Diwani
JF-Expert Member
- Oct 25, 2014
- 2,680
- 2,779
Kuna siku nilikuwa natoka Dodoma naenda Iringa, ilikuwa jioni, ikanilzimu ningoje gari kutoka Arusha, KIMOTCO, ikiwa imehitimu saa 11 Jioni, gari ilikuwa imeshawasili pale, tukaanza safari, pembeni yangu alikuwa amekaa mdada wa makamo, umri ni kati ya miaka 27-33.
Kwa kawaida mimi sio mtu wa stori, ila wakati nimefika Migori kwa ajili ya kupata hiki na kile wakati huo giza likiwa tayari limeshatanda, ilinibidi nikoleze stori na yule dada na hapa tulikuwa tayari kwa kiasi fulani tumeanza kuzoeana, na hata hivyo nilikuwa nimekaa nae meza moja.
Alichoniambia kilinifungua sana, akasema, "kama unataka pesa, ukimaliza masomo yako, karibu mpakani, Tunduma, TZ na ZAMBIA" maelezo yake tukaendeleza kwenye gari. Anasema biashara hunoga sana kwenye mipaka, watu wanapiga hela vibaya mnooo, kwa mfano yeye, awali alianza kununua nguo Kenya, tena kwa bei rahisi sana, good enough ni kwamba, quality ya nguo za Kenya ni kubwa sana, anakuja kuuza Dodoma, baadae akaanza kupeleka mzigo Zambia, kumbe hata siku ile alikuwa na mabalo anayasafirisha, ilikuwa jumatano, akaniambia hapo akikaa sana ni mpaka Jumapili, mzigo umeisha, baadae anatoka Dar na Vifaa vya Elekroniki anapeleka Arusha kwa sababu vina gharama kubwa mno', akisema hata nae hajui ni kwanini.
Kwa maelezo yake, alinambia mpaka siku ile niliyokutana nae, hakuwa hata na mwaka kwenye ile biashara, ila kuna uwekezaji mkubwa sana ameanza kuufanya Dodoma, nilikuwa na mawasiliano nae, akaniambia wiki mbili baadae angekuwa Dodoma kununua eneo ili baadae aje kukata vipande na kuliuza kwa ajili ya makazi.
Ni hayo kwa leo
Kwa kawaida mimi sio mtu wa stori, ila wakati nimefika Migori kwa ajili ya kupata hiki na kile wakati huo giza likiwa tayari limeshatanda, ilinibidi nikoleze stori na yule dada na hapa tulikuwa tayari kwa kiasi fulani tumeanza kuzoeana, na hata hivyo nilikuwa nimekaa nae meza moja.
Alichoniambia kilinifungua sana, akasema, "kama unataka pesa, ukimaliza masomo yako, karibu mpakani, Tunduma, TZ na ZAMBIA" maelezo yake tukaendeleza kwenye gari. Anasema biashara hunoga sana kwenye mipaka, watu wanapiga hela vibaya mnooo, kwa mfano yeye, awali alianza kununua nguo Kenya, tena kwa bei rahisi sana, good enough ni kwamba, quality ya nguo za Kenya ni kubwa sana, anakuja kuuza Dodoma, baadae akaanza kupeleka mzigo Zambia, kumbe hata siku ile alikuwa na mabalo anayasafirisha, ilikuwa jumatano, akaniambia hapo akikaa sana ni mpaka Jumapili, mzigo umeisha, baadae anatoka Dar na Vifaa vya Elekroniki anapeleka Arusha kwa sababu vina gharama kubwa mno', akisema hata nae hajui ni kwanini.
Kwa maelezo yake, alinambia mpaka siku ile niliyokutana nae, hakuwa hata na mwaka kwenye ile biashara, ila kuna uwekezaji mkubwa sana ameanza kuufanya Dodoma, nilikuwa na mawasiliano nae, akaniambia wiki mbili baadae angekuwa Dodoma kununua eneo ili baadae aje kukata vipande na kuliuza kwa ajili ya makazi.
Ni hayo kwa leo