Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Musiba alisema atachukua maamuzi magumu; naona ameamua kuanza na Membe. Bado Zitto Kabwe na January Makamba.View attachment 2618772
Aliyewahi kuwa waziri wa mambo ya Nje kwenye Serikali ya awamu ya nne, Benard Membe amefariki Dunia. Taarifa za awali zinaeleza Membe alipata changamoto ya Kifua na kupelekwa Hospitali ya Kairuki alfajiri ya leo May 12, 2023 na baadaye kufariki.
Benard Membe alipata kuwa mbunge wa Bunge la Jamhuri ya muungano wa Tanzania kupitia jimbo la Mtama na alihitimisha safari hiyo mwaka 2015 na kujaribu kuwania tiketi ya kuwania nafasi ya Urais kupitia chama cha mapinduzi(CCM), tiketi ambayo alipewa hayati John Magufuli.
Mwaka 2018 aliandikwa na gazeti la Tanzanite akituhumiwa kuweka ajenda ya kutaka Rais Magufuli asipewe nafasi ya kuwania Urais 2020, ambapo alifungua kesi ya madai ya kuchafuliwa na kushinda kesi hiyo, alikazia hukumu iliyomtaka mmiliki wa gazeti la Tanzanite, Cyprian Musiba alipe Tsh. bilioni 9 ndani ya siku 14.
duh kama kweli hata angesamehe angeishi milele?
Changamoto ya upumuaji bado IPO. Mwezi huu wanne ilipamba Moto Sana. Binafsi ilitupitia watu wawili nikiwemo Mimi tarehe 24/4-9 May nikawa Sawa. Nilipambania za hospital na kienyeji Ila ukweli mziki wake si wa kitoto. Kinga ilikuwa inashuka kwa speed ya radi sema nikawa napambana kuhakilisha nakula immune boosting stuff. Ila ya safari hii haikunipiga kama Ile ya August 2021 maana kipigo kile kulikuwa kibaya mno.Aliyewahi kuwa Waziri wa Mambo ya Nje Mhe.Bernard Kamilius Membe, amefariki dunia muda mfupi uliopita katika Hospitali ya Kairuki mkoani Dar es Salaam.
Taarifa za awali zinaeleza kuwa alipata changamoto ya kifua na kupelekwa alfajiri ya leo Hospitalini hapo na baadaye kufariki.
Ndio maana ameanza kutoa adhabu kwa kambi ya kina Nape baada ya kujimilikisha MunguMungu ni wa wote sio wapambe wa Maguu tu.
Kwa hiyo kafariki na kinyongoIla watu walimwambia aachane na Musibu hasa wazee wa Kanisa
Hatuwezi kujua yawezekana nyuma ya pazia wamesameheana. Maana siku za mahakama zilipita bila Mali zake kupigwa mnadaHawezi kupumzika kwa amani maana kafa akiwa na chuki na Musiba isiyo sababu.
Hivi kuna mtu au Mtanzania yoyote ambaye si mtumishi wao aliyewahi kwenda ku-print documents zake au kupiga photocopies tu ktk stationery au kiwanda cha TISS?Nchi ya kuuana tunaelekea kubaya
SlowlyUnataka chama gani kiingie madarakani ? Kama ni hv vya akina Chadema basi utakuwa na shida kubwa kwenye ubongo
Kuna kufa kishujaa tena??Tunashukuru Membe amekufa kishukaa baada ya kumjambisha Musiba et al
Sasa hapa itakuwaje au ndio Musiba kanusrika hivyo? Wanasheria mliomo humu JF tunaomba mtusaidie kudadavua hili sakata la kisheria.Mwaka 2018 aliandikwa na gazeti la Tanzanite akituhumiwa kuweka ajenda ya kutaka Rais Magufuli asipewe nafasi ya kuwania Urais 2020, ambapo alifungua kesi ya madai ya kuchafuliwa na kushinda kesi hiyo, alikazia hukumu iliyomtaka mmiliki wa gazeti la Tanzanite, Cyprian Musiba alipe Tsh. bilioni 9 ndani ya siku 14.
Ilinichapa wiki mbili zilizopita si mchezo. Nilipambania kiume kwa dawa za kizungu na asili nikatoboa japo haikuwa ya kitoto.Changamoto ya upumuaji awamu ya pili imeanza, baadhi ya viongozi waandamizi wachukue tahadhari..
Musiba hahusiki na kifo cha huyu bali ni Mungu ameamua kuonyesha ukuu wake dhidi ya mtu jeuri anaekaidi hadi viongozi wa dini.
Usishangilie kama WAPUMBAVU wafanyavyo.Musiba tupo naye hapa tuna choma buzi [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]