Uchaguzi 2020 Bernard Membe: Nina dhamira ya kuwania urais wa Tanzania

Uchaguzi 2020 Bernard Membe: Nina dhamira ya kuwania urais wa Tanzania

A failing failure! He just talks about past tenses.
Sijui kwa nini hakumbuki hata mambo waliyoyafanya baada ya awamu ya 4 kuingia madarakani. Anasifia kuachiana vijiti wakati waliingia wakijiita wana mtandao na kumuweka Mkapa mafichoni. Naona pia anapenda kupokea sifa za mitandaoni. Akiitwa mbobezi, anaamini kweli ni mbobezi. Ilikuwa ni janga wa mawazo haya kuyaruhusu kuongoza nchi. Nahisi kuna lengo tofauti nje ya siasa kiasi kwamba ananata presha.
Amechanganyikiwa Membe jamani.Hayupo normal.Anahitaji msaada wa kisaikologia huyu !
 
Sio kweli Tanzania kuna demokrasia

Tanzania chini ya awamu ya tano hakuna demokrasia hilo halina mjadala, lakini Membe ni tapeli kama matapeli wengine wa kisiasa mfano Lowassa, Sumaye nk.
 
Maembe ni mfano halisi ya watu ving'ang'anizi wa madaraka wanaotajwa na JPM (kwao uongozi ni swala la kufa na kupona) - lazima wapate, wasipopata wanahujumu

Kwa taarifa yako hakuna mtu king'ang'anizi wa madaraka kama magu. Mtu yuko kwenye nafasi ya madaraka, lakini hana sifa ya kushinda kwa box la kura zaidi ya figisu, mtu huyo anapata wapi moral authority ya kuzungumzia watu wenye uchu wa madaraka?
 
Yaani Membe alipofikia kwenye kusema Magufuli hakufanya vyema kwenye corona nimempuuza. Kama hatukufanya vyema mbona amezungukwa na watu huku hajavaa barakoa?
Hapo kachemka sana tu
Raisi Mgufuli aliyoa hadi solution ya watu kufunga na kuomba na kujifukizia na kama taifa tumenusurika .Membe hapo kachemka
 
Lugha anayoongea Membe ya ' utaratibu wa ovyo ushamba na upumbavu' siyo lugha yenye taadhima kwa mtu tunayeambiwa eti ni mwanadiplomasia aliyebobea.Kwa kweli anavyoongea ni mtu aliyekata tamaa kabisa ambapo nadhani huko baadae atahitajika kupata tiba ya kisasikologia. Huu mfumo ndani ya chama cha mapinduzi wakati wa kuchukua fomu katika awamu ya miaka mitano ya mwisho ya urais haujaanzia kwa Magufuli.Membe anaongea kwa hisia na chuki kali sana wakati mfumo huo walikaa nao kwa miaka yote.Kwa hili Membe nia yake ni kuleta fujo tu.Kwa nini asingeenda basi Dodoma awaambie wampe fomu kwa sababu anadai hajafukuzwa kwenye chama? yeye si anajinasibu kwamba ni mtu anayejiamini ? Sidhani ,Membe ni Mwoga tu.Kama ana hao wafuasi wengi si ameshakaribishwa kwa Zitto Kabwe aende akagombee huko ?
Kwa kifupi Membe ,Tanzania yote sasa hivi ipo na Magufuli.Hata huko kusini unaposema ni kwenu watakushangaza.Magufuli siyo namba ya kawaida kwa sasa hapa Tanzania.
Tunasikia eti una nasaba na Rais wa awamu ya nne lakini matarajio yako yaligonga mwamba wakati ule na hakuweza kukusaidia kwa lolote.
Badala ya kuongea maneno ambayo hayana taadhima kwa hadhi yako ,nenda chama kingine ujaribu au muombe Mungu wako CCM wakusamehe halafu ujipange kwa 2025 ,siyo mbali ,hapo utajua kwamba unakubalika au vipi kwa sababu mtachukua fomu zaidi ya watia nia 40.Na kwa tabia hii unayoijenga kwa sasa,ukichukua fomu 2025 ndipo utakapojua kwa nini wimbo wa taifa hauna Video.

😢😢😢😢eti anashauliana na viongozi wenzake, vingozi gani wakati yeye ni mstaafu,
Membe tofauti ma kiapo chake kwa sasa ni kama mlinzi tu.
Na kwa kutojiheshim hata kiapo chake kwa watawala watamuweka pembeni tu maana ameshindwa kukilinda, na sasa haaminiki.
 
Maembe ni mfano halisi ya watu ving'ang'anizi wa madaraka wanaotajwa na JPM (kwao uongozi ni swala la kufa na kupona) - lazima wapate, wasipopata wanahujumu

Kipindi hiki anajihujumu mwenyewe, huku kubwabwaja kutampatia shida na fedheha katika maisha yake.
Amesahau kuwa kuna vijana wengi ambao wanafundishwa spirit ya kuwajibika ili wakaitumikie nchi kuliko wao walivyokuwa wanatafuna nchi.
 
