Biashara ya Duka la Rejareja: Ushauri, Mchanganuo, Changamoto na Namna ya Kutunza Kumbukumbu

Biashara ya Duka la Rejareja: Ushauri, Mchanganuo, Changamoto na Namna ya Kutunza Kumbukumbu

Kijana Mimi binafsi huko sipa faham vizur ila Ni mwenyeji wa k'njaro na Dar hata mikoa mingne pia tofaut na huko.

WAZO LANGU KWAKO
Mahali kama hapa Dar, una weza anzisha hata saluni mbili kwa hela yako Hiyo
Una Fanya hvi,, unafungua ofisi ya kawaida sana maana saiv vyuma vime kaza kwahyo watu wengi hawapendi Kwenye saluni za gharama sana.....
Tafuta vijana uwaweke pale kila siku wana kulipa wewe eg 9000@ saluni moja,, ambapo una kuta Ni 18000 kwa siku hebu piga Mara wki then Mara mwezi, hhehehehheh,, hata Bachelors' holder haku fuati hata kidogo

Faida ya hii biashara
1. Una kua free kufanya mambo mengne.
2. Hakuna kinacho oza hapo kama biashara ya nyanya.
3. Na zingine nyingiii.

NB.Nina experience 100% so kama una swal au kama Kuna mwingne ambae pia ana mtaji wake na Yupo interested kufanya hyo biashara ana ruhusiwa kuuliza chochote
0763885349

Asante mkuu kwa wazo lako but tunaomba mchanganuo wake,i mean wap napata mashine za kunyolea,bei yake ipi ni nzuri na imara, vifaa gan muhimu napaswa kuwa navyo hapo na gharama zake na kadhalika
 
Ni sahihi,, ila sasa kama Uko na uhitaji weka no yako Nita kupigia au Ni text
 
asante mkuu kwa wazo lako but tunaomba mchanganuo wake,i mean wap napata mashine za kunyolea,bei yake ipi ni nzuri na imara, vifaa gan muhimu napaswa kuwa navyo hapo na gharama zake na kadhalika
Ni sahihi,,ila sasa kama Uko na uhitaji weka no yako au nitext
 
sio vitisho mkuu ni real..... ina faida ndogo sana ukizingatia pango sijui uweke hela ya umeme, then ukute umemweka mfanyakazi au pengine unakaa mwenyewe.... pia kinachofanya hii biashara iwe ngumu ni mchuano, yani unakuta mwenzio ana duka jiran na wewe atashusha bei ili apate wateja wengi, wewe ukisema unamuiga inakula kwako, kwa staili hii nishaona biashara nyingi sana zimekufa. ebu chukulia umenunua juice catoni moja (juice za mo), bei yake ni 5000 mpaka 5200, na zinakaa 12, hapo kwa haraka haraka unatakiwa uuze moja 600, lakini jirani yako anauza 500 akilenga kupata faida ya 1000 au 800 kwa catoni moja. je unadhani hii faida inakidhi ? hapo hatujaweka gharama za umeme wako, pia pengine mzigo unachukulia mbali kidogo umemlipa bodaoda au mwendesha mkokoteni , je hapo kuna kitu tena ? nadhani umeelewa kitu hapo, alafu watz tulio wengi mtu akipata hela kdg anawaza kufungua duka tu hawazi kingine, kuna biashara kama genge zinalipa sana mtu ukipata senta nzuri
Mkuu hii biashara unaijua vizuri nimekukubali, sema ndugu yangu hakuna biashara rahisi. Kwa mfano hyo ya genge nayo ni pasua kichwa kinoma. Vitu vinaharibika sana usipokua na wateja wa kutosha.
 
Aisee, huo mtaji wako ni wa genge wala si duka la reja reja.

Nakushauri,kama unataka kufanya biashara ya mtaji huo wa 1,000,000 basi usikodi kwanza duka,usijisajili TRA, ajiri kijana kwa ujira mdogo ikiwezekana ishi naye.

Vinginevo imekula kwako
 
Ni sahihi,,ila sasa kama Uko na uhitaji weka no yako au nitext
kwasasa nimeishiwa chaj mkuu ila ukini pm cont itapendeza zaid. sikuwa na wazo la kuanza hyo biashara lkn maelezo yako yamenifanya niwe interested
 
Ukipata eneo lenye makazi ya watu wa kipato kidogo na cha kati.

Hawa maisha hayaendi bila sukari, mafuta ya kula, ya kujipaka, unga wa sembe, ngano, maharage mchele, karanga, vocha, soda, bia, mikate, nk.

Ikipita siku hujauza hivyo vitu, basi kuna shida
Na hizi biashara ndio sehem zake, yani mtu hawezi kununua bidhaaa ya mwez ikae ndani. Yeye daily lazima azame shop.
 
Habari wadau,

Leo nizungumzie kidogo kuhusu boashara ya reja reja ya maduka ya bidhaa za matumizi ya nyumbani kama mchele,unga sabuni,nakadhalika.

Unapotaka kufungua aina hii ya duka ni lazima kwanza utambue eneo unalotaka kufungua je ni eneo la watu wenye kipato au watu wa hali ya chini,je ni eneo lenye mzunguko wa watu ni eneo ambalo halina mzunguko wa watu.

