Biashara inataka watu wenye roho ngumu, fikiria nimewekeza 300M+ napata 5M kama faida Kwa mwezi

Hiyo pesa angeingiza huku wala asingekuja kuleta hili bandiko.

Hapo ukipata gari 5 za 60 mln una uhakika wa kulaza 15 kila mwezi na hapo umetoa malipo yote.
 
Huyo jamaa atakuwa anakula ndefu sana mkuu, hebu imagine mtu ana 20B halafu wakupe 12% tu ni hela tamu kiasi gani?

12%×20,000,000,000 aisee dunia ni tamu ukiwa na hela ndefu. Imagine 2.4B kila mwaka wastani wa hela ya kila mwezi ni 200M! Hivi kila mwezi niwe naingiziwa million 200 nina haja gani ya kupasuka kichwa na TRA sijui uja file returns mara sijui ujinga gani.

Na ndio maana BOT wameshusha rates maana ni noma yani, matajiri wengi wamehamishia mitaji huko.
 
Naomba unieleweshe kuhusu hii kitu
Unapeleka hela hio bank wao ni wakala wa bonds wanazinunua BOT wanawauzia wateja wao. Kiasi utakachoingiza kwenye bonds unakuwa unapewa gawio kwa asilimia kadhaa kila mwaka. Kwa sasa hao UTT ni 12% ya hela yako kwa mwaka. Bonds ziko miaka tofauti kuanzia 10-15-25 wewe tu utataka hela yako ikae muda gani.

Hio miaka ikitimia unapewa hela yako kama ilivyo kama uliweka 200M utakabidhiwa bila kupunguzwa hata sent 5, hamna mambo ya makato kwenye bonds unakula faida kama ilivyo.
 
na ndio maana ili uwe na biashara yenye mafanikio, lazima uwe kwenye mtandao wakukwepa kodi, kufanya magendo,
Yani hilo ni dunia nzima, una option 2, ukwepe kodi au ufanye smuggling ndio utapata mafanikio ya kutisha kwenye biashara au uwe na mtaji mkubwa sana ili baada ya kuondoa expenses faida ibakie kubwa.
 
Hela hiyo ikukute huna majukumu ya ada sijui ujenzi ndio utafurahia sana na mpenzio
Bado ni hela ndefu sana
Ada inalipa,ujenzi unakuwa ushamaliza.
Huwezi kushika hela ndefu hivyo halafu usiwe umejenga.
 
Hii trend ya matajiri kufunga biashara na pesa kupeleka bot bond iko moto sana. Hata Shabiby alishawahi kulisema bungeni.

Shabiby alishawahi kulisema bungeni sikiliza Kuanzia dakika ya 8

 
2B kwa mwezi unaingiza sh ngapi mpaka aweze kuwapa 4mil watoto 7????
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…