Biashara Tanzania ni pasua kichwa. Ukiondolewa kwenye reli, kurudi na kukaa sawa si rahisi

Biashara Tanzania ni pasua kichwa. Ukiondolewa kwenye reli, kurudi na kukaa sawa si rahisi

Daaaah Wakuu ,sitaki kukumbuka ila haina jinsi ku share na kunikumbusha mbali japo sio mbali sana,2016 kipindi cha mwenda zake,yupo kwenye high peak ,Mshua bhana alijilupua kwa kuchukua mkopo au hela za watu Bank ,kwa ajili ya kuzungulishia kwenye biashara zake za mafuta,HFO au kwa lugha ya malkia Heavy Fuel oils, ni mafuta ambayo yanatumika viwandani kwenye ma Boiler, alinunua HFO zipato litre 150,000 kwa ajili ya masoko yake nche ya nchi ya Kenya.
Akafanya biashara na mkenya baada ya kuja yard na kuukagua mzigo na kuona mnzurii sana,akalipa advance nyingine mpka mzigo ufike ndio atalipia kwa njia ya bank,..Mshua akatafuta semi tatu za kukodi Tanker,na unzuri Mshua alikuwa na Mende mbili Scania pulling na trailer zake ,vyuma vikapakia mafuta yrd,vikatoka Dar es salaam vinzuri tu mpaka boarder ya Namanga, Changamoto ndio ikaanzia hapo bhana,tumeonyesha documents na vibali vyote vya mzigo,wale majamaa ya wanaohusika kuvusha magari upande wa Kenya ,
wakawa wanakaza ,wakawa wasema mambo ambayo sisi tulijua wanataka chochote kitu lakini wapii ,wanasema mmbo yamebadilika kutokana na mfumo wa Sera za nchi,Tukawa wapole tukaona ngoja tuvumulie pale mpakani Namanga mambo yanawenza kuubadilika lakini wapii,tulikaa kalibia miezi miwili tukaona mambo yamekuwa sio mambo,
fikilia gharama za kupark na ulinzi wa magari,plus madereva ma turn boy ,escorter wa mzigo ,mkenya naye anataka aludishiwe hela yake ,Bank nayo hawaelewi wanataka marejesho yao ilikuwa Mshua anapitia kwenye kipindi kigumu sana mpaka ikafikia sukari kupanda na presure juu, Ila tunamshukuru Mungu alirudi kukaa sawa ,japo sio kama mwanzo ku recover ni ngumu mno,Aliunza baadhi za nyumba,mzigo bei ya hasara na magari pia ili ikawe sawa,
Vinzuri = vizuri, aliunza = aliuza, fikilia = fikiria, kalibia = karibia. Mshua alikataa kukupeleka shule au wewe ndo ulikataa kusoma?
 
Bro hata huko pia watu wataongezeka na ushindani utakuwa mkali sana. Kule India watu wana viwanda vya vifaa tiba kiasi kwamba huo ushindani sio poa.... huku kwetu bado watu wa madawa na vifaa tiba sio wengi kiasi kwamba kuna baadhi ya vitu vinakua shida kuvipata. Inachagiwa pia na hiyo aina ya biashara pia kutaka shule kichwani. Wanapoendelea kuongezeka vijana wasomi kwenye game huko nako kutachafuka.
Labda mtaji ndo utasababisha wasiwe wengi
 
Afadhali hao Ndugu zako mitaji yao ilikuwa inapukutika kidogo kidogo, mimi rafiki yangu alienda kuchukua nguruwe 200 mbeya wenyewe thamani ya mil 50,kumbe homa ya nguruwe ilikuwa imeanza kuingia kimya kimya anafika dar anawaswaga zizini kesho yake asubuhi anakuta nguruwe zote zimekufa.
Napewa taarifa rafiki yako amepoteza fahamu yupo rabinisia baada kupata fahamu akasema mapambano yanaendelea😄
Mapambano yanaendelea, nimeipenda hii. Ni wachache wenye mioyo ya hivi.
 
Wahindi na waarabu wanabebana sana huwa hawakubali kuona mwenzao amefilisika,ila kwa watu weusi ukifilisika huo mzigo ni wako peke yako usitegemee kuna mtu atakuja kukuinua.
Utamaduni wetu ni wa kuchangiana harusi tu.

