Bernard Membe ataka Msaidizi wake Jerome Luanda aliyetekwa arudishwe bila Mchubuko, vinginevyo watafikishana Mbali, hela za Kampeni zatajwa

Bernard Membe ataka Msaidizi wake Jerome Luanda aliyetekwa arudishwe bila Mchubuko, vinginevyo watafikishana Mbali, hela za Kampeni zatajwa

Kufuatua jamaa aliyejizolea umaarufu na mpaka hatua ya kumpa jina la kachero mbobezi ndg Bernard Membe kutoka hadharani na kuuaminisha umma kuwa mlinzi wake katekwa.

Membe aliibuka na kutia kauli kama si kutaja majina basi angeongea wazi juu ya tukio hilo, kilichofuata mpaka sasa kakimbia na siku imekwisha.

Huyu jamaa inafikia hatua hadhira haimwelewi au ndiyo kuchanganyikiwa huko nq kama si kuchanganyikiwa basi anatafuta usikivu wa watu ila ana ukosa so anaamua kutafuta njia ya kufa na mtu.

Mzee baba nadhani siasa ya majukwaani inakuacha, ungebaki tu kule ili muda wako ukifika ujaribu tena.
 
Ndio ukachero wenyewe huo anao fanya 😂😁😀🤣😃😅😄
 
Mgombea Urais wa Tanzania kupitia ACT Wazalendo Bernard Membe ametoa muda wa mwisho kuanzia leo, kuachiwa kwa msaidizi wake Jerome Luanda ambaye ametekwa na watu wasiojulikana na kusema wasipo muachia, kesho ataweka kila kitu hadharani kuhusiana na tukio hilo.

ITV Tanzania

Ninachojua tu ni kwamba ukiona Mtu yoyote anajifanya ana 'Siri' fulani ila hataki kuitoa na anapiga tu 'Mikwara Mbuzi' jua hana anachokijua kabisa!
Yaan mtakaa msubiri hiyo siri kumbe sio siri utasikia anakwambia eti walitaka kujua nilienda kufanya nini dubai na nimerudi na shilingi ngapi.
 
Atahamisha magoli ....muachane Lisu muanze drama zake .....huyu ni wao wale wale
 
Kupitia ukurasa wake wa Twitter Bernard K. Membe amenena yafuatayo :"Tukio la kutekwa kwa Msaidizi wangu Jerome Luanda jana mara baada ya kutua kwenye kiwanja cha Kimataifa cha JK Nyerere international Airport nitalizungumzia kwa undani Saa 10 kamili leo. Nimewapa wahusika wanaodhani siwajui masaa matatu wamwachie akiwa mzima na salama."

Soma: Msaidizi wa Benard Membe, Allan Kiluvya adaiwa kutekwa na watu ‘wasiojulikana’



MEMBE ATAKA MSAIDIZI WAKE ARUDI BILA MCHUBUKO

Mgombea Urais kwa tiketi ya ACT-Wazalendo, Bernard Membe amesema waliomteka Msaidizi wake, Jerome Luanda na kwenda kumkagua nyumbani kwake wamuachie haraka

Membe amedai kuwa, Jerome alitekwa mara baada ya kutua kwenye Uwanja cha Kimataifa wa Julius Nyerere

Amesema, Septemba 17 ataongea na Waandishi wa Habari ili kuelezea zaidi kuhusu tukio hilo. Aidha, amesema sio vyema kutumia Polisi kama kichaka cha kujificha

#JFLeo #JamiiForums #Uchaguzi2020 #TZ2020
View attachment 1571927

Duu! hiyo ndiyo niguse............
 
Jn kwenye taarifa ya habari ya saa mbili Chanel ya ITV alionekana membe akitangaza kupotelewa na msaidizi wake ambaye ni ndugu yake (Jerome)

Lkn alitoa muda kwa waliomnyakuwa kuwa wamuachie bila masharti na asiwe na kovu hata moja la sivyo kesho ( Leo)ataita press ili akinukishe

Vp wenye habari zake ameshakiwasha? Tujuzane
 
Taharuki mnajiletea wenyewe, nyie endeleeni na shughuli zenu
Mbwa muoga huwa anabweka sana.ooh,niguse ninuke,oooh asiporudi mtaona.Membe,wewe huu ni mwaka wa tatu unabweka tuuu mpaka tukaona humu eti 'twende na Membe 2020' . Kumbe masikini huna lolote hata kuongea hujui na unachosema wala hakieleweki.Sasa kama juzi unaongea mambo ya kutiwa vimrija puani huko Dubai eti vinaumiza.Mbona haindeni kabisa na tunayotegemea toka kwako ? huko si umeenda kwa hiari yako ? yaani Membe huna mvuto, huna sera ,huna lolote na tabia yako ya uongo na ulaghai uiache.SIKUPENDI MEMBE.
 
Back
Top Bottom