Biashara ya Daladala: Ushauri na Mbinu za Uendeshaji Wake

Biashara ya Daladala: Ushauri na Mbinu za Uendeshaji Wake


UZOEFU: CHANGAMOTO YA MADEREVA KUTOKUWA WAAMINIFU
Nilipopata vicent nilishauriwa kuchukua daladala (Hiace) ili ifanye kazi kigamboni. kupitia JF nilifaninikiwa kuipata. Lakini kilichofuata hapo ni sawa na ndoto ya kutisha!... ukiamka hutamani usinzie tena.

Leo dereva anakwambia center-ruber imeisha, kwa hiyo badala ya Tsh 40,000 unapata 15.Kesho asbh ndo kwanza unaingia ofisini anakwambia timing belt imekatika...inatumika pesa ya jana na haitoshi inabidi utoe yako mfukoni.

Siku ya tatu na ya nne akikuhurumia ukakusanya 80 basi siku inayofuata unaambiwa nimepigwa bao na majembe. Ilikuwa nilipe 250,000 so nimewapoza 35,000. so hesabu yako mkuu hii hapa elfu tano! Gosh!!!

Picha hizo zimeendelea mpaka nikatia shaka, akipiga dereva wkt mwingine nachomoka kuthibitisha tatizo. Ajabu! Mara kadhaa ni uongo kunakuwa hakuna cha majembe wala mashoka! Bse of that nimewatimua kila nikigundua usanii huo, ndani ya mwezi 1 madereva wanne! Sasa naanza kuhisi kuwa they are probably all the same!! Na inanipunguzia concetration yangu kazini.

Baadhi ya watu wanasema ningeweza kuitumia vizuri kama nikitafuta tenda ya kubeba watoto (Nursery) na kuwa hiyo haina longolongo nyingi. Naomba ushauri wenu wakuu! Pse, pse!!
Vipi uliendelea na hii biashara?
 
Mnahangaika bure njoo garage-ni kwetu tuna madereva mafundi kabisaaa!! yaani ana vyeo viwili ni fundi na ni dereva ila mshahara wake ni mara mbili ya dereva wa kawaida!! gari ikiharibika aje garage kwetu sisi!

atachuku spana atafungua atarekebisha anavyojua yeye!...saweni ndg zangu!....ila service ni kwetu!! akipoteza uaminifu dhamana ni kwetu sisi km mkurugenzi wa garage! tunaweza weka mwingine!
 
Mnahangaika bure njoo garage-ni kwetu tuna madereva mafundi kabisaaa!! yaani ana vyeo viwili ni fundi na ni dereva ila mshahara wake ni mara mbili ya dereva wa kawaida!! gari ikiharibika aje garage kwetu sisi!

atachuku spana atafungua atarekebisha anavyojua yeye!...saweni ndg zangu!....ila service ni kwetu!! akipoteza uaminifu dhamana ni kwetu sisi km mkurugenzi wa garage! tunaweza weka mwingine!
Mnapatikana wapi na gerage yenu inaitwaje?
 
Hii biashara bana ina changamoto zake, ofcourse ni part ya biashara zangu kwa sasa.

Mimi naindesha hivi,
Ninazo 2, Nissan Civilian na Toyota Coaster, ambazo roughly nimezinunua kama kwa 50,000,000/= total

Kwa siku za wiki kila moja inaleta 80,000 x2 x5 = 400,000
Jumamosi ni 70,000 x 2 = 140,000
na Jumapili 60,000 x 2 = 120,000

Jumla 1,060,000 kwa wiki.

Matumizi yapo hivi.
Kila baada ya wiki 2 ni services ambayo gharama zake ni kama ifuatavyo.

Engine Oil Lita 20 = 96,500 (kila gari inakula 10Lita)
Oil Filter inaweza kua hata 36,000
Fundi 20,000

Matumizi ya kila mwezi
Msimamizi wa magari yote mawili 200,000

Hapa kuna matumizi mengine hayapo, yaani assumption ni kua kila kitu kiko poa. Hivyo sijaweka matairi, motor vehicle, TLB, bearing labda, Betrii, repair ya pasi ndogondogo n.k.

Msimamizi huyu ni mjomba wangu, na madereva + makonda katafuta yeye.

Hua napigaga tripu za kustukizia pale yanapolala kuangalia kama ni kweli yanalala saa 3-4 usiku. Maana yanaweza kua yanakesha wakakuulia gari.


Kifupi inanilipa kiasi,
Tafuta msimamizi, mlipe vizuri na jaribu kua nae karibu!!
Na vp kama nikiamua kuendesha mwenyew nikatafuta kondakta tu
 
Back
Top Bottom