Uchaguzi 2020 Bernard Membe tulimjua tangu awali. Hatusumbui, Mabadiliko ni lazima mwaka huu!

Uchaguzi 2020 Bernard Membe tulimjua tangu awali. Hatusumbui, Mabadiliko ni lazima mwaka huu!

Mnabadilika kama kinyonga! Mlikuwa mnamshangilia Usalama sahau nishike ninuke
 
Wote wawili wanataka nafasi moja, na wote wapo kwenye karatasi ya kupigia kura lakini mmoja anaambiwa amuunge mkono mwenzake, je maana ya yeye kuwepo kwenye karatasi iko wapi?
Kwani shida iko wapi? Suala sio nani awe kiongozi, Suala ni mabadiliko ya kweli ya kuikomboa nchi yetu!

Kwani kuna shida gani akisema pamoja na Jina langu kuwepo kwenye karatasi ya kura, anaomba watanzania wampigie kura Tundu Antiphas Lissu
 
Naona ameogopa kuwa wa mwisho,Ni aibu kwenye mashindano yeyote yale ukawa wa mwisho. Alishawahi sema ndoto yake imetimia yaani kugombea Urais ila hili la kuwa wa mwisho ndio anaona fedheha sasa🤣🤣🤣🤣🤣
 
Huyo Membe hata kabla hajafukuzwa CCM nilisema kabisa huyo sio wa kumuamini, na wengi wetu tulisema hata akiondoka CCM asipokelewe Chadema, na hata akipokelewa asipewe nafasi yoyote, kwani somo la Lowassa lilikuwa bado bichi. Na kweli kaondoka CCM kwa maelekezo maalum, akaenda ACT ambapo alikuwa analazimisha muungano ili yeye ndio awe mgombea kwa maslahi ya CCM. Nashukuru Mungu alipotezewa.

ukweli uko hivi, huko ACT mpinzani wa kweli ni Maalim Seif na wapemba wenzake, hata huyo Zitto ni wa kuwa naye makini, maana hicho chama cha ACT ni cha kina hao Membe, J.K. nk. Tahadhari Chadema wawe makini sana na Zitto, maana Membe ndio mwenye ACT na yuko upinzani ili kusoma ramani dhidi ya CDM. Katika mazingira hayo hakuna uwezekano wa kumuamini Zitto.
 
Ni Heri wachache tuumie na hata tuuwawe mwaka huu ila vizazi na vizazi vijavyo vya Tanzania viishi katika Tanzania bora yenye haki na maendeleo ya kweli ya watu na vitu.
Mpo hapa mnajitekenya na kucheka wenyewe, wala hutauawa utapigwa tu miguu ipinde na Lissu tarehe 2 November anakimbilia ubelgiji huku nyuma wewe na wenzako mnachechemea kwenye wheelchair.

Narudia tena Lissu hawezi kuja kuwa Raisi wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania. NEVER. Hizi kelele zenu humu zimebakiza siku 7 muufyate. Na mjiandae kisaikolojia mapema.
 
Huyo Membe hata kabla hajafukuzwa CCM nilisema kabisa huyo sio wa kumuamini, na wengi wetu tulisema hata akiondoka CCM asipokelewe CDM, na hata akipokelewa asipewe nafasi yoyote, kwani somo la Lowassa lilikuwa bado bichi. Na kweli kaondoka CCM kwa maelekezo maalum, akaenda ACT ambapo alikuwa analazimisha muungano ili yeye ndio awe mgombea kwa maslahi ya CCM. Nashukuru Mungu alipotezewa...
SASA UPINZANI NZIMA NANI MWADILIFU? MTAJE HAPA.
 
Tatizo la Act lipo Kwa zitto,hii mission yote anaijua vzr na wala kutoka moyoni hafurahishwi lisu kuwa raisi,zitto ni mnafiki na anajua kinachofanyika Kwa membe toka siku ya kwanza membe kujiunga naye,hata membe kutumwa kuja Act kuibomoa chadema ni mission za zitto.
 
Kwani shida iko wapi??? Suala sio nani awe kiongozi, Suala ni mabadiliko ya kweli ya kuikomboa nchi yetu!!
Kwani kuna shida gani akisema pamoja na Jina langu kuwepo kwenye karatasi ya kura, anaomba watanzania wampigie kura Tundu Antiphas Lissu
Mkuu, ninachotaka kusema hapa ni kwamba ACT wasingesimamisha mgombea kabisa ingeleta taswira yenye mashiko au mgombea wao angetangaza kujitoa kwenye kinyang'anyiro
 
Mpo hapa mnajitekenya na kucheka wenyewe, wala hutauawa utapigwa tu miguu ipinde na Lissu tarehe 2 November anakimbilia ubelgiji huku nyuma wewe na wenzako mnachechemea kwenye wheelchair...
Hata mtupige na kutuua wote. Hatuachi kulinda kura zetu mwaka huu!! Na kwa taarifa yako, Raisi wa Jamhuri ya Muungano Tanzania 2020-2025 ni Tundu Antiphas Lissu. Utake usitake
 
Mkuu, ninachotaka kusema hapa ni kwamba ACT wasingesimamisha mgombea kabisa ingeleta taswira yenye mashiko au mgombea wao angetangaza kujitoa kwenye kinyang'anyiro
Zitto ana tamaa sana, alitaka kupata viti vingi bungeni na alidhani Membe ni mtu sahihi kumbe ameingia cha kike
 
Mlimjua alafu makafanyaje?

[emoji23][emoji23][emoji23]Nyie watu wa Amsterdam mna shida sana.

Mkome kushobokea mambo ya ndani ya wana ccm!
 
Back
Top Bottom