Biashara ya Daladala: Ushauri na Mbinu za Uendeshaji Wake

Mkuu haya mambo ya Rifaro yana mahala pake, hapa tunaongelea biashara ya daladala.

wewe endelea kushikwa na akili na Rifaro, wajasiriamali wa kwel huanzisha biashara zao kama unavyoona hapa watu wanaongelea daladala "zao".

Wewe endelea kukesha mtandaoni ukitangaza biashara za watu, fikiria kuanzisha your own business, acha kuwa "DEIWAKA" wa RIFARO.
 
Gari ya kwanza niliinunua zanzibar mil 15,kuivusha na TRA ilikuwa 2.4 milion.,matairi mapya,road licence,Sumatra,bima na mapato,ushuru manicipal na nilinunua gari ikiwa na seat zake inazokuja nazo.,nilichofanya ni kuzisogeza mbele na kuongeza seat 1 nyuma na moja kushoto..,total weka 20,000,000
Ninachokifanya services zote nasimamia mm mwenyewe na nina fundi wangu mmoja tu.,ambaye ndio huwa nakwenda nae kuchagua gari..,Gari zang huwa zinakwenda route fupi ya km 7 tu,Nilipoanza 2010 kipande kwa siku ni 45,000 kwa cku,kwa siku 28 tzs 1,260,000 ktk fungu hili laki 6 kila mwez,lzm iingie katika akaunti maalum ya gari Nmb, inayobak namlipa dereva na matengenezo ya gari.,pia huwa inakodishwa na ina tenda ya watoto wa shule na kusambaza askri ulinz wa kampun flan katika tenda inaingiza kwa mwez inaingiza mil 2 na ushee.,sasaivi 2016 kipande ni 55,000,
Gari zang zinatumia log book.,kila siku dereva akirud lazima ajaze millage gari ilizotembe na kunikabidhi risiti ya mafuta ptinted.,na kwa siku max km ni 180.,zaidi ya hapo lazima anipe maelezo alikwenda wap.,so dereva akipata route ya nje ananijulisha na tunashauriana inalipa au la.,tena tunakubaliana analeta ya ofisi ngapi.,gari ya pili nilinunua znz kwa 18.9mil 2013 mpk inaingia barabarani ilinicost 24.8.,
Makosa yote ya barabaran yanayonihusu nalipia mm.,ila yote ya uzembe wa dereva ni juu yake mwenyewe.., na ili kupata dereva bora huwa nawanunua na kumjali kama rafiki hata nje ya kazi na mambo yote ya kifamilia ili kumfanya aithamin kazi yake
 

Nakuonea huruma sana kwa ufinyu wa fikra na uelewa wako. Nakuombea ili vizazi vyako visije kurithi uwezo wako wa kufikiri kwani ni dhahiri umeishia hapo ulipo na una tatizo kubwa la mental rut ambalo humzuia mtu kujifunza kitu kipya.

Rifaro sio biashara ya mtu mwingine. Ni yangu binafsi na nitaweza kuwarithisha warithi wangu baada ya kifo changu ili waiendeleze pale nilipoishia. Kwa mtaji wangu wa TZS 128,500 tu niliyowekeza kwenye biashara hii, nina fursa ya kutengeneza kipato cha mwezi kadri siku zinavyoenda ambacho hata ukiwa na madaladala 10 huwezi kuthubutu kunifikia.

Wewe ndio unafanya biashara ya DEIWAKA kwani kila siku lazima uwe na presha na biashara yako - traffic kakamata daladala, tairi limepasuka, dereva anaumwa, daladala limegongwa, dereva kanyonya mafuta, n.k. Mimi sina presha hizo kwani sihitaji kumuajiri mtu anifanyie biashara hii, siitaji kuisimamia kwani anaeisimamia ni kampuni ya Rifaro yenyewe kwa kunipatia ofisi yangu ndani ya mtandao yenye ripoti ya mapato yangu, wanachama waliopo kwenye mtandao wangu na mambo mengine mengi. Dakika mbili tatu kwa siku za kuongea na watu kama ninavyofanya hapa zinanitosha sana kufanya biashara hii kwa sababu hii ni Smart Business na sio biashara ya mitulinga kama ya Daladala na biashara zingine za karne ya 20.

Kwa wale ambao ni open minded na wangependa ku diversify business portfolio yao, mnakaribishwa kuangalia kuhusu mfumo na fursa iliyopo kwenye kufanya biashara hii ya Rifaro

Kwa nini utumie simu yako ya mkononi bila kulipwa wakati kuna Rifaro?
 
