Biashara ya Kununua na Kuuza Mazao (nafaka): Jifunze Mbinu za Kuanzisha na Kusimamia

Watu kama ninyi ndio mnasababisha watu wachome mitaji,

Mtaji wa laki nne unamshauri stoke mwanza aende kariakoo kuchukua mzigo?

Au unataka kumtapeli huyu dada? Isijekuwa umekaa na mzigo wako huko hujauza unataka kumshikisha dada wa watu?

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Kila kiumbe anapoishi lazima awe na plan B Kwan Kaka hapo nimeeleza toka nimejitambua na nimeanza kujitafutia maisha hiyo ndiyo kazi yangu ya kwanza ama pekee

Kwa kifupi tu nikueleweshe maishan mwangu sichagui kazi nimeuza Sana vitafunwa bagia chapati maaandazi kwa kutembeza nimezunguka kwenye mashule kutafuta tenda za t-shirt ambazo nanunua napeleka wenye mashine quality naprint Kisha mzigo unaenda sehemu husika na hapo naishi kwa Mali kauli ikitokea shule wameelewa maneno na wameniamini wanatoa advance (ambayo napigia gharama zote mpka mzigo kukamilika) napiga kazi ikitimia naenda kuchukua kiasi kilichobaki ambacho ni faida

Pia nimekua mpigadebe kwenye mabusi ya mikoani so akili ya maisha ipo kiasi furan ndo maana nimesema napenda maisha mazuri sababu naangaika kutafuta pesa.

Kuweka akiba ndio azina yangu

Hope umenielewa
 
Hongera ni wazo zuri Sana Asante, nimesoma chuo Cha T.I.A hapo na izo biashara nimefanya Sana ni nzur mno

Asante pambana utafika
 
Hizi akili nyingine bwana!!sasa wafanyakazi wa dangote, au bakhresa wakiwa wanapigia hesabu wanachoingiza na malipo yao si wangezimia woteee?!!huyo dada kwa mawazo hayo hawezi hata kufanya biashara!!
Asantee kila mtu ananamna anavyowaza ata uyo bakhresa asingewaza mbele sizan Kama angefika hapo aliwaza mbele na ni vipi angefika na ndio maana Leo yupo alipo na ww umemtumia Kama mfano
 
Hizi akili nyingine bwana!!sasa wafanyakazi wa dangote, au bakhresa wakiwa wanapigia hesabu wanachoingiza na malipo yao si wangezimia woteee?!!huyo dada kwa mawazo hayo hawezi hata kufanya biashara!!
Ndio maana darasan kukawa na mtu wa kwanza na wamwisho akuna asie na akili Bali ni namna ya kuzitumia
 
Asantee kila mtu ananamna anavyowaza ata uyo bakhresa asingewaza mbele sizan Kama angefika hapo aliwaza mbele na ni vipi angefika na ndio maana Leo yupo alipo na ww umemtumia Kama mfano
Hujanielewa!!sijamanisha kuwa na mtizamo wa kuanzisha biashara yako, ni mbaya!!nilichokataa ni kusema kuwa eti yeye anaingiza pesa kiasi fulani mimi ananipa 130, 000!! Nikasema ukiwa na mawazo hayo huwezi fanya kazi kwa mtu , bora uwe na mawazo ya kufanya mwenyewe!!hiyo unayoina kama fedha anayoipata , kuna TURNOVER, GROSS PROFIT, Halafu ndio uje kwwnye NET PROFIT, unawez usiamini anachobakia nacho!!kwakuwa unawazo la kufanya biashara kila raheli utakuja yaona hayo!!na wewe ukifanikiwa kuwa na mfanyakazi, atauza mauzo ya laki 3, kwa siku ukimwambia nitakuwa nakulipa 3000 kwa siku ataona kuwa unampunja, yaani 300, 000 yeye umpe 3000?!!kumbe kwenye hayo mauzo, faida yako halisi ni 15, 000!
 
