Benki ya Dunia yaikopesha Tanzania Tsh. Trilioni 1.2 za Miradi ya Maji na Afya

Benki ya Dunia yaikopesha Tanzania Tsh. Trilioni 1.2 za Miradi ya Maji na Afya

Hii nchi ni kama haina mwenyewe make na raia tushageuka kuwa mashabiki wa wapigaji, kwamba mkopo wa WB unaenda kufanya kazi ya usafi wa mazingira vijijini, aisee inachekesha sana kuhuzunisha sana.

Nchi inaliwa sana hii na mbaya zaidi sisi raia tunashangilia ila hii mikopo haitalipwa na Mwigulu wala Samia wala Majaliwa bali ni sisi choka mbaya ndio tutapandishiwa bei ya vitu kulipa hii mikopo.

Haiingii akilini kwamba hizo pesa zipo zitakazoenda vijijini kuboresha usafi wa mazingira.

View attachment 2533055
Naungana na wewe katika hili. Hii mikopo hailengi kwenye uzalishaji wa kutukwamua kiuchumi mbeleni bali kutukwamisha kwa kuwa mzigo mkubwa wa madeni huko mbeleni bila kuwa na uwezo wa kulipa kwa kuwa hailengi kwenye kuongeza uzalishaji bali ulaji (consumption) Mikopo inayolenga kwenye uzalishaji ndiyo itatusaidia mbeleni, mfano inakwenda kwa wawekezaji wa uzalishaji katika kufungua mashamba makubwa ya kilimo, kupanua umwagiliaji, viwanda vya uongezaji wa thamani mazao yetu n.k. Huu mkopo hautaleta tija! World bank, kwa matakwa ya wakubwa, wanajua wanachokifanya! Sisi tunajitambua kujua aina ya mikopo inayotufaa? Afya ya mama na mtoto inatushinda nini? Mazingira vijijini maanake nini, kupanda miti kunahitaji mkopo wa world bank? Nipisheni 🚶🚶
 
Tatizo hujaimgia kiundani ukajua inakuwaje. Iko hv hiyo fedha inaenda kuboresha Mambo matatu.
1. Ushambazaji wa maji vijijini. Kwanini maji? Kwa sababu kama Hamna maji Hamna usafi kwenye taasisi na kaya zetu hususani kwenye ishu ya sanitation
2. Uboreshaji miundombinu ya vyoo kwenye vituo vya kutolea huduma za afya na kwenye Shule za msingi
3. Uboreshaji wa hali ya usafi kwenye taasisi za elimu na afya. Lakini lazima ujue huu mpango hautafaidisha wote kwa kiwango sawa kwenye halmashauri zetu Bali Halmashauri zitakazokuwa na watendaji wenye bidii kutimiza vigezo vya uboreshaji hiyo miundombinu na usambazaji wa maji ndio watakaovuna fedha kwa ajili ya kupanua huduma. Yaan unavuna kwa kadri utakavyo perform. Kwa uchache ndio hvyo
Tunahitaji mkopo wa benki ya dunia kuboresha usafi? ...🚶🚶🚶
 
Under the arrangement, the World Bank will extend $300 million in credit and $4.93 million in grant funding to improve access to water supply and sanitation in Tanzania.

"We expect up to 10 million Tanzanian citizens will gain access to improved water supply and 9 million to improved sanitation facilities. Also, up to 2,500 healthcare facilities and over 1,600 primary schools will be provided with adequate sanitation and hygiene services," Mr Belete said.

Wacha wazungu wafanye biashara ya Vikoba kukopesha walalahoi. Eti 10 milioni tanzanians will have access to clean water. Kama miaka 61 hakuna maji,unadhani hizi ndizo zitasalimika, tena leo ambapo mteule anaonekama legelege katika kukemea WIZI! Mtu mwenyewe Nchemba? Time will tell!
Unajua accessibility ya maji Rural na Town Kwa Sasa au unaropoka tuu?
 
Naungana na wewe katika hili. Hii mikopo hailengi kwenye uzalishaji wa kutukwamua kiuchumi mbeleni bali kutukwamisha kwa kuwa mzigo mkubwa wa madeni huko mbeleni bila kuwa na uwezo wa kulipa kwa kuwa haipendi kwenye kuongeza uzalishaji bali ulaji (consumption) Mikopo inayolenga kwenye uzalishaji ndiyo itatusaidia mbeleni, mfano inakwenda kwa wawekezaji wa uzalishaji katika kufungua mashamba makubwa ya kilimo, kupanua umwagiliaji, viwanda vya uongezaji wa thamani mazao yetu n.k. Huu mkopo hautaleta tija! World bank, kwa matakwa ya wakubwa, wanajua wanachokifanya! Sisi tunajitambua kujua aina ya mikopo inayotufaa? Afya ya mama na mtoto inatushinda nini? Mazingira vijijini maanake nini, kupanda miti kunahitaji mkopo wa world bank? Nipisheni 🚶🚶
Akili Yako wewe inajua uzalishaji ni kwenda shambani tuu..

