Biashara ya Daladala: Ushauri na Mbinu za Uendeshaji Wake

Biashara ya Daladala: Ushauri na Mbinu za Uendeshaji Wake

Mm pia nipo kwenye biashara hii ya Daladala,kwa kifupi ukiogopa changamoto biashara hii utaona ni chungu sana,Ngoja ni share nanyi changamoto nilizopitia katika biashara hii,mara ya kwanza kabisa kununua hiace nikafanya taratibu zote vya vibali kisha nikaingiza barabarani gari ikafanya kazi siku mbili ya tatu ikapata ajali mbaya sana na baada ya hapo ikakaa gereji mwezi mzima niligharimu kama 1m kunyoosha bodi na mambo mengine,baada ya hapo gari ikaingia tena barabarani ikafanya kazi miezi mitatu ikaanza kula oil nikaifanyia overhaul ikagharimu kama Laki7,baada ya hapo gari ikaingia tena mzigoni ikafanya kazi miezi miwili ikanok engine ni mengi tu nayoweza kushare na ninyi lkn kwasababu ya muda naachia hapo,lkn hadi sasa nipo kwenye hii biashara ya Daladala
Hongera sana mkuu kwa upambanaji wako. Sasa hivi una daladala ngapi ?
 
Mm nipo kwenye hii biashara kitambo lkn sio sana kihivyo! Wengi wanadhani kununua gari bei kubwa ndio uzima wa gari wakati sio! unaweza ukanunua hiace 25ml na bado ikawa kimeo! Ngoja ni share jinsi mm navyoendesha biashara hii.

Kwa kifupi mm huwa sinunui hiace mpya ila nachofanya huwa nanunua bodi nzuri ya hiace kisha nafunga engine mpya pamoja na gear box yake kisha matairi mapya na service za bodi gari inasimamia 10-12ml, miezi sita tu kishaeleweka,kwa uzoefu wangu sitanunua Hiace mpya milele! Kama gari ni engine na engine complete ni 7.5ml, je ukinunua hiace 25ml ukitoa 7.5ml bodi utakuwa umenunua bei gani?

Japokuwa wapo wataoponda mchango huu lkn mm kila mwaka naona mambo yanajipa.....ni hayo2
Hongera sana mkuu, una daladala ngapi sasa hivi ?
 
Shukrani kaka kwa kunielewa!kwa kifupi biashara hii ukishapata uzoefu wa kutosha huwezi kuimba tena ule wimbo wa kuwa biashara ya magari ni pasua kichwa,wapo wanaopenda biashara lkn wanachukia changamoto!,jua ya kwamba biashara ni kama shule kuna test,mitihani na n.k,Juhudi,uvumilivu,maarifa yatakufikisha hadi kwenye ndoto yako na ndoto yako kuwa kwenye hali ya Uhasilia!
Ni kweli kabisa mkuu. Ni vema ukatupa uzoefu wako mpaka hii 2020 unaendeleaje na biashara yako ili watu wengi tujifunze kupitia wewe
 
Ipo shughuli nyingine yoyote ungeweza kufanya tofauti na kubeba abiria ukitumia hiyo Hice? Pengine umewahi kuwa na mawazo ya namna hii, labda ukaona hailipi.
Unaweza kushirikisha wadau hapa? Unaweza kuambulia different ideas usilazimike kuuza Hice.
Kabebe watoto wa shule mkuu. Haitakutupa kabisa
 
dereva wa kumpa n kitu cha kwanza kuangalia
Hili ni kweli kabuis aisee. Madereva wengi ni washenzi sana na hasa wakijua tajiri hajui magari ni rahisi sana kukulalia. Kama unataka kuiweza biashara ya daladala na ni mgeni ni vema sana uwe na usimamizi wa mtu mmoja mzoefu sana katika industry ya magari atakayekupa ethics na uzoefu wa uendeshaji wa biashara hiyo. Anaweza pia kukusaidia kutafuta watu wa kufanya kazi na wewe katika hiyo daladala na kuendelea kujifunza kutoka kwake
 
je taratibu za kukodi gari
dereva awe wa tajiri, mimi niwe kondakta
hiyo imekaaje?
 
Duh, huu uzi umejaa comments za kutisha sana kuhusu hii biashara...nimeghairisha kununua Dungu kwa ajili ya biashara hii ya daladala ambayo naikubali sana ndani ya moyo wangu ila hizo mbinde zake ndo zimenikata stim.
 
Duh, huu uzi umejaa comments za kutisha sana kuhusu hii biashara...nimeghairisha kununua Dungu kwa ajili ya biashara hii ya daladala ambayo naikubali sana ndani ya moyo wangu ila hizo mbinde zake ndo zimenikata stim.
Pambana mkuu talentboy pengine ndo kipaji chako kilipo ...afu pia sio lazima biashara hii uifanye kama wanavoifanya wengine ..unaweza ukaja na mfumo mwingine ambao ni rafiki kwako
 
Pambana mkuu talentboy pengine ndo kipaji chako kilipo ...afu pia sio lazima biashara hii uifanye kama wanavoifanya wengine ..unaweza ukaja na mfumo mwingine ambao ni rafiki kwako
Shukrani mkuu kwa kunitia moyo...ila najaribu kuchanganua na kufanya utafiti zaidi
 
Shukrani mkuu kwa kunitia moyo...ila najaribu kuchanganua na kufanya utafiti zaidi
Kweli Mkuu fanya tafiti kwanza ujiridhishe mwwnyewe then uingie ni biashara nzuri sana ila ukiingia kichwa kichwa utajuta.
Mimi iliniacha na madeni hata sina hamu, tatizo sikufanya tafiti za kutosha nilikurupuka.
 
Kweli Mkuu fanya tafiti kwanza ujiridhishe mwwnyewe then uingie ni biashara nzuri sana ila ukiingia kichwa kichwa utajuta.
Mimi iliniacha na madeni hata sina hamu, tatizo sikufanya tafiti za kutosha nilikurupuka.
duh, poa mkuu nitazingatia hilo..ila pole ndo mambo ya kutafuta yalivyo
 
Biashara ya daladala ni sawa na kufuga kuku! Kama hufugi au huendeshi mwenyewe personally, hesabu umeumia. Sasa subiri nyepesinyepesi kuwa dereva wako naye kanunua daladala, mjini hapa.
[emoji16][emoji16][emoji16][emoji16]
 
Thanks Ngalikihinja,

Nimepokea challenge ya what matters is not how much you are investing, but the returns!Kwa mtazamo huo guta linaweza kuwa na faida kuliko biashara iliyoku-cost hela nyingi tuu.

I should admit pia kuwa JF ni mahali ambapo napatumia kujifunza mambo mengi sana. Na it was JF that made me set my foot into this bussiness, ambayo honestly I do not think it is that bad. Issue ni management hasa kwa mtu amabaye unafanya monitoring kwa simu.

Mkuu I have been moved by your analyisis on biashara ya guta na mkokoteni! Tunachomiss ni knowledge or rather awareness kuhusu biashara kama hizo ambazo unaweza ku invest less na kupata return ya kueleweka tuu. Maana kupata mtu anayejihusisha na biashara ya guta/mkokoteni ili ujifunze, hilo tuu ni mtihani tosha. Mfano mdogo tuu, si rahisi ukapata thread ndani ya JF inayoongelea kitu kama hicho. May be we are underestimating them kwa sababu unachosema status ya mtaani.

So far, mchango wako wa mawazo na changamoto imepokelewa! Thanks!!
[emoji1666][emoji1666]
 
Back
Top Bottom