Biashara gani unayoweza fanya yenye uwezo wa kuingiza milion 300 kwa mwaka kwa kutumia mtaji wa bilion 1?

Wazo sahihi kabisa, maana iyo B uitumbikize mtaani Tra wamekuangalia, manispaa wapo hapo mala fire mala wafanyakazi wanataka kutokea hapo yani kwa mwaka utakuta imebaki 500M na faida amna, mazingira ya biashara Tz sio rafiki hata kidogo
Mazingira ya biashara Tanzania (tuseme kwa nchi zinazoendekea) ndiyo yanasababisha biashara zife ama kudorola chanzo chake ni jamiii kunyamaza kwakupokea hata sera ambazo hazina tija. Huwezi kupanga namna ya kuendeleza biashara yako kwa sera ambazo hazina muelekeo
 
Milioni mia tatu Kwa mwaka ni sawa na milioni 25 Kwa mwezi na ni sawa na laki 8.34 Kwa siku. Inawezekana!
 
Mtaji wa 100M kufungua wholesale pharmacy ni uongo (hautaweza kuhudumia).

Ukitaka kutoboa kwenye biasha ya madawa, ubahatike kuwa wakala wa kikanda wa pharmaceutical companies za maana kama Shelys na nyinginezo (sanasana shelys maana hao hawajau kuleta dawa sokoni ikafeli), angalia dawa kama AZUMA waliyoileta hivi karibuni, nani haijui?

Kuliko kupigania kujenga brand kwa 1B (ambayo ni ngumu), ni bora kufukuzia uwakala.
 
Elezea zaidi kuhusu Shelly's, unawajua Regal pharmaceutical wa Kenya?

Kuna faida zipi kuwa wakala na kuna risk zipi kuleta brand mpya sokoni?
 
Yeah na ndo nilichomshauri, apambane awe wakala wa drugs ila sio kuleta wholesaler pharmacy
 
Nimecheka sana baada ya kusoma comments zote [emoji38][emoji38][emoji38][emoji1787][emoji1787][emoji1787] nimeamini matapeli ni kama maji kuwakwepa kazi
 
Je, ni biashara gani unayo weza fanya yenye uwezo wa kuingiza milion 300 kwa mwaka kwa kutumia mtaji wa bilion 1?

Wekeza kwenye hisa za hati fungani, nmb, crdb, utt amis, Kama umewekeza 1b , basi Kwa mwenzi 1 utakuwa unapewa 10m, Kwa mwaka 120m , alafu uhakika bila kufanya Kazi , ni pesa ndio inayofanya Kazi .
 
Hii ni uhakika asilimia 100 maana huduma ya madawa bado haijasambaa kwenye wilaya zote na vijiji vyote Tanzania,lakini ukiachilia mbali pharmacy pia kuna biashara ya zahanati/hospitali haina upinzani ni uhakika.
Nimeshuhudia mifano ya watu kadhaa ambao walianzisha zahanati miaka ya nyuma na sasa hivi ni mamilionea wanaelekea kwenye ubilionea.

Sent from my SM-C7000 using JamiiForums mobile app
 
Biashara ya mabus unapata pesa hio pesa lakini hii biashara inawafaa vijana umri ukienda Jenga za kupangisha utu mabus utakufa siku si zako
Hii ni ukweli kabisa imagine uko zako nyumbani umetulia unapiga hesabu za makusanyo unapigiwa simu gari yako imetekwa Congo na ilijaza mzigo wa mtu

Sent from my SM-C7000 using JamiiForums mobile app
 
Dah kuna watu mko na michanganuo mikali sana ya biashara sema ishu mitaji tu.
Inaonekana Bongo hakuna project kama hii bado

Sent from my SM-C7000 using JamiiForums mobile app
 
umesema kitu kitu kinachowezekana... Ila anapotaka kuanzia ni mlima wa juu sana, kuanguka ni rahisi na moja moja, huamki tena.... Anza na mtaji kidogo kwa plan hiyo hapo juu, halafu uscale kadri itakavyokuwa inawezekana.
 
Wazo sahihi kabisa, maana iyo B uitumbikize mtaani Tra wamekuangalia, manispaa wapo hapo mala fire mala wafanyakazi wanataka kutokea hapo yani kwa mwaka utakuta imebaki 500M na faida amna, mazingira ya biashara Tz sio rafiki hata kidogo
Hivi hawa fire huwa wanachukua hela za nini ilikiwa shirika lao ni la kipumbavu vile kila wanapohitajika kutoa huduma.?

Tz ni nchi ya kijinga sana...!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…