Benki ya Dunia yachelewesha tena kuipa Tanzania mkopo wa Dola 500M

Benki ya Dunia yachelewesha tena kuipa Tanzania mkopo wa Dola 500M

The Assassin

JF-Expert Member
Joined
Oct 30, 2018
Posts
4,942
Reaction score
20,077
Bank ya Dunia imeahirisha kupiga kura ya kuikopesha Tanzania mkopo wenye masharti nafuu wa Dola za kimarekani milioni 500 sawa na shilingi trillioni 1.3 za kitanzania kwa ajili ya kufadhili elimu.

Kama mnakumbuka Benki ya Dunia ilikuwa ipige kura wiki hii kuamua kama iikopeshe Tanzania au la kutokana na sheria ya kuwanyima watoto wa kike waliopata mimba haki ya kusoma, Serikali ikaahidi kuwa imeandaa njia mbadala wa hao watoto kupata elimu ila sio katika shule za umma, na hata Waziri wa Mambo ya Nje, Prof. Kabudi jana tarehe 27 kwenye kuapisha mabalozi na mawaziri aligusia hilo neno na kuwalaumu baadhi ya wanaharakati na wanasiasa kupotosha nia ya serikali.

Wanaharakati na wanasiasa kadhaa wa Tazania waliaandika barua Benki ya Dunia kuitaka kusitisha mkopo au kuinyima Tanzania mkopo kwakuwa Tanzania ina sera za ubaguzi kwenye elimu kwa watoto wa kike wanaopata ujauzito hivyo haistahili kupewa mkopo.

Benki imeamua kusitisha ama kuahirisha kujadili hilo jambo hadi hapo baadaye. Jana Mheshimiwa Rais alisema Benki ya Dunia watatoa pesa kwa kuwa wanajua msimamo wa Tanzania.

Je, Benki imesikiliza maoni ya wanaharakati na wanasiasa ama ina sababu zake nyingine?

Soma hapa👇.

BARUA YA CSOs:

7E825732-DCC3-469F-B0B9-E4B85746B68C.jpeg

3C0382E0-02DF-4197-B063-4891B71C1970.jpeg

2598C2A8-C570-42A0-AD92-043F69BB6436.jpeg
 
Kama serikali inahitaji sana huu mkopo basi ikubali masharti kuwa watoto wakipata mimba na kuzaa warudi tena kwenye darasa lenye wanafunzi ambao hawajapata mimba na kuzaa kama ambavyo wanaharakati na baadhi ya wanasiasa kama Zitto wanavyotaka!

Yaani, msichana akijisikia kupata mimba anapata na kuzaa halafu baadaye anarudi tena kwenye darasa lake na kuendelea na masomo pamoja na wanafunzi wengine!

Hili suala sio rahisi kama ambavyo baadhi ya washabiki wa wanasiasa wanavyoshangilia ndio maana CHADEMA wameamua kukaa kimya kwa sababu wanajua ugumu wake kijamii na kiimani ya dini!
 
Hili Tatizo sio dogo wala la kisiasa. Kabla hatujawazuia watoto kusoma shule kwa mimba tuangalieni vyanzo vya mimba utotoni. Tumekuwa na jamii ambayo ni wepisi kulaumu watoto bila kulaumu mila za kizamani na zisizo na maendeleo sehemu nyingine.

Kuna jamii wanaruhusu watoto waolewe wakiwa wadogo sasa serikali hiyo hiyo inasema lazima mtoto asome na serikali hiyo hiyo inasema huwezi kusoma na mimba. Hatutaweza kutatua matatizo kama serikali inafumbua macho mila zetu hasa vijijini. Pili hili Tatizo Vilevile ni la nafasi watoto wa masikini tu ndiyo wataahidwa kusoma.

Ni lazima tuweke sheria ngumu lakini mila zingine nazo tusiziache tu. Hebu tuonyesheni wangapi walio jela kwasababu ya mimba za utotoni!
 
Mkuu jadili ideas sio mipasho

Hapa Tanzania hata kabla ya Rais wa sasa JPM mwanafunzi akipata mimba alikuwa hana haki ya kusoma shule za Kawaida na hata sasa hana haki

Haya mambo ya haki yanahitaji elimu kubwa na ustaarabu wa muda mrefu

Ukiruhusu warudi shule hapa Tanzania hata sisi wengine tutaanza kutembea na wanafunzi kwani bado wa moto

Mataifa ya magharibi wao kila kitu mtu anatakiwa aishi atakavyo lakini usivunje katiba

Ukiwa shoga ni wewe, Ukivuta bangi ni wewe, ukitembea uchi ni wewe

Serikali ikikubali Haya mambo wanafunzi watajazwa sana mimba kwani akipata bado shule atarudi
Serikali ikubali watoto wakipata mimba na kuzaa warudi tena kwenye darasa lenye wanafunzi ambao hawajapata mimba na kuzaa kama ambavyo wanaharakati na baadhi ya wanasiasa kama Zitto wanavyotaka!
 
