Biashara ya Kununua na Kuuza Mazao (nafaka): Jifunze Mbinu za Kuanzisha na Kusimamia

Hakuna biashara mbaya kwa uchumi wa sasa kama kumkabidhi dalali mzigo wako tena wenye thamani ya 15 ml then uje kuchukua pesa after sijui 2 days mkuu acha kabisa hii kitu nenda sokoni mwenyewe epuka dalali utafilisika

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu inshort kama mm nishafanya biashara ya mahindi mkuu nilikuwa nayatoa mbozi mlowo nayaleta iringa nasaga na kufunga mifuko ya kg 5 , 10, 25 na kimsingi nilifanikiwa kwa kiasi kikubwa nilipata watu wa kuwasambazia hizo sembe tena kwa bei za jumla mkuu sasa kwa ww kama upo Dar nenda tandale pale kuna mashine nyingi sana za kuzalisha sembe pia kuna wateja wengi sana pale wananunua mahindi kama nafaka incase ukiona kuyasaga mwenyewe ni ngumu nenda pia kuna mashine zipo hapo tandale zinanunua mahindi au unaweza kwenda na mahindi yako ukayasaga ukafungishiwa kwe viroba ukaubeba unga wako incase una wateja lkn pia kama hauna wateja unaweza kuwauzia wao pia wananunua then hii kitu kwa sasa haihitaji mtaji mkubwa insuch way hata mil 4 au 5 utafanya kazi vzuri tu mkuu.

Kikubwa jua haya masoko ya tunduma na mbozi mahindi roba la debe sita ni 24000. Na usafiri tani moja kutoka mbozi mpaka dar almost huwa 60000 atleast nimetoa mwanga kidogo na kwa ufupi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Weka mbali pesa/biashara yako na dalali hasa zama hizi za unlce hawafai. Kwanza ingekuwa ni idhini yangu ningepiga marufuku kabisa biashara ya dalali hawa ndio wanaofilisi wakulima na wafanyabiashara maana wao kama vile ndio wamekamata soko. Inakera. I HATE DALALIS!!
 
Ndugu zangu wana JF mimi ni mwanachuo mwaka wa pili hapa dsm ninapenda sana kufanya biashara lakini nabanwa na mda sana nitumie fursa hii kuwaomba ndugu zangu mchango wa mawazo ni kitu gani ninaweza kufanya na bado nikaendelea na masomo yangu ninao mtaji wa laki saba 700,000/= tafadhali msaada jamani ninafikilia sana juu ya nini nifanye mpaka kichwa kinauma sasa kwa kuwa naamini wapo watu creative ndani ya jammiiforum watanisaidia mchango wa mawazo na ni kitu kipi nifanye kulingana na hali yangu ya uanafunzi.
 
Ni vzr ukaanzisha uzi wako itakuwa rahisi kuonekana
 
Kifupi kipindi hichi biashara ya kununua na kuuza tafuta mazao ambayo kweli yana shida katika upatikanaji wake. Achana na mahindi kabisa na hata kama utaamua kununua mahindi nunua na saga mwenyewe fanya packaging peleka mzigo sokoni kama unga hapo ndio utaona faida yake maana mahindi yapo mengi sana na inafika mahali watu hawana mahali pa kuyapeleka jaribu kuangalia miaka ya nyuma miezi kama hii ,mahindi yalikuwa juu sana ki bei hayo mahindi ya tunduma miaka ya nyuma miezi hii yalikua gunia ni 52000, sasa ukiangalia kutoka hiyo amount mpaka 24000.. jua hapo hakuna biashara.
 
Shika moja kwanza. Maliza masomo,haraka ya nini? Biashara zipo tuu siku zote.
 
Kwa mfano mahindi kuyanunua na kuyahifadhi kusubiria bei iwe nzuri alafu unayauza baadae,naomba muongozokwa aliyewahi ifanya
 
Mahindi tumevuna ziada ya zaidi ya tani milioni moja msimu uliopita. Mpaka hii surplus iishe ndipo bei zipande, sio leo...
Mahindi sio zao zuri, kwa sasa. Utakuja kukaa nayo ndani miaka mitatu na bei zisipande. Jaribu mazao mengine kama ufuta na alizeti.

Mazao yanayoharibika mapema kama nyanya, vitunguu, mihogo sio biashara ya kufanya kama hutaki kupata ugonjwa wa moyo!
 
Ninampango wa kuanzisha biashara ya mchele dar naomba kujua n mahali gan kunaeza kua na mzunguko mkubwa, garama na mtaji pia.
 
Ninampango wa kuanzisha biashara ya mchele dar naomba kujua n mahali gan kunaeza kua na mzunguko mkubwa,garama na mtaji pia

una pesa Cash kiasi gani.!? kama mtaji
 
Habari wakuu.

Wakuu Mimi nimenunua mpunga almost gunia 500 zipo store huku Mbeya sido, sasa wakuu ningeomba mnisaidie yafuatayo:

1. Ni kuanzia mwezi wa ngapi bei utakuwa inafaa kutoka mzigo wangu na kuuza kwa faida

2. Mwenye uzoefu na hii biashara anisaidie kunipa elimu jinsi ya kuwapata wateja wa mchele ili niweze kuuza mchele wangu

Natanguliza shukrani zangu za dhati kwa wale wote mtakao nisaidia kushare information nami

Mungu awabariki sana

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…