Sent from my SM-C7000 using JamiiForums mobile app
Kuna familia ya wachaga naifahamu, ndugu yao alipata shida na benki wakataka kuuza nyumba. Ulipigwa mchango mbaka madogo wengine wa chuo walitoa, yule mzee alinasuka na sasa dealer mkubwa tu wa vinywaji .....kubebana ni talent nadhani, kabila zingine hizi mko wachache mbebane, mnarogana wote muwe chini. Aseeee
 
Kuna familia ya wachaga naifahamu, ndugu yao alipata shida na benki wakataka kuuza nyumba. Ulipigwa mchango mbaka madogo wengine wa chuo walitoa, yule mzee alinasuka na sasa dealer mkubwa tu wa vinywaji .....kubebana ni talent nadhani, kabila zingine hizi mko wachache mbebane, mnarogana wote muwe chini. Aseeee
yes ni kabila chache wana mwamko wa kusaidiana,ila kabila zingine ukifirisika ndio wanafurahia ushuke wote muwe sawa
 
Vinzuri = vizuri, aliunza = aliuza, fikilia = fikiria, kalibia = karibia. Mshua alikataa kukupeleka shule au wewe ndo ulikataa kusoma?
Mama Samia
Kwa huo mda nilikuwa nasoma mbado,nipo 1st year ndugu
 
Mimi mshahara wangu unanitosha... Napata pesa najenga nyumba zangu mdogo mdogo... Nikikaribia kustafu nyumba zangu mbili tatu na fremu zitanilisha...
Biashara ni kipaji sio kila mtu anacho... Na sio kila mtu anaweza kufanya biashara... WaTz wengi mnafilisika kwasabab ya kuiga kufanya biashara kama fulani... WaTz wengi wakiona biashara fulani ina trend basi wote wanaitaka... WaTz wengi sana wanafanya biashara ili waonekana tu wakat ukweli hakuna faida wanayoingiza... WaTz wengi biashara zao ndogo wanataka ziwalipie kodi zisomeshe watoto wale bata na kuhudumia ndug, jambo ambalo haliwezekani kiuchumi ktk biashara...

dah we jamaa mbona kama tunatembea kwenye boat moja.. maana plan hio ndio naifanyia kaz sasa hv..
 
Mimi mshahara wangu unanitosha... Napata pesa najenga nyumba zangu mdogo mdogo... Nikikaribia kustafu nyumba zangu mbili tatu na fremu zitanilisha...
Biashara ni kipaji sio kila mtu anacho... Na sio kila mtu anaweza kufanya biashara... WaTz wengi mnafilisika kwasabab ya kuiga kufanya biashara kama fulani... WaTz wengi wakiona biashara fulani ina trend basi wote wanaitaka... WaTz wengi sana wanafanya biashara ili waonekana tu wakat ukweli hakuna faida wanayoingiza... WaTz wengi biashara zao ndogo wanataka ziwalipie kodi zisomeshe watoto wale bata na kuhudumia ndug, jambo ambalo haliwezekani kiuchumi ktk biashara...
hili la trend nakubali 100%

Watz wanaigana mnooo
 
dah we jamaa mbona kama tunatembea kwenye boat moja.. maana plan hio ndio naifanyia kaz sasa hv..
Hiyo ya kujenga nyumba pia ni biashara ila na yenyewe ina chagamoto zake kubwa pia, unajenga nyumba ya 20m, unakuasanya 150k kwa mwezi, hapa ni biashara au kuua mtaji, pia kuna kuchelewesha kulipwa na mpangaji, hiyo ni biashara ya wastaafu ili kuwatunza tu ila haina masilahi
 
Hiyo ya kujenga nyumba pia ni biashara ila na yenyewe ina chagamoto zake kubwa pia, unajenga nyumba ya 20m, unakuasanya 150k kwa mwezi, hapa ni biashara au kuua mtaji, pia kuna kuchelewesha kulipwa na mpangaji, hiyo ni biashara ya wastaafu ili kuwatunza tu ila haina masilahi
Nyumba siyo kitu Cha kukuza pesa kibiashara, wengi tinaopanga kujenga nyumba za kupangisha ni kujiwekea uhakika wa pesa ya matumizi hasa chakula, maji,umeme na matibabu pindi ambapo huna kazi au umefikia umri wa kupumzikia, nyumba za kupangisha ni kitu kizuri sana iwapo mtu anaweza kuziweka town, zinalinda sana baadhi ya mahitaji muhimu nyumbani
 
Back
Top Bottom