Biashara ya hardware kwa mtaji wa mil.7

Biashara ya hardware kwa mtaji wa mil.7

Kabla sjakushauri naomba kukuuliza hizo hela ulizo nazo ndo utategeme maitaji yote hapo hapo au una vyanzo vingine vya uhakika vinavyokuingizia kipato?
Nilivyomuelewa kasema huo ndio mtaji tu

Lakini mbona huo unatosha kwa kuanzia tu afungue pembeni watu wanakojenga sana fano Bunju kwandani, Goba, Mbezi juu, Makongo, Chanika lakini azame ndani zaidi
 
Huo mtaji mkubwa inatakiwa atafue uchocholo wanakojenga sana mbona atauza tu hasa wajengaji wadogo wadogo
Biashara ukianza kwa ukubwa itawavutia wateja na watajihisi kama wapo kwa mkulima vile watapata kingi kwa bei nafuu lakini ukianza kwa uchache wateja watahisi utawapunja tu hawatakuja hiyo nilio mshauri na mtaji alionao ataweza kuifanya hiyo biashara kwa ukubwa zaidi tofauti na hiyo ya hardware
 
Na mimi natamani kuanzisha biashara ya spear mtaji ninao kama m5 ila siwezi kukaa sehemu moja kusubili wateja na wahudumu ni pasua vichwa maana mimi nadeal na biashara ya mazao kwa sasa
Inategemea maeneo uliyopo, unaweza kufungua hardware ndogo ukaikuza taratibu, ila uwe na adabu faida irudi dukani mpaka mtaji ukue.

Yupo rafiki yangu alifungua duka la spear na milioni 3 saivi zinakimbilia 15, disciple ndo kila kitu.

Wanaokuambia pesa ni kidogo waambie wakuongezee.
ninao
 
Kwa hardware hiyo pesa ni chache tafuta frame maeneo yaliyochangamka kama maeneo ya stend au sokoni na uuze simu za batani na smart phone za kuanzia 100k mpaka 280k uweke na vifaa vya simu na vitu vidogo vidogo vya electronic kama Bluetooth speaker na vingine vidogo vidogo pesa ikibaki unaweza ukaweka na huduma ya M-pesa. Note usiweke pesa yote kwenye biashara utafeli
Thx
 
Usikate tamaa mimi nilianza na mataji ulio Chini ya hapo nilianza na kuuza cement tu vitu vingine niliendelea na naendelea kuongeza hadi saiv
Sorry mkuu cement za jumla uklikua unaenda kufata kiwandani au wap na je mashart yapoje kuanzia kiasi gan ndio unatakiwa kufunga mzigo kiwandan,pia kama unauzowefu Gypsum board za jumla nazo natakiwa ninunue za kias gan ili niweze kuweka dukan
 
Usikate tamaa mimi nilianza na mataji ulio Chini ya hapo nilianza na kuuza cement tu vitu vingine niliendelea na naendelea kuongeza hadi saiv
Nina mpango kama wako.....cement kila mfuko nimeona unapata kati ya shs 500- 800
 
Sorry mkuu cement za jumla uklikua unaenda kufata kiwandani au wap na je mashart yapoje kuanzia kiasi gan ndio unatakiwa kufunga mzigo kiwandan,pia kama unauzowefu Gypsum board za jumla nazo natakiwa ninunue za kias gan ili niweze kuweka dukan
Inafatana na eneo ulilopo mimi nipo mbeya kuna watu wanaosambaza nilianza na cement 100, gypsum board uwa nanunua dar maduka tofauti tofauti kuna 92hardware, shananga group, datina building, fmj hardware
 
Inafatana na eneo ulilopo mimi nipo mbeya kuna watu wanaosambaza nilianza na cement 100, gypsum board uwa nanunua dar maduka tofauti tofauti kuna 92hardware, shananga group, datina building, fmj hardware
Mpaka saiv sijafikia hatuna ya kwenda kuchukua kiwandani nachukua kwa mawakala sababu kiwandani kuna kuwa na foleni ndefu, na gharama zake hazipishani sana ukichukulia kwa mawakala, uhakika zaidi wa kiwandani uwe na gari yako ya kwenda kubeba semi inabeba cement 650 kwa uku kwetu inagharimu kama million 11
 
Inafatana na eneo ulilopo mimi nipo mbeya kuna watu wanaosambaza nilianza na cement 100, gypsum board uwa nanunua dar maduka tofauti tofauti kuna 92hardware, shananga group, datina building, fmj hardware
Nipe namba A92 hardware mkuu nahitaji jipysum za shine shine
 
Gypsum kwa bei ya jumla huwa wanauza kiasi gan mkuu na ili uweze kuuziwa kwa jumla unatakiwa uwanze na kias gan
Hata 10 unauziwa ila fanya utafiti wa bei zilizopo sokoni kwako, kisha wapigie simu ujue bei zao
 
Back
Top Bottom