Membe amechanganyikiwa
Kama anajiamini akachukue fomu PONA
 
Kuna kitu kimoja ambacho kinaonekana wazi katika haya mazungumzo ya Bwana Membe iwe unakubaliana au haukubaliani na hoja zake. Ule utaratibu wa kuruhusu mijadala kwenye vyama vyote wakati wa uchaguzi tena hasa kwa nafasi ya Uraisi ulikua ni muhimu sana ili kujua misimamo na uwezo wa kila mgombea.

Nakumbuka Mwl. Nyerere alisema utaratibu wa kumpata mgombea wa Urais kwa CCM ni utaratibu wa "Mzengwe". Tena alipoondoka yeye imekua ni "Mizengwe". Maana yake ni kwamba hakuna uwazi wa kutosha na pengine kuchaguliwa mshika Bendera wa CCM hua ni maamuzi ya watu wachache. Kumbuka kua unapomtangaza mgombea Urais kutoka Chama Cha Mapinduzi asilimia kubwa umemtangaza rais wa Tanzania

Hatari ya mizingwe kwenye kumpata mgombea ni kwamba ipo siku atapitishwa mgombea ambaye hajulikani vyema, asiye na uwezo na atakayekuja kuivuruga nchi

Tabia hii imerithiwa na vyama vingine vyote vya upinzani na pengine katika sura ya kushangaza zaidi. Kwenye vyamaupinzani wanaweza wakakaa watu wachache kwenye chama wakamchagua mtu ambaye pengine wala hana itikadi ya chama husika na labda kajiunga nao muda mfupi tu wakamkaribisha hadi chumbani na kumpa bendera ya chama chao kugombea Urais wa nchi!!!!

Hii maana yake wanasiasa wote wako tayari kutumia kila njia, kila hila, kila kituko ili mradi waingie ikulu kwa sababu wanadhani(pengine ndivyo ilivyo) wakishashika dola wataweza kutumia advantage ya kua na serikali kufanya mambo mengine yote wanayotaka hata ikiwa ni kuvunja katiba au kinyume na sheria. Bado tuna safari ndefu sana kama taifa kuhusiana na kitu kinachoitwa demokrasia ya kweli
 
Kuna kitu kimoja ambacho kinaonekana wazi katika haya mazungumzo ya Bwana Membe iwe unakubaliana au haukubaliani na hoja zake. Ule utaratibu wa kuruhusu mijadala kwenye vyama vyote wakati wa uchaguzi tena hasa kwa nafasi ya Uraisi ulikua ni muhimu sana ili kujua misimamo na uwezo wa kila mgombea.

Nakumbuka Mwl. Nyerere alisema utaratibu wa kumpata mgombea wa Urais kwa CCM ni utaratibu wa "Mzengwe". Tena alipoondoka yeye imekua ni "Mizengwe". Maana yake ni kwamba hakuna uwazi wa kutosha na pengine kuchaguliwa mshika Bendera wa CCM hua ni maamuzi ya watu wachache. Kumbuka kua unapomtangaza mgombea Urais kutoka Chama Cha Mapinduzi asilimia kubwa umemtangaza rais wa Tanzania

Hatari ya mizingwe kwenye kumpata mgombea ni kwamba ipo siku atapitishwa mgombea ambaye hajulikani vyema, asiye na uwezo na atakayekuja kuivuruga nchi

Tabia hii imerithiwa na vyama vingine vyote vya upinzani na pengine katika sura ya kushangaza zaidi. Kwenye vyamaupinzani wanaweza wakakaa watu wachache kwenye chama wakamchagua mtu ambaye pengine wala hana itikadi ya chama husika na labda kajiunga nao muda mfupi tu wakamkaribisha hadi chumbani na kumpa bendera ya chama chao kugombea Urais wa nchi!!!!

Hii maana yake wanasiasa wote wako tayari kutumia kila njia, kila hila, kila kituko ili mradi waingie ikulu kwa sababu wanadhani(pengine ndivyo ilivyo) wakishashika dola wataweza kutumia advantage ya kua na serikali kufanya mambo mengine yote wanayotaka hata ikiwa ni kuvunja katiba au kinyume na sheria. Bado tuna safari ndefu sana kama taifa kuhusiana na kitu kinachoitwa demokrasia ya kweli
Democracy is overrated. Watu tufundishwe nidhamu, respect kwa watu wote, uzalendo na hofu ya Mungu tu.

Namna nyingine yeyote ya kuendesha maisha yawe ya mtu binafsi au taifa bila kuzingatia hayo is doomed to fail. Demokrasia bila uzalendo ndio tunayaona haya ya Membe. Kila kinachofanyika Tanzania anakipima kwa mizania ya WHO, IMF, IFC, Marekani, n.k. kana kwamba hii sio nchi huru yenye uwezo wa kujiamulia mambo yake.

Membe bila shaka angekuwa Kikwete version 2.
 
Back
Top Bottom