Kwa sababu za kiuchumi huku kwetu Super market culture bado haijakuwa vizuri kwa hiyo basi maduka haya yanauza sana.Unapotaka kufungua biashara hii haya ni baadhi ya mambo ya kuzingatia.
  1. Kodi ya fremu ya duka la reja reja yapaswa kuanzia shilingi 30,000 kwa mwezi hadi shilingi 150,000 kwa mwezi iwapo imazidi hapo ni lazima uwe na hakika kuwa eneo lina mzunguko wa uhakika.
  2. Leseni ya duka la rejareja ni kati ya shilingi 50,000 hadi 200,000
  3. Kodi kwa duka la rejareja inayolipwa TRA inaanzia shilingi 300,000 kwa mwaka kutegemea na makadirio ya mapato yako
  4. Kuna vitu vya aina mbili katika duka la rejareja,kwanza ni vitu vya kupima ambavyo ni muhimu zaidi kama vile unga,mchele,mafuta taa,maharagwe n.k.hivi unaweza kuviwekea mtaji wakuanzi shilingi 450,000 hadi shilingi 900,000 kutegemea kiasi na uwezo na pili ni vitu ambavyo si vya kupima mwenye kama vile sabuni,mafuta ya kupikia,sabuni za unga,sabuni za kuoga,lotions na mafuta ya kupaka,dawa za mswaki,viberiti,stili waya,mishumaa,soda,maji na vifaa vidogo vidogo.Hivi unaweza kuviwekea mtaji wa kati ya shilingi 600,000 na 1,500,000
  5. Kama una uwezo ongeza huduma za Mpesa,na uuzaji wa LUKU
  6. Unaweza kuhitaji kuwa na FRIJI,MIZANI,MASHINE YA KUUZA LUKU ambavyo unaweza kuvitengea mtaji wa angalau TZS 1,500,000
Jambo la muhimu katika duka la rejareja ni kuhakikisha kuwa unaweka kumbukumbu za manunuzi na mauzo ya kila siku na kama unaweza kufunga stock basi funga stock kila baada ya miezi mitatu au unaweza kufunga stock kwa kuchagua upande wa duka yaani,vitu vya kupima peke yake na vitu vya mashelfu peke yake. Vile vile hakikisha unaweka mtu muaminifu unamfuatailia hasa kwenye mauzo na iwapo unasimamia mwenyewe usipende kutoa pesa za dukani kwa matumizi ya nje bila kujua katika mauzo hayo faida yako ni kiasi gani.

Kwa kawaida vitu vingi vya dukani profit margin yake ni ndogo sana hivyo kwa ajili ya makadiria weka margin ya 0.5 % mpaka 5% na hapo utajua iwapo mauzo yako yanakupa faida kiasi gani.

Tuendelee na mjadala
Safi sana kamanda tunavuna elimu na ujuz mkuu.
 
Kijana Mimi binafsi huko sipa faham vizur ila Ni mwenyeji wa k'njaro na Dar hata mikoa mingne pia tofaut na huko.

WAZO LANGU KWAKO
Mahali kama hapa Dar, una weza anzisha hata saluni mbili kwa hela yako Hiyo
Una Fanya hvi,, unafungua ofisi ya kawaida sana maana saiv vyuma vime kaza kwahyo watu wengi hawapendi Kwenye saluni za gharama sana.
Tafuta vijana uwaweke pale kila siku wana kulipa wewe eg 9000@ saluni moja,, ambapo una kuta Ni 18000 kwa siku,, hebu piga Mara wki then Mara mwezi,, hhehehehheh,, hata Bachelors' holder haku fuati hata kidogo,,

Faida ya hii biashara.
1. Una kua free kufanya mambo mengne.
2. Hakuna kinacho oza hapo kama biashara ya nyanya.
3. Na zingine nyingiii.
NB: Nina experience 100% so kama una swal au kama Kuna mwingne ambae pia ana mtaji wake na Yupo interested kufanya hyo biashara ana ruhusiwa kuuliza chochote
0763885349
Kaka sijakuelewa kuuliza kuhusu saluni au biashara ya rejareja.
 
HIV haya maduka ya uswahilin mbona wansema pesa huwa zinapotea kiajabu ajabu je kuna ukweli hapo na kama itakua kwel dawa ni ipi
 
Habari zenu wakuu,

Nimetafuta ajira sana ila sijafanikiwa, nimeona nijiajiri, kuna biashara imenivutia ya kuweka kibanda maeneo ya stand au ktk vituo vya daladala, mf wa bidhaa kama maji, pipi, juice n.k.

Linakuwa kama duka la rejareja dogo, swali langu kwenu wakuu ni wapi kwa hapa Dar kwenye mzunguko wa watu wengi na ninapoweza pata nafasi ya kuweka kibanda hicho ambacho kwa baadaye naweza weka na M-Pesa.
 
Wewe una ishi wapi kwanza. Mana unaweza kuweka kibanda mwenge arafu wewe una ishi mbagala au kibaha mwisho wa siku nusu na robo ya faida ina kuwa ina ishia njiani. Kwenye kugharamia usafiri na mambo mengine
 
Wewe una ishi wapi kwanza. Mana unaweza kuweka kibanda mwenge arafu wewe una ishi mbagala au kibaha mwisho wa siku nusu na robo ya faida ina kuwa ina ishia njiani. Kwenye kugharamia usafiri na mambo mengine
Naishi Mbagala mkuu ila umbali si tatizo naweza hamia karibu na eneo endapo, biashara ni nzuri.
 
Back
Top Bottom