Bila maji ya uhakika huo uzalishaji hasa wa viwanda utatoka wapi? Utakuwa unasubiria masika?
 
Kukopa siyo tatizo, tatizo ni kule kupokea taarifa za CAG zikibaini upigaji kwenye fedha za mikopo na kuyapuuza mapendekezo yake. Anyway mbuzi wa bwana heri nisisahau CAG kweli nae analipwa kwa fedha hizohizo anazoo-odit asante.
Pesa ya mkopo sio sawa na pesa ya Halmashauri,hii ni mikopo specific kwenye miradi na inafanyiwa monitoring na mkopeshaji imf/wb
 
Mbona mlituambia zile za uviko zimemaliza tatizo la vyoo maeneo yote hayo!!!???

Ila bado kwa Nchi kukopa pesa kwa ajili ya vyoo ni aibu,nadhani wewe utakuwa umeweka maneno yako tu siyo kusudio la serikali kukopa mapesa yote hayo kwa ajili ya vyoo

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
Ukiambiwa na nani na wapi kwamba zimemaliza matatizo? Leta ushahidi
 
Mikopo ni mizuri hasa kama ina masharti nafuu...ila awamu hii wapigaji ni wengi balaa kitakachofika kwa wananchi ni % 50 yaani pasu kwa pasu kudadek!.
73% ya deni la Nchi yetu ni mikopo ya masharti nafuu yaani consessional
 
Hivi hiyo #2 ninyi ccm huwa hamsikii aibu kuitaja?

Yaani dunia ipo 21 century lakini ninyi hela ya kuboresha vyoo tena vya sehemu muhimu kama hospital mnaandika kabisa proposal kwa mzungu mpewe hela ya kwenda kuvikarabati,nitakuwa wa mwisho kuamini kwamba huwa mnaandika kweli dhumuni la matumizi ya hizo hela then muweke sababu hizo.
Hakuna anayeandika proposal za vyoo Bali hivyo vyoo ni sehemu ya component ya mradi.

Kwani wewe choo unakichukuliaje mbona kama unapata shida sana.
 
Hakuna anayeandika proposal za vyoo Bali hivyo vyoo ni sehemu ya component ya mradi.

Kwani wewe choo unakichukuliaje mbona kama unapata shida sana.
Napata shida kwa sababu mimi mwenyewe muhangaikaji mwananchi wa kawaida nimejenga nyumba yenye vyoo viwili ndani na bafu na bado nikajenga choo kingine nje.

Kijijini nako nimejenga the same kama mjini ila sijawahi hata mara moja kukopa ila viongozi wa taifa wanaojipambanua kwamba watatuvusha kwenye lindi la umaskini wanaenda kwa wazungu kukopa hela za kujenga vyoo!!!inakuingia akilini hii?yaani waziri alipoenda kusaini huo mkataba alienda na V8 ambayo ukipiga hesabu ya bei yake kuinunua itajenga vyoo vya kutosha mkoa mmoja.

Hovyo kabisa na ni aibu!
 
Napata shida kwa sababu mimi mwenyewe muhangaikaji mwananchi wa kawaida nimejenga nyumba yenye vyoo viwili ndani na bafu na bado nikajenga choo kingine nje.

Kijijini nako nimejenga the same kama mjini ila sijawahi hata mara moja kukopa ila viongozi wa taifa wanaojipambanua kwamba watatuvusha kwenye lindi la umaskini wanaenda kwa wazungu kukopa hela za kujenga vyoo!!!inakuingia akilini hii?yaani waziri alipoenda kusaini huo mkataba alienda na V8 ambayo ukipiga hesabu ya bei yake kuinunua itajenga vyoo vya kutosha mkoa mmoja.

Hovyo kabisa na ni aibu!
Wewe unahusumia familia serikali inahudumia jamii,hayo ya V8 sijui nini hata wakiacha kununua Changamoto hazitakwisha ,Taja Nchi walikomaliza Changamoto.
 
Akili Yako wewe inajua uzalishaji ni kwenda shambani tuu..

Bila maji ya uhakika huo uzalishaji hasa wa viwanda utatoka wapi? Utakuwa unasubiria masika?
Umechangia jambo hili kwa uwezo wako mzuri! 🚶🚶
 
"Mpango endelevu wa maji na usafi wa mazingira vijijinj utapokea Sh689.51bilioni ambao ni mkopo wa masharti nafuu wa IDA, eneo la mradi wa afya ya mama na mtoto litapokea Sh574.59 bilioni," amesem Dk Nchemba.
Hayo maneno ndiyo yanatumika kutupotezea mwelekeo mwisho wa siku wanatupiga
 
Chonde Chonde Pesa Zisijetoka Kwa Watu Wa Upinde Wa Mvua Ikawa Heka Heka
 
Back
Top Bottom