Tissaphernes
JF-Expert Member
- Mar 27, 2018
- 2,902
- 3,560
Pasua kichwa
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Pole ndugu ila biashara hainaga ukaka, umjomba, wala usista! Bora hata mtu baki anaweza kukuogopa kidogo lakini si ndugu yako! Maana anajua hata akiharibu hutamstaki wala kumfunga!mimi nilimpa kaka yangu,tukaelewana kwa wiki anipe elf 25000, ila alichonifanyia,Mungu ndo anaona
Biashara hii wengi walipiga chini, iwe kwa mkataba au bila mkataba changamoto zake ni nyingi na zinaleta stress, kwa upendo kabisa tafuta idea nyingine sio hii, Mara nyingi mfaidika ni derevaWadau habari zenu.
Ninataka kuanza biashara ya bodaboda ila kwa mkataba. mwenye ujuzi naomba msaada wa maelezo inavyokuwa tafadhali. nahitaji kujua dereva anapaswa alete kiasi gani cha fedha kwa wiki, na mkataba huwa wa muda gani? na service anafanya yeye kwa pesa zake au nafanya mimi mmiliki? Naomba kueleweshwa tafadhal. natanguliza Shukrani.
Hovyo kama huna cha kuongea kaa kimya dharau ni kitu kibaya sana ....akuhiyo hela yako ya kununua boda boda bora unipe mimi niizungushe tu non risk.. nikurudishie kwa mfumo ambao boda boda ya mkataba inampa mmiliki..
tofauti yake ni kwamba mimi nakupa faida nusu ya boda wa mkataba angekupa... sabab hutakuwa na risk yoyote tofauti na boda boda inaweza ikagongwa au kuibiwa before mkataba kuisha...ukala hasara..
mimi naitumia kwenye tshirt business tu... naongeza tu mtaji na naagiza zangu plain tu somewhere
Tshirt Garage Mabibo Hostel (@tshirt_garage_mabibo_hostel) • Instagram photos and videos
na loundry shop yangu naongeza hela nanunua mashine heavy duty
[emoji121]hiyo hela yako ya kununua boda boda bora unipe mimi niizungushe tu non risk.. nikurudishie kwa mfumo ambao boda boda ya mkataba inampa mmiliki..
tofauti yake ni kwamba mimi nakupa faida nusu ya boda wa mkataba angekupa... sabab hutakuwa na risk yoyote tofauti na boda boda inaweza ikagongwa au kuibiwa before mkataba kuisha...ukala hasara..
mimi naitumia kwenye tshirt business tu... naongeza tu mtaji na naagiza zangu plain tu somewhere
Tshirt Garage Mabibo Hostel (@tshirt_garage_mabibo_hostel) • Instagram photos and videos
na loundry shop yangu naongeza hela nanunua mashine heavy duty
Pole kwa hiyo uliamua kuachana na hiyo biasharaHii biashara bwana bora uendeshe mwenyewe yaani ww ndio uwe dereva,vijana wanashida sana + mihemko basi tafrani tupu,labda umpate mwaminifu kwelikweli...mm ndani ya mwaka mmoja niliiuza tena kwa hasara sana,maana kijana wa kwanza kumkabidhi aiseee baada ya wiki mbili tu chombo kiko hoooi yaani mpaka roho iliniuma maana sikununua kwa mtu,.hapo bado hela huletewi kwa wakati nikaona isiwe tabu mwenyewe nikanyoosha mikono juu..
Utaendesha mwenyewe....???
Utanyanganywa.
Utampa dereva..??
Itaibiwa
Achana na hiyo biashara kichaa
Kweli kabisa.Boda boda kama hauna shuguli nyingine iendeshe mwenyewe, inalipa sana...la sivyo uifanye kama biashara ya kukusaidia kulipa kodi na hela ya mboga.
Nimekutana na watu wawili watatu baada ya kuona mishahara haikidhi (wasomi) wakaamua kuendesha boda boda...wote hawatafuti tena kazi.
Tatizo ni wale boda boda mapepe, wanafanya hio kazi ionekane ya wendawazimu.
Lakini wanapata zaidi ya hiyo mm ninaZimekuwa ni nyingi mno kwanza siku hizi wanaleta elfu saba sio 10
Biashara zote pasua kichwa hakuna biashara rahisi bodaboda mbona wengine wanafanikiwa na magari hivohivo na maduka hivohivo hakuna biashara rahisi muhimu ni kujipanga tu na kukubali changamoto,mfano bodaboda mpaka inakamilika mpya ni kama 2500000,dereva kila wiki hssabu 50000 service inategemea kwa wiki wiki mbili au mwezi inategemea na oil.kwa mwezi unaweza kupata 170000.muhimu hesabu zako uzieke sawaPole kwa hiyo uliamua kuachana na hiyo biashara
Unatumia mbinu gani kwenye Ku manage hapo vijana?Dah pole kwa kuishia njiani,kuna mbinu ulikosa za kuimanage .
Mkuu hapa umetoa mwangaBiashara ya boda boda ni nzuri, ila inategemea na aina ya madereva unaowapata, na aina ya mfumo unaotaka kuutumia. Njia ya mkataba ndio nzuri zaid kwani inakuwa haikupi stress. Madereva wako wengi ila madereva wazuri ni wachache sana. Cha msingi kama unaweza tafuta dereva aliye mzuri ongea naye awe kama msimamizi uwe unamlipa na kazi yake iwe ni kuwatafuta wenzake ambao anaona wanafaa(maana yeye ni mzoefu) na pia awe anahakikisha madereva wanaleta fedha kwa wakati(yaani wasipokutumia ww unaongea na huyo msimamizi awafuatilie kwa sababu ndio kazi yake na unamlipa). Hivyo nadhani utafanikiwa. Mm ninatumia njia hiyo na nina boda boda nyingi tu.
Pia suala la muda wa mkataba linategemea na makubaliano ya wewe pamoja na dereva wako, penda kumpa flexibility dereva ajiangalie uwezo wake wa kufanya marejesho.
Ipo ya miezi 8@15,000 per day, miezi 10@ 12,000 per day, miezi 11@ 11,000 per day na miezi 12 au wengine miezi 13@ 10,000 per day.