Kuna mengi nimejifunza hapa....mkuu mlikua mna import dawa gani na gani?Naweza nikawa nje ya mada ama sahihi
Kipindi nikiwa kwenye kampuni x kabla haija stop operation zake.....
Ilikuwa ni kampuni ya pharmaceuticals na ilikuwa inaagiza dawa kutoka uchina .......
Maake hapo naona umesema pia una kampuni na una wafanyakazi wanne.....
Basi ile kampuni ukimweka MD, MIMI, WATU WA SALES 3, MLINZI KAAJIRIWA NA KAMPUNI YAKE SO SIMWEKI HAPO...
Tulikuwa watu watano tuu...... Mtaji wake ulikuwa mkubwa kwakweli japo mwanzoni alikuwa mbishi mpaka ajisikie ndo aruhusu oda....
Mimi nikawa naichukulia biznez kama yangu ikitokea odaa hata hajaruhusu namwambia mteja aingize pesa kwenye account ya kampuni then mm ni deal na MD,
Biashara ukiichek Haina matangazo sijui insta wala Facebook.... Ila nilikuwa nikisimamia shoo kwa siku hata mio 20 tunauza nikishirikiana na watu wa sales....
Na mtaji wake unasoma parefu kuleta dawa maake alikuwa anashusha 40ft container
Naamini hata wewe mkuu usife moyo utafika wakati unashusha container tuu ...... na kufanya kile unachotaka kwenye biashara yako mkuu....
Kila la khery
kwanza dawa ni paracetamol zenye box la kijani kutoka chinaKuna mengi nimejifunza hapa....mkuu mlikua mna import dawa gani na gani?
Kwenye pharmaceutical industry kipindi unaanza ukiwa na team nzurii...ukiweka miezi mitatu ya kuingia mtaa kufanya marketing na uwe na Bei nzurii pia delivery ya haraka una kick off.
SEMA madawa Yana brand nyingi mfano fluconazole tabs Kuna brand zaidi ya 10 kwa uchache flucan,flucoz, fluderm,zocon,flucazol,flucona denk,fungstop, treflucan, diflu,austfluzole
Dawa moja Ina Brand nyingi Sana Kuna cheap brand pia Kuna brand za Bei juu so you need huge capital
Ushindani sokoni Kuna cutrought competition pia kutafuta customer base/ you can't own customer ndio maana Kuna mtu atakupa oda Kwako na ataenda kununua kwingine pia MUHIMU ""A SATISFIED CUSTOMER IS A FREE AGENT""
Mkuu,
Kumbe hata wewe una madini mengi Sanaa...nikipata utulivu ntakua na donoa donoa..
Umeandika vyema Sana reputable institution/company nyingi huwa wanapenda njia nyoofu..risit ni must hakuna janja janjaa... otherwise uwe na accountant/ mhasibu mzuri wa kucheza na FINANCIAL STATEMENTS OF THE COMPANYkwanza dawa ni paracetamol zenye box la kijani kutoka china
Japo alisema kwa badae angeanza ku import na nyinginezo.......
Lakini nilichojifunza kwenye pharm industry cha kwanza uhakika wa mtaji uwepo, hii itakufanya uweze kununua mzigo mkubwa kwa wakati ama kupishanisha muda.....
Mfano contena linaweza toka china Leo mpka lifike dsm.... (Bandarini sio chini ya siku 40 na kuendelea hapo ni pamoja na siku za kukaa anchor rage labda itatumia siku 28 itafika pale zinakopaki anchor rage ili kusubr foleni kama ipo ama issue za documentation na clearing ili meli iingie bandarini ambapo ni siku kumi na mbili ...... Inabidi ucheze na ratiba kama ikiondoka Leo mzgo mwingine uondoke next week au kila week unaagiza kama mtaji upo ama unafanya sales kwa haraka)
Kingine ni Kujua bei sokoni....... Kuna wakati unakuta box ni 300,000 sehemu zingine na 310,000 kwingine 290,000..... Kwahiyo unavyo mchek mteja unamsikilizia kama atakupa news maybe dawa zimepanda ama zimeshuka asiposema chochote ni kuandaa invoice, EFD receipts then mzigo umfikie.......
Akionyesha kulia sana labda achukue box nyingi kwa mia tatu pengine.......
Maake ukikaza na bei kubwa watakimbia, ama ikiwa chini utapata faida ambayo siyo......
Delivery na kuzingatia muda.......
Wateja wengi walikuwa wahindi plus wabongo najua wabongo akiomba oda saa hz km Hana haraka hata kesho atakwambia fresh.... Tunajijua 😂
Njoo kwa muhindi akisema saa hz..... Yaani delivery yake fanya haraka it's better umpe taarifa kwamba Leo hutoweza au utachelewa afu umzingue...... Ataenda kwa wahindi wenzie......
Lakini awe mbongo muhindi mkenya kwenye delivery kuwa smart...... Kama huna gari la kampuni hakikisha una watu unaowatumia at least kwenye gari una watu watatu na bajaji ili ukimkosa huyu mwingine ni rahisi kuja na kukupelekea mzigo
Kwa muhindi invoice na risiti ya EFD ni muhimu huna utarudi na mzigo hapo ndo nilipoona tofaut ya wabongo na wao kwenye business.......
