwake ni habari mbaya sana kwake. Hali ikiwa nzuri kimaisha wala hutaweza kufikiri hayo yote.
Maisha ni magumu sana mfano ni miaka minne na miezi kadhaa serikali haijaongeza mishahara kwa wafanyakazi kwa mujibu wa sheria (according to annual increment act) lakini viongozi wa vyama vya siasa wapo wanahangaikia matumbo yao tu, wabunge nao kimya, sasa sijui nani mtetezi wa raia wa kawaida
Ni kweli kwasababu watanzania walio wengi ni wakulima na wafugaji ambao kwa vyovyote vile wanaishi chini ya dola moja. na katika secta ya uma kama hali ni mbaya basi hata ule mzunguko wa hela ni shida. ni maombi yetu sasa serikali iliangalie hili suala la hii migahawa ili walaji watendewe haki.
 
Mimi siku hizi nimembuni binu mpyaaa nikifika kwenye hivyo vihoteli kama nina njaa naagiza chai ya rangi na mandazi au chapati. Uwezekano wa vitu hivyo kuwa vimechacha ni mdogo, na ukiwa na 2000 inatosha.
Kwa muda mrefu nimekuwa nikikerwa na hili jambo.

Bei ya chakula cha hizi hoteli/migahawa ya njiani kwa wasafiri haiendani na huduma wanayopewa lakini naona mamlaka husika zimekaa kimya. Na hili naomba lisichanganywe na suala la wakulima kujipangia bei, msafiri sio mkulima ni mtu anayekuwa hana option maana pengine amesafiri masaa kumi na mbili au ishirini bila kuonja kitu na analazimishwa anunue chankula kwa bei ya juu. Au anaenda hospitali kupeleka mgonjwa.

Kiuhalisia sahani ya wali nyama ni 1500 - 2000 lakini kwenye hiyo migahawa wali nyama wanauza 5000 - 6000. Mbaya zaidi vile vidada vihudumu vinanyodo utafikiri vinahudumia hoteli ya nyota tano kumbe mgahawa wa barabarani tena kwa wasafiri (ref: nangurukuru). Ukiviambia dada ongeza kidogo basi ili nishibe kanakukata jicho utafirikiri umetoa mawe kumbe umetoa 6000.

Wanaosafiri wengine ni wagonjwa, watu wa vijijini na wengine hawajiwezi kabisa, unapomlazimisha mtu kuwa tutachimba dawa hoteli fulani na kupata chakula hapo ni ukiukwaji wa haki za wasafiri. Kwanini mamlaka wasimoderate na kucontrol hili suala? ikiwezekana sehemu ya kuchimba dawa ijitegemee na sehemu ya kula ijitegemee ili hao watoa huduma wasiwalipishe watu bei kubwa kisa umechimba dawa kwao.

Madereva na makondacta wao huwa hawalipii hiki chakula kwasababu ni deal kwa mwenye hicho kihoteli. hii ni ajabu sana, ndio maana inapelekea hawa madereva wanawapeleka abiria sehemu ambayo mwisho wa siku watalazimika kulipia hata kama hawataki.

Naomba mamlaka husika waaanze na Nangurukuru, Singida, Shinyanga, Morogoro, Alj jazeera na sehemu zingine ambazo mimi sijafanikiwa kupita huko kwasababu inakera sana na ni ukiukwaji wa haki za wasafiri kabisa kuwalazimisha kupata huduma wasipopenda halafu mbaya zaidi kwa bei ya juuu kuliko uhalisia.

Bei ya choo cha kulipia inajulikana ni 300, Bei ya wali maharage inajulikana 1500-200, bei ya wali kuku inajulikana ni 3000-4000, bei ya kile kitake away inajulikana kuwa ni 300. Iweje tutozwe bei zisizoendana na uhalisia?

Wakuu wa nchi wao husafiri na private mara nyingi kwahiyo hii inweza isiwe na mashiko sana kwao, lakini kiuhalisia vyombo vya dola na mamalaka za miji na halimashauri ambako huduma hizi hutolewa inabidi walichukulie serious.

Wakuu Nawasilisha, naomba ndugu zangu tusaidiane kupinga huu unyanyasaji kwa abiria.

Pia soma
 
Kwa muda mrefu nimekuwa nikikerwa na hili jambo.

