Mac Alpho
JF-Expert Member
- Aug 5, 2019
- 13,953
- 27,825
Ninaweza kusema Shelys ni moja kati ya makampuni ambayo yamepenyeza na kuuza dawa zao kwa wingi sana sokoni na mara zote hawajawahi kuja na dawa kisha ikawa na mauzo madogo. Kwahiyo unapokuwa wakala wa kampuni kama hii ni wazi kuwa mzunguko wa biashara unakuwa ni mkubwa sana.Elezea zaidi kuhusu Shelly's, unawajua Regal pharmaceutical wa Kenya?
Kuna faida zipi kuwa wakala na kuna risk zipi kuleta brand mpya sokoni?
Faida zake ni kwamba wakati wanakuletea mzigo kuna kuwa na mzigo mwingine ambao unakuwa ni kama bonus, na mara nyingi utapokea mzigo mkubwa kuliko kile ulichostahili kutoa kama ungekuwa unanunua ilu ukauze, sambamba na hayo kuna incentives mbalimbali ambazo hutolewa pale unapofikia na unapovuka matarajio ya mauzo kwa kipindi kadhaa kama vile Magari (ya maana) nk.
Hapa chini ni orodha ya dawa zilipo sokoni chini ya Shelys:-
COLDRIL, AZUMA, HEMOVIT, ALBENDAZOLE, ERTHROMICINE, PANADOL, SHELADOL, ACTION ,GOODMORNING, DICLOPER, CYPROFLOXACIN, MALAFIN na nyingine nyingi tu.
Hebu angalia hizo dawa kisha uniambie ni dawa gani hapo ambayo haikukimbiza sokoni? Fikiria umekuwa wakala wa kampuni kama hiyo, kisha ujiulize mzunguko wake. Nina mfahamu jamaa mmoja aliyekuwa wakala wa Shelys kanda ya ziwa (Ashif Ladhan) walipiga sana hela enzi hizo.
Kuhusu Regal pharmaceuticals sifahamu mengi zaidi kuwahusu japo ninatambua uwepo wao.