Benki ya Dunia: Tanzania hatarini kukumbwa na "stress za madeni"

Hawa walalamikaji,ndio watumiaji wakubwa wa hiyo miradi,ndege,barabara,madaraja,meli,vivuko,mahospital,maofisi nk.Badala ya kufuatilia fursa za biashara na uwekezaji,wao ni kulalamika,fursa za biashara na uwekezaji,wanawachia wageni.
 
Manake pato tulilitegemea kupitia watalii lilipotea ndio mana tukaenda kukopa...so bado tuko mule mule kwenye mikopo.

#MaendeleoHayanaChama
Na huko kukosa pato la watalii,kumesababishwa na uviko 19,kwa mujibu wa ripoti ya WB,hiyo iliwekwa humu jf.
 
Changamoto ya nchi zetu za kiafrica... Kodi nying inatumika katika vitu visivyo vya msingi na ela za mikopo ndio za maendeleo...

Tanzania inabid ipunguze mapato kwa viongozi wa serikali.... Unakuta wastaafu wanalipwa zaidi mili 5 hapo bado gari inajazwa mafuta na dereva juu.. Wakati mstaafu huyo bado ana lundo za pesa za nssf..

Vile vile serikali mgawanyo wa majukumu hata ueleweiki kwa viongozi.. Mfano sehemu mmoja unakuta kuna mkuu wa mkoa,mkuu wa wilay,diwan,mbunge,mwenyekiti wa serikali za mitaa.. Hawa wote karibu wanalipwa na?serikali..

Vile vile unakuta viongozi wengi wanasafiri na lundo wa watu.. Wale wote lazima walipwe..

Kingine unakuta kulipana posho au seat allowance,ambapo hlo ni jukumu lake katika kazi..

Bado haya mqmbo ya sherehe zisizo na tija kwa serikal...

Yatupswa kupunguza matumiz kwa serikali yenyewe
 
Sio kweli, naomba ulete kipande Cha sehemu ya bajeti kinachosena ni trillion 10.
Kwenye bajeti hakuna wanaposema kakope kasi fulani. Wewe hapo unamaanisha kwenye bajeti wamesema tukope trillion 10 kwa mwaka, hivyo naomba hiyo sehemu kweye bajeti inayosema hivyo
 
Wakati huo walioko watakuwa wanaitwa wastaafu wasioguswa. Ipo siku atakuja Raisi kichaa na Bunge la vichaa watakaotengua Kinga za viongozi zisizo na tija.
Bila kuondoa ccm hiki unachotamani kitokee itakuwa ndoto
 
Utawala upi wa nyerere uliojitegemea!?....pekua vizuri makabrasha yako,huenda ndiyo nchi iliyokua ikipewa feddha kuliko nchi yoyote afrika
Umezaliwa mwaka 2000 na kulishwa crap mbalimbali za kumchukia Nyerere, ndiyo maana unafikiria kutoka kwenye "makabrasha." Mimi nimekulia ndani ya utawala wa Nyerere na ninaju nchi ilivyoenedshwa wakati wa utawala wake pamoja na siasa zake za ujamaa na kujitegemea; sikusimuliwa au kusoma kwenye makbrasha kama wewe.

Hakuna sehemu alikosema serikali iskubali misaada, bali alisema serikali haiwezi kujiendesha kwa kutegemea misaada na mikopo. Misaada yote aliyopewa Nyerere ilikuwa inakwenda moja kwa moja kule kulikokusudiwa na watoa misaada hiyo, haikuwa sehemu ya bajeti ya serikali. Hakukuwa na bajeti ya Jamal au ya Mtei au ya Msuya iliyokuwa na kipande kinachosema bajeti ya "serikali itakuwa kiasi kadhaa, kiasi kadhaa tutakusanya mapato ya ndani, na kiasi kadhaa tutategemea misaada na mikopo kutoka kwa wahisani." Kama hujui kwa nini Nyerere hakutaka kutegemea serikali misaada soma historia iliyoepelekea kuvunjika kwa uhusiano kati ya Tanzania na Marekani mwaka 1965 na kuvunjika kwa uhusiani kati ya Tanzania na Ujerumani mwaka 1964 baada ya Muungano.
 
Maza anaupiga mwingi, rubbish
 
Dingi umeshuhudia utawala wa ticha? hatari sn na heshima kwako
 
Usiseme sana maana Job atasikia 😂 😂 😂 😂 😂 😂
 
Fundisha hao vijana wanajifanya wajuaji! Misaada yote iliyokuwa inaletwa nchini ilikuwa inasimamiwa moja kwa moja na watoaji, kwa mfano danida walisimamia miradi ya maji Mbeya, Iringa na Ruvuma; Finida walisimamia Mtwara na Lindi; Norad walisimamia Rukwa na Kigoma nk.
 
Kwa maana hiyo Spika Mstaafu alisema sahihi kabisa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…