Bei ya chakula cha hizi hoteli/migahawa ya njiani kwa wasafiri haiendani na huduma wanayopewa lakini naona mamlaka husika zimekaa kimya. Na hili naomba lisichanganywe na suala la wakulima kujipangia bei, msafiri sio mkulima ni mtu anayekuwa hana option maana pengine amesafiri masaa kumi na mbili au ishirini bila kuonja kitu na analazimishwa anunue chankula kwa bei ya juu. Au anaenda hospitali kupeleka mgonjwa.

Kiuhalisia sahani ya wali nyama ni 1500 - 2000 lakini kwenye hiyo migahawa wali nyama wanauza 5000 - 6000. Mbaya zaidi vile vidada vihudumu vinanyodo utafikiri vinahudumia hoteli ya nyota tano kumbe mgahawa wa barabarani tena kwa wasafiri (ref: nangurukuru). Ukiviambia dada ongeza kidogo basi ili nishibe kanakukata jicho utafirikiri umetoa mawe kumbe umetoa 6000.

Wanaosafiri wengine ni wagonjwa, watu wa vijijini na wengine hawajiwezi kabisa, unapomlazimisha mtu kuwa tutachimba dawa hoteli fulani na kupata chakula hapo ni ukiukwaji wa haki za wasafiri. Kwanini mamlaka wasimoderate na kucontrol hili suala? ikiwezekana sehemu ya kuchimba dawa ijitegemee na sehemu ya kula ijitegemee ili hao watoa huduma wasiwalipishe watu bei kubwa kisa umechimba dawa kwao.

Madereva na makondacta wao huwa hawalipii hiki chakula kwasababu ni deal kwa mwenye hicho kihoteli. hii ni ajabu sana, ndio maana inapelekea hawa madereva wanawapeleka abiria sehemu ambayo mwisho wa siku watalazimika kulipia hata kama hawataki.

Naomba mamlaka husika waaanze na Nangurukuru, Singida, Shinyanga, Morogoro, Alj jazeera na sehemu zingine ambazo mimi sijafanikiwa kupita huko kwasababu inakera sana na ni ukiukwaji wa haki za wasafiri kabisa kuwalazimisha kupata huduma wasipopenda halafu mbaya zaidi kwa bei ya juuu kuliko uhalisia.

Bei ya choo cha kulipia inajulikana ni 300, Bei ya wali maharage inajulikana 1500-200, bei ya wali kuku inajulikana ni 3000-4000, bei ya kile kitake away inajulikana kuwa ni 300. Iweje tutozwe bei zisizoendana na uhalisia?

Wakuu wa nchi wao husafiri na private mara nyingi kwahiyo hii inweza isiwe na mashiko sana kwao, lakini kiuhalisia vyombo vya dola na mamalaka za miji na halimashauri ambako huduma hizi hutolewa inabidi walichukulie serious.

Wakuu Nawasilisha, naomba ndugu zangu tusaidiane kupinga huu unyanyasaji kwa abiria.

Pia soma
Mi nimi
Tuzidi kupiga kelele ili wahusika washughulike hili tatizo. Inakera sana
nimeishia kumwaga chakula maranyingi....
 
Yule jamaa wa mabasi yaABC naye kafungua hoteli yake pale Morogoro wali nyama sh 7000 mshikaki 3000 marufuku kubakia kwenye basi abiria wote mnashushwa mnalazimishwa kwenda hotelini.
Uongo,sijawahi shushwa abc na nasafiri nalo mara kwa mara
 
Hili sidhani kama linahitaji mamlaka kulidhibiti. Kwa kifupi limejengwa na sisi watanzania wenyewe.Kwani mtu unashindwa kujibebea chakula chako? Mama una watoto wadogo, unaandaa chakula kinachobebeka kirahisi unakula na wanao njia nzima.

Mimi najibebea mahindi ya kuchemsha na mayai. Nikifika hizo hoteli nakwenda kuwajazia choo tu, sigusi vyakula vyao. Kwanza si salama wala havina ladha. Chips mafuta kibao ,halafu nyeusi.Wali ladha ya udongo,kha!

Abiria tukiamua wanafunga hizo hoteli ndani ya siku moja tu.
 
Back
Top Bottom