Hii biashara bana ina changamoto zake, ofcourse ni part ya biashara zangu kwa sasa.
Mimi naindesha hivi,
Ninazo 2, Nissan Civilian na Toyota Coaster, ambazo roughly nimezinunua kama kwa 50,000,000/= total
Kwa siku za wiki kila moja inaleta 80,000 x2 x5 = 400,000
Jumamosi ni 70,000 x 2 = 140,000
na Jumapili 60,000 x 2 = 120,000
Jumla 1,060,000 kwa wiki.
Matumizi yapo hivi.
Kila baada ya wiki 2 ni services ambayo gharama zake ni kama ifuatavyo.
Engine Oil Lita 20 = 96,500 (kila gari inakula 10Lita)
Oil Filter inaweza kua hata 36,000
Fundi 20,000
Matumizi ya kila mwezi
Msimamizi wa magari yote mawili 200,000
Hapa kuna matumizi mengine hayapo, yaani assumption ni kua kila kitu kiko poa. Hivyo sijaweka matairi, motor vehicle, TLB, bearing labda, Betrii, repair ya pasi ndogondogo n.k.
Msimamizi huyu ni mjomba wangu, na madereva + makonda katafuta yeye.
Hua napigaga tripu za kustukizia pale yanapolala kuangalia kama ni kweli yanalala saa 3-4 usiku. Maana yanaweza kua yanakesha wakakuulia gari.
Kifupi inanilipa kiasi,
Tafuta msimamizi, mlipe vizuri na jaribu kua nae karibu!!