Hapo sioni kama ni sawa, hizo pesa zingefanya mambo makubwa kwa nchi yetu, zitto na wenzako mlaaniwe

Sent using Jamii Forums mobile app
mambo makubwa gani mzee unajuwa kama CCM washakaa madarakani huu ni mwaka wa 60 ni lipi la maana walilofanya Zaidi ya kuzalisha wajinga hivi mtoto anamaliza darasa la saba atafanya nini huyu mitaani kama hakuwa jambazi?
 
Ni bora kuachana na huo mkopo. Huwezi idhinisha umalaya kwa wanafunzi kisa dola milioni mia tano.
Kutunga sheria ya kuidhinisha umalaya kwa wanafunzi kutaharibu mabinti zetu wanaojitunza.
Bye bye WB.. U can keep your money.
 
Serikali ikubali watoto wakipata mimba na kuzaa warudi tena kwenye darasa lenye wanafunzi ambao hawajapata mimba na kuzaa kama ambavyo wanaharakati na baadhi ya wanasiasa kama Zitto wanavyotaka!

Yaani, msichana akijisikia kupata mimba anapata na kuzaa halafu baadaye anarudi tena kwenye darasa lake na kuendelea na masomo pamoja na wanafunzi wengine!
huu upotoshaji ndo unao waponza, nani alikwambia kupata ni kujisikia.

kwa nini wameiweka katika ilani yao kama waliona haifai, wangapi wamepata mimba na kurudi shule na kufanya vzr

sera ya kuwazuia kurudi shule ina athari kwa makapuku kwa kuongeza wajinga (mama anakuwa mjinga na mtoto atafata huko pia)

wale wenye pesa na uelewa kdg wanawarudisha watoto wao shule za kulipia na wanafanya vzr sisi makapuku tunabaki ongeza wajinga na mawazo ya kichawi kama yako haya (mtoto akirudi shule kuna ubaya gani)

ikiwa tangu uhuru tunawafukuza na matokeo yake tusha yaona ni kuongezeka kwa wajinga mtaani na ma single mama tujaribu warudisha shule tuone tofauti.
 
Ulimi unaponza kichwa....zamani mtoto alipokuwa anapata mimba akiwa shuleni tulikuwa hatauhangaiki naye..kwa kuwa haukuwa utamaduni wetu wa mtoto kubeba mimba kisa akaingia darasan basi mtoto huyo alikuwa anajiondoa mwenyewe shuleni bila hata kufukuzwa...na hata ingebainika akiwa shuleni basi alikuwa anaadhibiwa kimya kimya mambo yanaenda.....songombingo lilianzia pale amabapo Rais Magufuli aliutangazia ulimwengu kuwa yeye hasomeshi wajawazito..ulimi umeponza kichwa...leo wanaandamwa wapinzani kweli?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni bora kuachana na huo mkopo.. Huwezi idhinisha umalaya kwa wanafunzi kisa dola milioni mia tano.
Kutunga sheria ya kuidhinisha umalaya kwa wanafunzi kutaharibu mabinti zetu wanaojitunza.
Bye bye WB.. U can keep your money.
hujui hata unacho tetea, binti anajitunza ataharibika vipi? kwamba iyo sheria ndo itamfanya aache jitunza

alafu kupata mimba si umalaya, wapo mabinti zenu wanatumia uzazi wa mpango na wanatoa mimba kila uchwao ila kwa kuwa tu hawajapata mimba mnawaona wamejitunza kumbe malaya wa kutupwa
 
Mtoto akipewa mimba kuwepo na special schools za wazazi ambazo ni private kama walivyofanya juvenile courts. Wasichanganyikane na wenzao ambao ni fresh.

Na kitendo cha mtoto kupata mimba kinafutia validity ya kuitwa mtoto. Ngumu ku exercise haki za mtoto maana keshakuwa mzazi. Apambane na hali yake maana alipovua chupi alijua kabisa kuwa madhara yake atavimba juu.Tusiendekeze ujinga.
 
MsemajiUkweli, Usizungumze kama mtoto, mazingira ya upataji mimba mbona yamezungumzwa sana katika forums mbalimbali? Nani atawatetea hawa watoto kama kila mtu anataka kumtetea Magufuli na tamko lake?

Kabla ya tamko lake mbona CCM ilikuwa na Sera nzuri tuu za kumlinda Huyo mtoto? Au Magufuli ni mkubwa kuliko CCM?
Watoto hawa wengi wao wanabakwa, hawana elimu ya uzazi dhidi ya maumbile yao, umasikini unawaponza na yote hayo ni wajibu wetu wazazi kuwalinda nayo badala kuwaachia ili yatokee na kuwaadhibu maisha yao yote

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom