Uchaguzi 2020 Bernard Membe tulimjua tangu awali. Hatusumbui, Mabadiliko ni lazima mwaka huu!

Uchaguzi 2020 Bernard Membe tulimjua tangu awali. Hatusumbui, Mabadiliko ni lazima mwaka huu!

Lord denning

JF-Expert Member
Joined
Jun 3, 2015
Posts
15,819
Reaction score
33,255
Amani iwe nanyi wadau!

Kwa wapenda mabadiliko wenzangu napenda kuwasalimu kwa furaha sana. Furaha Hii ni kwa sababu Kuu kuwa ile siku yetu muhimu i karibu sana. Tumebakiza siku Saba watanzania tuandike historia kuu, itakayosomwa na kuheshimiwa na vizazi na vizazi.

Naomba nirudi kwenye mada. Leo Kiongozi wa ACT Wazalendo Maalim Seif Sharif ametoa maneno mazuri na mazito sana akimzungumzia Mgombea wao wa kiti ya Urais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania, Ndugu Bernad Kamilius Membe kuwa kama Chama kimeshaamua kumuunga mkono Tundu Antiphas Lissu hivyo pamoja na yeye kuwa mgombea hivyo aheshimu maamuzi ya Chama.

Baada ya maneno haya ya Maalim Seif, CCM wameamua kuuvalia njuga huu mjadala kujaribu kuleta picha kuwa hili suala linaweza kuharibu kura za upinzani.

Napenda kuwapa pole sana wana CCM kwa hoja zao hizi mfu wanazojaribu kuzileta kwa sababu kamwe haziwezi fanikiwa na hii ni kwa sababu zifuatazo.

1. Wapenda Mabadiliko waliojitoa kweli kufanya mabadiliko mwaka huu walishajua kuwa Membe si mwana mageuzi. Walijua kuwa yeye ni Lumumba project na walikuwa wanasubiri tu muda ufike aoneshe rangi zake halisi. Mungu anatupenda sana Watanzania rangi halisi za Membe zimeshaonekana. Hivyo suala la Membe kukataa kumuunga mkono Lissu kamwe haliwezi kuwastaajabisha Watanzania. Huyu anajulikana na alishaonekana tangu awali.

2. Membe kumuunga mkono au kutomuunga mkono Tundu Antiphas Lissu haiwezi kupunguza vyovyote kura za kimbunga atakazopata Tundu Antiphas Lissu mwaka huu. Watanzania wengi wameshaamua kwenda na Lissu na kuachana na Magufuli na CCM yake baada ya miaka zaidi ya 50 ya mateso chini ya CCM. Anachofanya Membe ni michezo ya kitoto ya Miaka ya 70 ambapo propaganda ndo zilikuwa na nguvu kuliko ukweli.

Napenda kumaliza kwa kusema vyovyote vile kwa kuungwa mkono na Membe au kutoungwa mkono na Membe, Watanzania tumeshaamua mwaka huu kuwa tunaenda na Tundu Antiphas Lissu. Mpakwa mafuta wa Mungu aliyeponywa risasi 16.

Viva Lissu, Viva Chadema.

#LissuforPresident
 
Nauona umuhimu wa kupiga kura kipindi hichi
Hakuna mwaka muhimu wa kupiga kura yako na kulinda kura yako Kama mwaka huu. Hakuna mahali atakapotokea Magufuli mwaka huu. Si kwa wafanyabiashara, si kwa wafanyakazi, si kwa wakulima si kwa vijana.

Kite ameharibu sana ndo mana unaona matamko kila siku kutoka NEC sijui msilinde kura. CCM keshaelekea kibra ni sisi tu wananchi kujitoa kwa moyo wote
 
Hakuna mwaka muhimu wa kupiga kura yako na kulinda kura yako Kama mwaka huu. Hakuna mahali atakapotokea magufuli mwaka huu. Si kwa wafanyabiashara, si kwa wafanyakazi, si kwa wakulima si kwa vijana.

Kite ameharibu sana ndo mana unaona matamko kila siku kutoka NEC sijui msilinde kura. Ccm keshaelekea kibra ni sisi tu wananchi kujitoa kwa moyo wote
Nauona umuhimu wa kupiga kura kipindi hiki, nitapiga kura
 
Jamaa alitumwa tu kuja kukamilisha mission sasa amekuta akili kubwa zinafanya kazi, na nimefurahi kwamba cdm na act wanampuuza kwa kiwango cha lami
Mission yake imefeli vibaya. Inabidi CCM na vibaraka wao wajue tu kuwa mwaka huu wananchi hatutaki utani. We really mean business
 
Ni Heri wachache tuumie na hata tuuwawe mwaka huu ila vizazi na vizazi vijavyo vya Tanzania viishi katika Tanzania bora yenye haki na maendeleo ya kweli ya watu na vitu.
Hata waje na vifaru na wale makomandoo wanaovunjaga tofali pale taifa, kura tutalinda, hatuogopiii
 
Nauonaumuhimu wa kupiga kura kipindi hiki....ntapiga kura
Ni muhimu kuliko sana kupiga kura mwaka huu. Hamasisha kila mtu akapige kura mwaka huu. Ndugu, marafiki na hata majirani. Hatma ya kweli ya Tanzania yetu, sisi na uzao wetu tunaenda kuiamua hapo tarehe 28 Oktoba.
 
  • Thanks
Reactions: Lee
Wote wawili wanataka nafasi moja, na wote wapo kwenye karatasi ya kupigia kura lakini mmoja anaambiwa amuunge mkono mwenzake, je maana ya yeye kuwepo kwenye karatasi iko wapi?
Ili kuihadaa tume na mtungi
 
Back
Top Bottom