Biashara ya Kuonesha Mpira wa Miguu (Kibanda-umiza): Fahamu Kiasi cha Mtaji, Vifaa na Mbinu za Uendeshaji

David webb

Senior Member
Joined
Nov 20, 2011
Posts
159
Reaction score
84

Wanandugu, naombeni msaada tafadhali.

Mimi ni kijana mwenzenu nimebahatika kuchanga pesa zangu na nimefanikiwa kupata milioni moja na nusu; nataka kufungua biashara ya kuonesha mpira kwa jijini Dar (hasa mpira wa Ligi Kuu ya Uingereza). Je, vipi ni biashara nzuri kufanya au niachane nayo nifikirie kingine cha kufanya?

Wadau naombeni msaada wetu please. Kufanikiwa kwa hili ndo mwanzo wa biashara nyingine.

Asante, natanguliza shukrani.

Wenu mdau katika JamiiForums

WADAU WENGINE WANAOHITAJI UELEWA WA BIASHARA HII
Tafadhali wale wenye uelewa kuhusu hii biashara watujuze, hasa kuhusu taratibu zake na kampuni za TV zenye haki ya kurusha mechi hizo kama azam TV na DSTV.
Kwenye hyo milion 2 nahitaji Screen 1 kubwa, projector na king'amuzi cha DSTV chenye uwezo wa kuonesha mechi mbili kwa pamoja. Je kwa mtahi huo nitaweza?
Nahitaji mwongozo kwa anayefahamu hii biashara. Nampango wa kufungua banda la mpira Tabora ila uhalisia wa vitu muhimu kwenye hii biashara ndo sifahamu kama gharama za kufungua banda,faida na hasara zake.Ahsanteni


MAJIBU NA MICHANGO MBALIMBALI YA WADAU
 
Nini malengo ya hiyo biashara unayotaka kufanya? You want to make life or you want to make changes.
 
Kaka andaa vijana wawili utakaofanya nao kazi wawe good movie wachers nitakupa idea Nadhani itafunction.
 
Hiyo biashara tafuta kuweka kwenye eneo lenye umati wa watu wasio na uwezo wa kufunga dstv. zaidi uswazi. Screen iwe kubwa iwezekanavyo na clear kabisa bila chenga.

Funga DSTV na uweke viti au mabenchi ya kutosha. Premier League itakuingizia hela. Kama upo uswazi wakati hamna ligi utapata hela kwenye video za movies
 
Wadau nilikuwa na wazo la kununua Projector na satelite dish ili kuonyesha mipira ya ulaya ninaeneo langu kubwa linaweza kuingiza watu mia mbili naombeni msaada wa kujua gharama ya projector na satelite dish nianze hii biashara kwa yoyote mwenye uzoefu na biashara hii anisaidie kunipa ushauri zaid ni vitu gan vya kuongeza hapo.

Nawatakia mafanikio mema wote ndan ya mwaka huu Mungu awe pamoja nanyi. Nasubiri msaada wa mawazo yenu.
 
Dstv kila kitu ukilipia kwa hapa bongo dar es salaam ni kama laki 2 na elf 80 kama sijasahau, hapo unakua pia umelipia kuona machannel yote ya mipira na kila kitu dish na fundi wa kukuwekea dishi na pia king'amuzi na nini na nini na kila kitu.

Kila mwezi gharama ni shs 129,000 kuona machannel yote yenye mupira. Uonyeshe hata video ikiwezekana si unajua mambo ya vibanda umiza? ili upapate pate na pesa za ziada.
 
Itakuwa zaidi ya laki tatu kwani kama unaonesha mpira wenye uwezo wa channel 3 kwa wakati mmoja au wanaita commercial package ni dolla 115 kwa mwezi. king'amzi na package zake ikiwemo ufundi ndani ya radius ya 10km ni kama Tshs 135,000. hivo kwa kuanza unahitaji takribani laki 400,000.
 
Hivi hii biashara bado inauzika, kweli Tanzania ni kubwa, maana huku kwetu Mpitimbi watu wanaonesha mpira kwenye Bar kiingilio bia yako; unaonaje hilo eneo ukifungua bar ukawa unaonesha mpira ligi zote kubwa! Ni wazo tu mkuu.
 

Ubarikiwa mkuu nitafuata maelekezo yako.
 

Shukrani ubarikiwe mkuu.
 
Mawazo mazuri, kwa siku ambazo hakuna mpira onyesha movie asa ambazo zimetafsiliwa kiswahili na Mkandala

Ahsante na hilo ndilo lengo langu pia kuonyesha picha za Kaptain Gasper Mkandala Lufufu ahahaha hahaha kumbe unajua watu wanampenda huyu mjasiliamali eeeh kwan nimefikiri hvyo kutokana na wengi uswahilini kwetu wanapenda kukodi mikanda yake na wanakosa pa kuangalia mpira.
 
Hivi hii biashara bado inauzika, kweli Tanzania ni kubwa, maana huku kwetu Mpitimbi watu wanaonesha mpira kwenye Bar kiingilio bia yako; unaonaje hilo eneo ukifungua bar ukawa unaonesha mpira ligi zote kubwa! Ni wazo tu mkuu.

Wazo zuri nitalifanyia kazi mkuu shukrani ubarikiwe
 
Mkuu Tripo9

Endapo kama unatumia satelite dish inayotumia ving'amuzi vya Free to Air(FTA channel) kama Media com au strong vp matangazo ya mpira pale siwezi kupata free au kama ni ya kulipia naweza kupata kwa kiasi gani?
 
Wadau nashukuru kwa maon yenu nakaribisha mwenye maoni pamoja na ushauri kuhusu aina ya projector na ubora wake ninayoweza kutumia kwa shughul hii
 
Kama ni EPL na unatumia dstv wakijua unaweza kufungwa.

Labda utumie Arab sat etcl
 
Nakushauri ufungue bar ambapo pia utakuwa unaonyesha mpira ligi mbalimbali, namaanisha biashara yako kubwa iwe ni hiyo ya bar na mpira iwe ni njia tu ya kuwavutia wateja, lakini hakikisha kila anayeingia hapo ananunua kinywaji ikiwezekana kwa kuwauzia coupons mlangoni wakati wa kuingia ambazo zitatumika kulipia vinywaji.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…