Bei za vyakula yashuka nchini

Bei za vyakula yashuka nchini

Kwa msiojua kipindi hiki ni cha mavuno, msishangilie sana. Huku niliko mchele kilo moja ni 1700 mpaka 1600.

Ikifika mwezi wa 8 hadi wa 12 mje mlete mrejesho kama kilo ya mchele haitakuwa ni sh.4500/=[emoji23][emoji23][emoji23]
Juhud za Rais wetu, nyie misukule wa magufuli simlikuwa mnasema Samia kapandisha bei ya vyakula
 
Ni Arusha pekee mchele wa Kamsamba maarufu wa Mbeya kipindi cha mavuno na kipindi ambacho sio cha mavuno bei ni ile ile...hawashushi bei wao watakubadilishia Mchele tuu sijui wa Magugu au Kahama...mchele sasa hivi huko Mbeya kwa 20Kg ni Tsh 35,000 mpaka 45,000 ule uliokobolewa vizuri zaidi ila mchele ni ule ule ule bei tofauti...
 
Vipi wewe huko ulipo bei zipoje?
Bei bado ziko juu ya miti. Tumejaribu kukata miti zishuke chini. tumeambia tunaharibu mazingira. Tunatakiwa tuote mbawa tuzifuate huko huko juu ya miti.
 
Bei bado ziko juu ya miti. Tumejaribu kukata miti zishuke chini. tumeambia tunaharibu mazingira. Tunatakiwa tuote mbawa tuzifuate huko huko juu ya miti.
😂😂 nyie ndio wale mnaishi kwa dada zenu,
Sikulaumu.
 
Sasa nunueni akiba ya chakula kwa ajili ya familia yako kipindi hichi ambacho mazao yashuke bei , badae hatutaki lawama za kijinga dhidi ya bashe utadhani ndo aliwasaidia kuwazalisha wake zenu.
 
Mimi Mwanza nimenunua mchele kg 2000 nikashangaa, maana Bei ilikua 2900 nikahisi hiyo Bei ya sokoni tu, nimeulizia Jana dukani hapa mtaani Bei hiyohiyo 2000 per kg
 
Kamsamba mwaka huu wamevuna sana mpunga, muelekeze aende kwa Raphael pale bei ni hizo ulizotaja japo atakutana na misamiati kama debe na ndonya
Achana nae,akafie mbele
 
Watu hawatanunua chakula cha kutosha afu wanataka bei zibaki hivohivo zikiwasubiri. Na hivi zimeshuka Hawaongei zikipanda tu wanaanza kelele.
Wakulima wanazalisha chakula cha kutosha kiuzwe na nchi jirani. Subir jirani waje uone.
 
Ndugu zangu leo nimestaajabu pale wife aliponiambia, mchele sasa hivi kg moja inaanzia 2400 kwa kilo hadi 3000.

Tofauti na hapo awali bei ilikuwa inaanzia 2800 hadi 3500 kwa kilo.

Mafuta ya kupikia nayo yameshuka kutoka 4500 kwa lita hadi 3800.

Maharage na mahindi nayo yamashuka kwa kiwango kikubwa.

Vipi ndugu zangu huko mlipo bei zipoje?
Duh hii hatari muulize vzr mkeo
 
Geita mchele Kilo 1800
Maharage kilo 2400
Nyama kilo 7000-8000
 
Nchi hii ina chakula kingi sana sema serikali ni wapumbavu tu! Sasa hivi Wakenya wamezagaa vijijini wanakusanya mahindi kama hawana akili nzuri! Jamaa yangu yuko Hanang' anasema gunia limefika 80k muda si mrefu chakula kitaisha turudi kule kule! Huku kwetu sasa Mchele 1500 kwa kilo, mafuta ya alizeti 3500 kwa lita na mahindi 12k kwa debe!
 
Back
Top Bottom