Benard Membe: Trump alishindanishwa na wenzake na akashinda kugombea awamu ya pili

Membe alizoea kubebwa mzee kikwete ila yeye binafsi ni mweupe mno

Nakubaliana na wewe 100%.

Membe ni mweupe, alibebwa na Urais wa jamaa yake, na hawezi kukuonyesha alipowahi kuleta impact nchi hii, na ukachero mbobezi wake ni hekaya tu, ndio maana walimnasa kirahisi kwenye maongezi, utetezi wake wa demokrasia ndani ya CCM ameuanza baada ya kutoka kwenye utawala, mfumo ambao ndio ulimjenga na yeye aliujenga, akanufaika nao, akatajirika wakati wa awamu ya ndugu yake. Kama alivyokuwa akisema Musiba, sawa kabisa. Ni kiongozi dhaifu asiye na principles. Na inawezekana kabisa nchi hii ingekuwa ishauzwa kama 2015 angepita Membe (au Lowassa) watu ambao wanashiba ndio wanasema chakula kina mchanga.

Lakini mpeni fomu!

Msidhani sisi wajinga hatumjui Membe. Tunatetea Demokrasi. Kwa nini mnamuogopa?

Mpeni fomu!
 
Nakubaliana na wewe 100%.

Membe ni mweupe, alibebwa na Urais wa jamaa yake,

Msidhani sisi wajinga hatumjui Membe. Tunatetea Demokrasi. Kwa nini mnamuogopa?
Mpeni fomu!
Tuna fomu moja tu na imeshachukuliwa, labda akaprinti ya kwake na kisha airudishe kwa mkewe.
 
Vipi kuhusiana na Kikwete yeye alishindanishwa na nani
 
Achana namambo ya utamaduni angalia katiba inasemaje.kama enzi za jakaya mgombea mwenza hakuwepo unalazimisha na sasa asiwepo.
sasa unanishauri mimi nini?? na kwanini??, we mshauri membe
 
Hii TANZANIA SIO MAREKANI... mbona hajatumia mfano wa China au Urusi ( Demokrasia sio kama chupa ya coca cola ifanane kila nchi) ... Tanzania has its own model of Democracy Zwazwa mkubwa
Model ya CCM ni kuwa wagombea wa urais watashindanishwa na kupigiwa kura, hiyo model unayoisema wewe umeitoa chama gani, kama CHADEMA hawana upuuzi kama huo.
 
Utaratibu wa CCM hautofautiani na huo wa Republican, wagombea urais wanapigiwa kura za maoni, anayeshinda anapeperusha bendera ya chama.
 
Mkamateni mumfungulie mashtaka
 
Aende huko marekani akagombee,kama nchi hatufanyi mambo kwa kopi na pesti.

Mamabo mangapi tunafanya sisi na wao wamarekani hawafanyi,au wamarekani wana mambo mangapi amabayo sisi hatuna.

Kama amevutia ahamie huko

Sent from my TECNO KB7j using JamiiForums mobile app
 
Tuna fomu moja tu na imeshachukuliwa, labda akaprinti ya kwake na kisha airudishe kwa mkewe.
Ndio maana tunashindwa kuvi run hivi vi nchi vyetu vichanga changa.

Huo ni ubabe, matusi, na kushindwa kufuata taratibu tulizojiwekea, i.e. Katiba.

KATIBA ya chama haisemi Rais lazima apewe nafasi ya muhula wa pili.

Walioshikiria dhamana za dola. jifunzeni kuheshimu mikataba ya kijamii tunayowekena, i.e. KATIBA ZETU
 
Na mimi mkuu naomba kukumbushwa, nmefatilia sana ila sioni wagombea wengne walo mchallenge Mzee wa msoga 2010.....

Wajuvi wa mambo nisaidien hii historia.
Hawakugombea kwa sababu ya upumbavu wao wa kutoijua katiba ya CCM.
 
Sasa kumbe mpaka mwelekeo wa mwamko wako?

Mwambie atulie basi kama mwamko wake haujakaa vizuri kichukua form
Acha kudharau dhana ya kutoa maamuzi kutokana na mtu alivyoamka, unaidhalilisha taasisi pendwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…