Hahaha

Haya Mkuu we endelea na biashara yako ya kuuza vocha....

tuache sisi tuongelee mambo ya daladala.
 

Ubarikiwe sana mkuu kwa maelezo yako mazuri sana aisee...
 
Hahaha

Haya Mkuu we endelea na biashara yako ya kuuza vocha....

tuache sisi tuongelee mambo ya daladala.

Ndio maana nikakwambia uwe open minded kabla hujahukumu. Hii sio biashara ya kuuza vocha. Mimi si mtu wa level ya kufanya biashara za kuuza vocha na kwenye thread hiyo kuna maelezo ya kina kuhusu biashara hii.
 
Ndio maana nikakwambia uwe open minded kabla hujahukumu. Hii sio biashara ya kuuza vocha. Mimi si mtu wa level ya kufanya biashara za kuuza vocha na kwenye thread hiyo kuna maelezo ya kina kuhusu biashara hii.
Mkuu tuache sisi tujadili mambo ya daladala, wewe katafute watu wa kuwaaunganisha RIFARO kwenye threads nyingine ili ujipatie hizo elfu 20 unazopata kwa kila unayemshawishi ajiunge na hiyo biashara yenu ya kuuza vocha a.k.a Rifaro.

Pia karibu katika biashara ya daladala...
 

Nimeshafanya biashara ya daladala miaka kumi na mbili iliyopita na nikaamua kuuza daladala yangu kwa sababu nilizoelezea hapo juu
 
Mkuu nmejifunza kitu... unamanage biashara yako vizuri sana; na ndo siri ya kufanikiwa. huwa unakaa na gari muda gani kabla ya kuuza?
 
Nimeshafanya biashara ya daladala miaka kumi na mbili iliyopita na nikaamua kuuza daladala yangu kwa sababu nilizoelezea hapo juu
Nini kilikushinda mkuu?

maana kuna watu nawajua walianza kama miaka tisa iliyopita from scratch na sasa wana mabus yutong dar to dodoma?

what went wrong? mismanagement??
 
Nini kilikushinda mkuu?

maana kuna watu nawajua walianza kama miaka tisa iliyopita from scratch na sasa wana mabus yutong dar to dodoma?

what went wrong? mismanagement??

Sababu zipo kwenye post niliyokujibu awali
 
Mkuu nmejifunza kitu... unamanage biashara yako vizuri sana; na ndo siri ya kufanikiwa. huwa unakaa na gari muda gani kabla ya kuuza?
Weng wananishauri niiuze ya kwanza lkn naona bado iko vzr haijaguswa engine.,cjauza hata moja.,ila sasa kuna mtu keshafika anaitaka ya kwanza kwa 20,nitakapopata ya 3,nafikiri kuiuza ya kwanza mkuu,japo nataka nijarib sasa make ya Toyota.,spare za Nissan ni pasua kichwa
 
Asante mkuu,natumai wamekuelewa wadau,umeelezea vizuri saana.
Mia siku zote huwa nasema haya mambo ya kila kitu kumlaumu Dereva wakati tatizo kubwa ni kwa maboss.
Wamiliki wengi wa magari haya wakiitwa tu maboss basi jeuri,na kuona Driver kama mtumwa tu.
Na wengi hufeli kwenye services,wapo ambao hata mpira tu anakuambia endelea kutumia huo huo.Na wengi akiba ya gari hawaweki,wanatumia pesa zoote.
Suala la kumfanya driver ndugu ndio ngao muhim saana,kwenye kazi yoyote ile.Maana hata mie kwenye Carry zangu naona faida yake.Driver anakuheshim saana,na anajua kweli unaujali utu wake na kazi yake.Usisubiri hadi driver akuambia tatizo la gari au matatizo yake binafsi,wewe mwenye jaribu kuwa karibu nae na karibu na mali yako basi itakuwa rahisi na utampa wepesi.
Drivers wengi wamekuwa waoga kusema matatizo ya gari kwa kuwa maboss wengi ni wakali,ukileta tatizo anaona kama unataka kumuibia,na driver anahofia kibarua analiacha hadi tatizo linakuwa kubwa.
 
Ni kweli Nissan nazijua vizuri sana,ni tabu sana hasa kwa Dar.
Na ndio maana hata huku Zanzibar zinakuwa bei ya chini ukilinganisha na Toyota
 
Wakuu kuna haice yangu nimeipaki ina tatizo la injini naomba mwenye kujua garama itakost sh kufanya overholl ngapi kurudi barabarani tena. Na kulipia tra, bima na Sumatra itanicost how much
 
Ushauri mzuri umetolewa kwa wanaotaka kumiliki biashara hii!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…