Mkuu mi ninakushauri huo mtaji utenge katika mafungu kadhaa.
Tenga milioni 100, tafuta kiwanja/viwanja katika mji wa kiserikali au kibiashara (sio lazima uwe mji mkubwa sana) jenga apartment hata 2 kwa ajili ya kupangisha
Mil. 30, weka hardware maeneo ya miji inayojengeka kwa sasa
Mil. 30 wekeza kwenye biashara ya kununua na kuuza viwanja
Mil. 20 weka benki ya saving, kusubiri mchongo wowote (kumbuka kuna kipindi unaweza letewa mchongo wa maana kwa bei ya chini kwa kuwa muuzaji ana shida sana ya hela)
Mil. 20 iliyobaki iwepo kwa ajili ya back up endapo kuna shida itajitokeza kwenye business nyingine
Sikushauri uwekeze kwenye
1. Kilimo kama huna mzuka na kilimo na kama hujawahi kulima
2. Kwenye madini (kimbia kabisa)
3. Fixed account