Pia mbali na watu wa sales unaweza kutafuta watu au kutoa offer kwa mtu yeyote mradi ajue ishu za kumpata mteja ........ kwamba akipata mteja anaechukua maybe kuanzia box 50+ na kuendelea utamlipa commission hii ilikuwa inatumika sana unapata wateja wengi tofaut tofaut kwahiyo watu wa sales zaidi ni kupeleka mizigo na kukusanya hela......
Niliobserve zaidi hii ..........
In JF we are anonymous.Mbona hapa jf hutangazi!?
Hizi ni fikra za kimasikini.Anyway kifupi we na wenzako ni matajiri ila jua yote mtayaacha hapa hapa duniani
Usiwe na hasira sana boss mengine ni kuchamsha mada na genge ila tunapambana Kila kukichaIn JF we are anonymous.
Hizi ni fikra za kimasikini.
Usiache kupambana, tafuta sanaa pesaaa.
#YNWA
#YANGA_BINGWA
Hata wewe hujui maana ya business.. ku-buy na ku-sale ni aina ya biashara kwa jina la TRADING. Business sio trading peke yake. Kuna kuuza huduma pia. Wewe Dr wa mifugo rudi shule.Ukienda kupanda miti njombe, kulima mpunga, kuweka mizinga ya nyuki Tabora au kujenga nyumba ni baadhi ya mifano ya investments
Business ni ku buy na ku sale bidhaa nadhani umenielewa japo nimeelezea kwa uchache..
Nakubaliana na wewe watu wengi hupoteza focus wakidhani wanafanya vibaya kumbe wanayotamaniMkuu kuhusu mienendo ya wenzio isi kupe wasiwasi au morali ya kufanya Kama wanavyo fanya wao.
Kwani Kuna msemo una sema¹ 'jikune uwezavyo", kwani kila mtu ana kimvuli chake, kwa urefu wake na hata upana wake.
Kikubwa tazama biashara yako kwa makini, uone Kama Kuna sehemu ya kuboresha, kurekebisha au hata kuongeza ili uji kuze.
Hii tamaa ya kufanya kila biashara imewafilisi watu wengi wasio na msimamo na kujikuta kila siku wakianza mojaKingine biashara ni Kama mke (japo sisi ni kataa ndoa), njiani uta ona wanawake wengine wazuri, wanene, warefu au warembo zaidi ya ulio muacha nyumbani.
Zingatia hao unao waona huwa jui vizuri kitabia, kimawazo, ki fikra na hata asili zao.
Je uta muacha mkeo ili uendane na speed ya hao wazuri??, jibu ni lako mzee.
Genge la nyanya hawezi kuliwekaBiashara si ni matangazo, weka hapo hio insta page Yako Wana jf tukupe support
Nimecheka kama mngeseHii inasaidia nini kwenye Kitabu cha Kaflag?
Nimekuja K11Tanzanian Dream njoo utupe data za kiroho ili biashara itoboe
Do business in order to become an investor.....so business is not the end goal it's just a tool to reach the end.Business is better than investment.
Tuendelee kutafuta pesa.
Faida za receipts ukipata mtu anaejua kazi ya hesabu vizuri ni kuwa utawatolea wateja risiti za TRA, then wakati huo huo unarekodi mauzo kwenye Tally /quick books kwako sijajua mnatumia nini ama wengine wanatengeneza kwenye excell .....Umeandika vyema Sana reputable institution/company nyingi huwa wanapenda njia nyoofu..risit ni must hakuna janja janjaa... otherwise uwe na accountant/ mhasibu mzuri wa kucheza na FINANCIAL STATEMENTS OF THE COMPANY
Paracetamol tabs za china kwa 1pc mlikua mnauzajee...maana kwa Sasa kwenye whole sale wanauza kwa box moja 1250 mpaka 1500 nyinyi mlikua mnauzajee..
Madini ya pharmaceutical industry yapo mengi Sana mkuu tukaendea kuandika andika kila tukipata wasaa wa kufanyaa
Invest in active income and not in passive income.Do business in order to become an investor.....so business is not the end goal it's just a tool to reach the end.
1. Mohamed Enterprises Tanzania Limited wapo kwenye ....Mkuu Liverpool VPN , naomba elimu ya ufahamu hapo kwenye "kampuni moja inayofanya biashara tofauti tofauti".
1. Mohamed Enterprises Tanzania Limited wapo kwenye ....
a. Tradeco Soap = Brand Name MO SOAP
b. Vinywaji = Mo Colla, Mo Extra, Mo Pineapple
c. Kampuni ya Usafirishaji
d. Mo insuarance
E.T.C
2. Vunja Bei group and Company wapo kwenye ...
a. Mavazi
b. Dawa (pharmacetical)
E.T.C
3. Bakhresa Group wapo kwenye ....
a. Vinywaji
b. Chakula
c. Media
d. Usafirishaji
E.T.C
#YNWA
#YANGA_BINGWA
1. Paint manufacturers wapo InstaHayo ya Instagram na Facebook,
Nadhani pia yanategemea na aina ya biashara mnazofanya
(Huenda bidhaa zenu Ni za kufunua na kuchagua chagua Sana).
Sisi wa electrical na Hardware sidhan Kama inatuhusu Sana, mteja anahitaji bidhaa na brand, anakupa pesa.
Mwaka WA 18 huu Niko kwny game, nauza fresh kabisa bila hizo ista Wala Facebook.
Unamiliki kampuni ila unakuwa na brand name.Shukrani mkuu. Nimeelewa.