Biashara inataka watu wenye roho ngumu, fikiria nimewekeza 300M+ napata 5M kama faida Kwa mwezi

Watu wanachanganya sana kati ya
aina za Uwekezaji, Biashara ,Kuajiriwa na kujiajiri...!

Sio kila Biashara ni Biashara, nyingine ni ajira (kujiajiri) tu
imagine umejiajiri hujilipi mshahara ,huna likizo,huna bima , hujilipi mshahara unaoeleweka
Watu wanatudharau ambao tumeajiriwa eti tunakuwa watumwa. Inategemea na ajira yenyewe jamani. Mtu unalipwa net salary kuanzia 5 m na kuendelea , hapo unalipiwa bima ya afya, mshahara wa likizo, NSSF etc. Kwa ambao hatutaki kukopa bank ajira zinasaidia kukusanya mitaji na kufanya biashara huko ukiendelea kula mshahara wako
 
Haipaswi kudharauliana ...kwakweli mana kujiajiri na kuajiriwa kuna faida na hasara respectively
 
Tatizo wewe hujui elimu ya biashara.
Biashara ni kipaji kama ambavyo watu wanavipaji katika issue zingine. Tukubaline tukigrade talents kuna best mpaka worst katika kila talent. Na ukubali tu wewe sio talanta yako biashara.

Sio kisa una 300m unawekeza sehemu ambayo haihitaji uwekezaji wako. Tuliokulia katika biashara huwa tunasema hakuna biashara mbaya Dunia, tatizo biashara yako umeweka sehemu sahihi?

Nikupe pole sana faida unayoipata kwa wastani huzalishwa na mtaji wa 30m.

Sent from my TECNO BA2 using JamiiForums mobile app
 
Hapo kwenye ardhi fafanua bhac mpendwa ...kuwekeza how ...coz kuna wigo mpana sana hapo.....
A) Kununua ardhi na kusubiri ipande thamani
B) Kilimo
C).......
D).....

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama

Ukilenga ist kwa million 7 kisha ukaingizia laki 5 unaweza kuja kuiuza 9m kwa haraka ikawa ni ongezeko la million2. Ukiuza gari 3 kwa mwezi una bei gani???

khee nmejiuliza hii kitu[emoji1787][emoji1787][emoji1787] mwisho ndio nikaelewa unatumotivate[emoji38][emoji38][emoji38] eti ukiuza gari 3 kwa mwezi una beingani??? nikasema biashara ganinhii nzuri ivi imenipita[emoji23][emoji23]
 
Kabisa mzee mwenzangu wa forex..

Mimi nikipata hiyo milioni 300 ambayo ni sawa na dola 120,000 kila mwezi ntakuwa natengeneza dola 40,000
 
khee nmejiuliza hii kitu[emoji1787][emoji1787][emoji1787] mwisho ndio nikaelewa unatumotivate[emoji38][emoji38][emoji38] eti ukiuza gari 3 kwa mwezi una beingani??? nikasema biashara ganinhii nzuri ivi imenipita[emoji23][emoji23]
Eeh lazma uchangamshe ubongo
 
Hapo kwenye ardhi fafanua bhac mpendwa ...kuwekeza how ...coz kuna wigo mpana sana hapo.....
A) Kununua ardhi na kusubiri ipande thamani
B) Kilimo
C).......
D).....

Sent using Jamii Forums mobile app
Inategemea ardhi ipo sehem gani, kuna sehem zinafaa real estates etc.

Nb usije nunua ardh ya kama mil 300 ukaweka kilimo utasaga meno.
Hapo kwenye ardhi fafanua bhac mpendwa ...kuwekeza how ...coz kuna wigo mpana sana hapo.....
A) Kununua ardhi na kusubiri ipande thamani
B) Kilimo
C).......
D).....

Sent using Jamii Forums mobile app
Kiwanjaa kama kiko barabarani sehem nzuri wawekezaji wa shell za mafuta lazima ule pesa zao.

Au kiwanja kipo ushuani basi ule pesa za matajiri wasiopenda kuishi changanyikeni.

Au kujenga ma Godown. Yanahitajika sana. All in all inategemea kiko wapi na kinafaa kwa matumizi yapi.
 
Siwez kumuamini mbongo Kwa hizi story Kwa nilivyotapeliwa
 
Upo sahihi kabisa, ila najiuiza kiwanja cha barabarani kwa sasa unakipata kwa bei gani, yaani nafikiria barabara kama goba-madale-wazo, sioni wapi utapata eneo la barabarani kwa bei ya kawaida, au mbezi-kinyerezi-segerea, kifupi 300m kupata kiwanja barabarani ili uvizie wateja wa kujenga filling station au godown ni ndogo. Niko tayari kukosolewa.
 
kwa nini usikope benki kama hiyo biashara inalipa sana?
 
Sio forex kweli hii
 
Kwa hiyo hela nafikiri kama ungeiweka kwenye bonds ungeondokana na hizo headaches kabisa. Fanya 12%×300,000,000, hio ni uTT ila BoT wanatoaga hadi 15% at times.
Mimi hii kitu nataka sana elimu yake
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…