zunya ishile
Member
- Dec 21, 2013
- 68
- 19
wewe graduate wa finance na banking unahitaji ushauri wa kufungua banda la chips kweli?
Nilipata ajira nbc bank na ndo nipo mpaka sasa but bado ninawazo hilo maana nimekuja kuona maisha ya mshahara yanatesa duuu I never imagine!!"
mkuu ishu ya chips inalipa sana ukiwa na kiasi kizuri. Sis hapa mabibo hostel waga tunafunga safari ya zaidi ya dakika 20 kwenda kwa mtu mmoja anakiasi kizuri. Kule udom wanaendaga kwa mama mjasi mwendo wa zaidi ya nusu saa wana angalia kiasi. Tena huko tunakoenda kunaforeni nduguuuu! Kwa ujumla usitake faida kubwa taka faida! Wengi sasa wanapunja saana na kutaka faida ya kutisha matokeo yake tunawakimbia! Angalia mahali ambapo viazi vinauzwa kwa beinzuri, nasikia vya njombe ni vizuri sana
Nakushauri nenda pale namnga kwa eddo chips atakupa ushauri mzuri sana. Jamaa yupo kwenye game ya kuuza viepe kitambo sana na yupo poa sana wala sio mbinafsi.
Weka cctv na efd machine
Hesabu viazi tu...
Mpe hesabu(fixed) ambayo kila siku inabidi akukabidhi itakayoongezeka iwe ya kwake vinginevyo labda ufunge efd na cctv kwenye brain yake
Fanya hivi...
Tenga siku 2 ambazo utakua free, shinda kijiweni vijana wanapiga kazi we unakusanya pesa, then calculate the average earnings, kuanzia hapo utajua nini kinatakiwa kipatikane kwa siku, (jisemeshe kwa sauti kijana asikie- ah hii biashara nzuri sana, yani kila siku ntakua naingiza say 40'000)
Mwache kijana apige kazi, kamwe hawezi kukuibia..