Biashara inataka watu wenye roho ngumu, fikiria nimewekeza 300M+ napata 5M kama faida Kwa mwezi

Kabisa mzee mwenzangu wa forex..

Mimi nikipata hiyo milioni 300 ambayo ni sawa na dola 120,000 kila mwezi ntakuwa natengeneza dola 40,000
Hizo mbona nyingi sana hata USD 15,000 tu kitozi.
 
Nissan civilian zinalipa sana kwa biashara ya dala dala , wapemba wengi zimewatoa .
Siri kuu ninkuwa tumia nissan kama Big G, ikiisha utamu unatupa!! Usije jaribu kutengemeza nissan.
Hii ya kutengeneza Nissan (Caravan) ilinigharimu sana.
 
Kuna jamaaa walijiunga haya madude sijui ukiunga mtu level inapanda mara Hela ya siku inapanda wanafurahi mtihani ukaja walipotaka kutoa ndio wakajua hawajui....
Hela zinatoka bosi mimi kabla sijaanda hizo link na kuzisambaza nilijiridhisha kabisa nijue kama zinatoka au laa
 
Kuna motivational speaker atakuja hapa atakwambia 'mimi nipe mil 10 tu nakupa faida ya mil 3.5 kila mwezi"
Usiwawenge sana motivational speaker, kuna uwezekano mkubwa kabisa mleta mada ni muongo! Mil.5 ni faida ndogo mno kwa capital ya 300mil.

Katika hali ya kawaida kabisa, bila presha, milioni 10 inaweza kukutengenezea faida ya milioni 1 kwa mwezi. Mimi siyo motivational speaker, Huu ndio uhalisia.
 
Nilichokigundua Kwa watanzania wengi hawajui biashara na misingi yake ndio maana Kuna kufeli sana kwenye biashara.
Asili ya biashara imekaa kimfumo na lazima ujifunze kuufuata, biashara sio kuwa na mtaji tu na kuzalisha faida.Tena Kwa watanzania wengi wanawaza faida ya nusu Kwa nusu au super profit Kabisa ya 150%au 250%,sasa Kwa mifumo ya biashara na asili yake hiyo sio biashara huo ni wizi.
Kwa asili ya biashara na mifumo yake,inapoanza inaanza kufuata hatua,hizo hatua zikirukwa tu basi hapo baadae kidogo tu lazima biashara itadondoka na huyo mfanyabiashara atafunga biashara na ataanza kufikiria kuanzisha biashara nyingine.
 
Biashara lazima ianze Kwa kujengewa misingi katika hatua za mwanzo,na katika hilo inaweza chukua muda kidogo kuweka misingi imara na katika hizo hatua za ku cement au ku intensify msingi wa biashara husika faida ya 5 Hadi 8% Kwa mwaka ni sahihi Kabisa Tena sahihi haswa haswa Kwa sababu kumbuka kuwa hauwezi ku control soko,ila unaweza kudhibiti baadhi ya mienendo ya baishara yako ili uende sawa na soko.
Kumbuka soko ni muunganiko wa wateja na wauzaji na Bei ya bidhaa,katika huo muunganiko ndio tunapata soko na kwa maana hiyo soko linaundwa na watu,ndio wauzaji na ndio wateja na watu wanayo maamuzi Yao binafsi wakiwa kama wauzaji na wateja pia.
Kumbuka Hawa participants wanafanya maamuzi kila dakika wanafanya maamuzi kwa hivyo katika hiyo dynamic zinatokeza nguvu za soko ambazo hakuna anayeweza kukinga ngoko zake na akazizuia,Cha msingi kufanya ni kufuata ethics za biashara ili kuweza kumudu kudumu sokoni.
 
Kumbuka wataalamu wanakuambia biashara yoyote mpya inaanza kuwa stabilzed sokoni baada ya miaka 7 plus,haijalishi biashara imeanza na ku boom au na kudorora,ila ukiweza kumudu kudumu sokoni miaka 7 basi hapo Kuna angalau uhakika wa kuanza kukua kibiashara,sio suala la muda mfupi kama watanzania wafanyavyo.
Ndio maana Hawa wenye asili ya Asia wenye biashara zao hawajaanza biashara Jana Wala juzi,sote sisi tu mashahidi unakuta familia ya kihindi au kiarabu na Wachaga Kwa mbaali wanafanya biashara miaka na miaka sio kwamba wamedandia tu.
 
Biashara hiyo Kwa gross return ya 5%per annum Kwa mwanzo wa biashara sio mbaya Kabisa na nadhubutu kusema kaanza vizuri tu,Cha msingi ni kuendelea kulisoma soko kutokea angle aliyopo kadiri muda unavyokwenda utakuja muda kupata faida ya 10 to 15% Kwa mwaka ni jambo la kugusa tu na baada ya hatua kadhaa tena ataweza kushuhudia faida Hadi ya 50% mpaka 150% kiasi Cha miezi kadhaa tu.
Na hayo yote hakuna chuo au mkufunzi nguli duniani atakufundisha,yote utayajua wewe mwenyewe sokoni,in a very unique way of yours.
Ndio maana kila mfanyabiashara au kampuni ya biashara inakuwa na Siri zake za kibiashara.
 
Seriously ninachokwambia na hiyo 7m nimeweka minimum hela unaweza pata mpaka 10m kwa week kwa 300m.
Just Google novatechfx come
Soma then kama you need more information lemme know.
Hizo fx zitakufilisiji
 
Uko sahihi hizo connection sio za kila mtu inategemea unaishi wapi.mimi ninapoishi naitwa mezani ishu kubwa kubwa chap nawafata matajiri au kuwapigia pale inapowezekana tho wenye mkwanja hawapokeagi simu lazima kumuona face to face.
Hapa kuna mkubwa namtafuta yaani ni ngumu kumpata mpuuzi yule. Chawa wake wanauliza nataka wa nini na staki kuwaambia sababu, panya wale lazima nipitie mgongo wa kazi nimuone yule mtu.
 
Biashara zinatofautiana Sana katika uwekezaji na faida inayopatikana.
Unaweka kikubwa unavuna kidogo Sana.
Unaweka kidogo unavuna pakubwa.
Hatuwezi kufanya biashara za kufanana. Kila mtu ana fursa zake katika maisha.
 
Achana na hicho unachokifanya
SCALP
NASDAQ, DW, US30, XAUSD
million 300 ni sawa na dollar 120000 hv
Ukikaza, hiyo million tano unapata kwa siku
Lakini hiyo shughuli yake kwanza, kwanza n'cheke
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23], niko uko mkuu, ni hatari, ila hella napata kwa lot ndogo tu
 
Achana na hicho unachokifanya
SCALP
NASDAQ, DW, US30, XAUSD
million 300 ni sawa na dollar 120000 hv
Ukikaza, hiyo million tano unapata kwa siku
Lakini hiyo shughuli yake kwanza, kwanza n'cheke
Et ngoja kwanza nicheke[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Biashara niloanza nayo ni ya mil10.8
Ilikuwa inanipa faida ya 1.6 au 1m net profit kila uzo, ko kwa mwez mida mingine mpaka mil3
Japo nilipewa frame na stoo bure
 
Biashara ni mahesabu, haina formula, ila kujenga bland ndo formula
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…