Hiyo biashara ni nzuri sana mikoa ya Pwani, hasa wilaya ya Kilwa, na Lindi yenyewe, watu wa kule n wavivu hawawez kazi, kazi ni kuvua tu kila kitu wanahemea dukani.
 
Naifaham BUHONGWA vzr sana kibiashara. ni mahali nilipozaliwa na nikakulia hapo na nikafanya biashara hapo. Kwanza dada naomba usikatishwe tamaa na watu iwapo kweli umekata shauri kuingia kwenye biashara....
Nilipomaliza Chuo (2018) nilirudi nyumbani Buhongwa nikamkuta mdogo wangu ambae elim yake ilikua ni form 4 (tena mtihani hakufanya) ndio kawa mhimili wa familia, I mean ndio alikua akilisha familia kwa biashara hiyohiyo ya MCHELE alikua akiuzia BUHONGWA... nilikaa nikaongea nae alinieleza kua alianza na mtaji wa laki mbili tu (200000), bahati nzuri mzani ulikuepo nyumbani. Alikua anaenda vijiji vya wilaya ya misungwi kwenye mashine za kukoboa mpunga ananunua mchele hata kilo mia mbili analeta buhongwa, jioni anapeleka pale stand kuuza na anamaliza siku hiyo hiyo au kesho yake mapema tu....
Ninavozungumza hivi sasa japokua nilimuacha nyumbani mm nikaenda kufungua salon ya dreads rock city mall lakin anamaendelea makubwa tu, kanunua viwanja na vitu vingine ingi kafanya pale nyumbani...

Sasa kama yeye aliweza akiwa na laki mbili kwa nn ww ambae una laki nne ushindwe? Sidhani kama kuna mahali hapa mwanza ambapo pamechangamka kibiashara (kwa mitaji ya kawaida laki moja mpaka mil 3) kama buhongwa, biashara ya juice unayoifikiria nimeifanya sana hapo buhongwa na nilikua napiga faida kwa siku sio chini ya 10000 tena sitembezi mm nilikua nampa dogo flani ananitembezea alafu nampa 2000.... so biashara zote hizo mbili unazozifikiria kwa buhongwa zinafanyika vzr sana watu wasikukatishe tamaa....

Sio lazima ununue mzani dada angu, kuna watu wanakodisha mizani unalipa kwa siku au wiki. BUHONGWA ni sehm yenye mkusanyiko mkubwa sana wa watu kwa kata za mwanza ikifuatiw na igoma, hvyo biashara ziazohusu vyakula, nafaka

KILA LAKHERI
 
Yaan Kati ya watu walionielewa vizuri kabisa Kaka we ni wakwanza kabisaaaaaa
 
Dah.. sijawai kuwa tapeli na sijawai mtapeli yeyote chini ya jua..

Nmesema aje ili aelewe na A B C za huku, tatizo linatoka wapi Ostadhi?
 
Dah.. sijawai kuwa tapeli na sijawai mtapeli yeyote chini ya jua..

Nmesema aje ili aelewe na A B C za huku, tatizo linatoka wapi Ostadhi?
Usijali Kaka kila kitu kina mapokeo tofauti kulingana na nini mtu anawaza ama kufikiria, pia isitoshe ndugu yetu katoa wazo akifikilia mbali zaidi maana najua nawe unaelewa namna utapeli wa kimtandao unakua kwa Kasi usiku na mchana .
 
Usijar Kaka kila kitu kinamapokeo tofauti kulingana na nn mtu anawaza ama kufikiria, pia isitoshe ndugu yetu katoa wazo akifikilia mbali zaidi maana najua nawe unaelewa namna utapeli wa kimtandao unakua kwa Kasi usiku na mchana .
 
Jenga maize/storage tank la chuma au anything kama la tani 50 au 100 au zaidi ( yapo Alibaba au mafundi wanaweza kukutengenezea), mahindi wakati wa mavuno yanakuwa bei rahisi sana karibu na bure nunua yahifadhi then kiangazi kikifika au mahindi yakipanda bei uanaachia mzigo sokoni, utatengeneza pesa kirahisi sana ila inahitaji mtaji mkubwa kidogo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…