Benard Membe, hii ni zaidi ya ukachero

Benard Membe, hii ni zaidi ya ukachero

ChangeTZ

Member
Joined
Nov 13, 2018
Posts
52
Reaction score
129
LAZIMA tujue kuwa anguko la CHADEMA mwaka huu ni la kihistoria. Haijawahi kutokea tangu kuanza kwa Mfumo wa Vyama vingi mwaka 1992. Labda kwa wasiofahamu dhambi ya kumkataa Jasusi au Kachero (Membe) kwenye Chama hicho ndio mwanzo wa kujiangusha wenyewe. Membe hakuridhika kukataliwa na CHADEMA akaamua kwenda ACT - Wazalendo ili iwe route ya kuwavuruga wote wawili.

Ubaya ulianzia wapi?
Baada tu ya mazungumzo na Viongozi waandamizi wa CHADEMA na Membe kutokubaliana kwa kuwa Membe alionesha kuwa anakwenda kwenye Chama na CASH za kutosha lakini Viongozi hao waliona ni bora aliyepigwa risasi (Lissu) kwa kuwa wananchi watamuonea huruma.

Alichofanya Membe baada ya kutemwa CHADEMA
Kwa kuwa Membe alikosa njia ya kuingia na kuibomoa CHADEMA aliamua kujiunga na ACT Wazalendo ili kuwapasua vizuri wote wawili kwa pamoja na lengo la kwanza likatimia.

CHADEMA na ACT Wazalendo walijikanyaga wapi?
Siku ambayo Mgombea wa Urais wa CHADEMA Lissu alipoenda kwenye Mkutano Mkuu wa ACT Wazalendo na kuhutubia kama vile ndio mgombea wa ACT Wazalendo pale ndipo alipovuruga atmosphere bila wao kujua. Hapo Membe alikuwa anawasoma tu nyumbu wanavyojikanyaga. Na, baada ya Mgombea wa Urais Zanzibar Maalim Seif na Zitto Kabwe kutangaza kumuunga mkono Lissu kwenye Urais, hapo ndipo Membe akaona mikakati yake inakwenda sawa akaamua kujitokeza na kuwaambia Watanzania kwamba yeye ndiye mgombea halali wa Urais ACT Wazalendo. Hapo tunaona namna alivyowachanganya Mazezeta ya ACT na CHADEMA. Hii inaitwa akili Kubwa.

Na, Maalim Seif akaanza kujikanyaga na yeye kujibu alafu sasa na akili ya uzee akasema kuwa wao walikubaliana wote kwenye Kikao wamuunge mkono Lissu. Haya yote walikuwa wakiyafanya bila kujua lengo la Membe ni kuwachanganya Wanachama wa Vyama vyao. Hili ndio lile bao la dakika 89 alilokuwa akilizungumzia.

Mwisho wa siku Wanachama wakaone isiwe tabu wakajikalia zao majumbani na hawakwenda kupiga kura na matokeo yake ndo haya CHADEMA na ACT wameangukia pua.

Mwisho.
 
Upinzani watajua hawajui.

Baada ya miaka miwili, kachero wetu tunamrudisha CCM kama Lowassa
 
Mi nilimsoma siku nyingi kachero km kule kaenda kuwapiga bao la tiktaka then anarudi kijiweni kutulia,eti karudisha kadi thubutuu,mbobezi bana😅😅😅
Mungu anamuona
 
Membe kaenda kuharibu kabisaa maana wengi hawajapiga kura watu wakaona kama hawa Wapinzani hawaeleweki
 
Watu wameona isiwe tabu, mtu umepigwa risasi na bado hujapona vizuri halafu tena tukuongezee majukumu ya urais, afadhali tukuonee huruma kwa kumpa kura magufuli ili ukatibiwe vizuri
 
Membe anahusikaje na kuibiwa masanduku ya kura za ubunge na kura feki kwenye mabegi majimboni ! Think twice ukweli utabaki ni kuwa hapo kulikua na maigizo hakuna uchaguzi mtu anakwapua sanduku na kukimbia unasema ukachero, useless!Nkt
 
Uzi wa kijinga kutoka kwa mjinga.
Inamaana hujui kwamba huu uchaguzi ni figisu za NEC na ma Wakurugenzi ndio zimeumaliza?
Wajinga nyie tulieni dawa iwaingie, mlidhani hizo multiple accounts zenu humu ndo zingepiga kura? mnajitekenya na kucheka wenyewe si tunawachora tu, the majority tumeamua, ingieni road na huko tuje tuwanyooshe.

Sent from my itel it1556 Plus using JamiiForums mobile app
 
Wajinga nyie tulieni dawa iwaingie, mlidhani hizo multiple accounts zenu humu ndo zingepiga kura? mnajitekenya na kucheka wenyewe si tunawachora tu, the majority tumeamua, ingieni road na huko tuje tuwanyooshe.

Sent from my itel it1556 Plus using JamiiForums mobile app
Mje wewe na nani?
Halafu kama unaiweza ligi njoo dm tupange mimi na wewe tukutane kuoneshana uwezo.
 
LAZIMA tujue kuwa anguko la CHADEMA mwaka huu ni la kihistoria. Haijawahi kutokea tangu kuanza kwa Mfumo wa Vyama vingi mwaka 1992. Labda kwa wasiofahamu dhambi ya kumkataa Jasusi au Kachero (Membe) kwenye Chama hicho ndio mwanzo wa kujiangusha wenyewe. Membe hakuridhika kukataliwa na CHADEMA akaamua kwenda ACT - Wazalendo ili iwe route ya kuwavuruga wote wawili...
Hakuna kitu hapa, ulichoandika zungumzia nguvu tu utaeleweka
 
Huu uongo. Wanachama hasa akina mama walijitokeza kwa wingi sana. Kama huyu hapa chini:

1603979953321.png

Mwisho wa siku Wanachama wakaone isiwe tabu wakajikalia zao majumbani na hawakwenda kupiga kura na matokeo yake ndo haya CHADEMA na ACT wameangukia pua.
 
Back
Top Bottom